< Sprueche 6 >

1 Mein Sohn! Hast du für deinen Nächsten dich verbürgt, hast Handschlag du für einen anderen gegeben,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 bist du verstrickt durch deines Mundes Reden, durch deines Mundes Worte selbst gefangen,
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 dann, Sohn, sieh zu, daß du dich rettest, da du doch in die Hand des Nächsten eingeschlagen: Geh ohne Säumen hin! Bestürme deinen Nächsten!
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 Gönn deinen Augen keinen Schlaf, nicht deinen Augenwimpern Schlummer!
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Errette dich gleich der Gazelle aus der Schlinge, gleich einem Vogel aus des Fängers Hand!
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Zur Ameise, du Fauler, geh, schau ihre Art und werde klug
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 durch sie die keinen Fürsten hat, nicht Amtmann, nicht Gebieter,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 sie, die im Sommer schon ihr Brot bereitet und in der Ernte ihre Speise sammelt!
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 Wie lange, Fauler, willst du liegen? Wann willst du dich vom Schlaf erheben?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 "Ach noch ein wenig Schlaf, ein wenig Schlummer, ein wenig noch die Hände ineinander legen, um zu ruhen!"
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 Schon kommt die Armut über dich, gleich der des Strolches, und Mangel gleich dem eines Bettlers.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 Ein Teufelsmann ist der Halunke, der in der Falschheit seines Mundes wandelt,
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 der mit dem Auge blinzelt, mit dem Fuße deutet, mit seinen Fingern Zeichen gibt
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 und der Verkehrtes sinnt im Herzen und allzeit Streitereien anfängt.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Das Unheil, das er stiftet, kommt ganz plötzlich; in einem Augenblicke schlägt er unheilbare Wunden.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 Sechs Dinge sind dem Herrn verhaßt; ein Greuel sind ihm sieben:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 hochmütige Augen, falsche Zunge, Hände, die unschuldig Blut vergießen,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 ein Herz, das arge Tücke sinnt, und Füße, die behend zum Schlechten eilen;
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 wer Lügen haucht als falscher Zeuge; wer Händel zwischen Brüdern stiftet.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 Mein Sohn, beachte das Gebot des Vaters! Verwirf nicht deiner Mutter Mahnung
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 und bind sie dir aufs Herz für alle Zeit! Leg sie um deinen Hals als Schmuck!
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 Bei deinem Gehen möge sie dich leiten, bei deinem Niederlegen dich bewachen, und dich ansprechen, wachst du auf.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Denn das Gebot ist eine Leuchte, ein Licht die Weisung; ein Weg zum Leben ist die Mahnung und die Warnung.
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 Denn sie bewahren dich vorm schlimmen Weib und vor der Fremden glatter Zunge.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Nach ihrer Schönheit giere nicht in deinem Herzen! Sie fange nicht mit ihren Blicken dich!
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 Für eine Dirne geht ein Brotlaib drauf; doch eine Ehefrau macht Jagd auf teures Leben.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Kann jemand Feuer in den Schoß einscharren, und seine Kleider würden nicht dabei versengt?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Auf glühende Kohlen sollte jemand treten, und seine Füße würden nicht verbrannt?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 Also ergeht es dem, der zu des Nächsten Weibe geht; wer sie berührt, der bleibt nicht ungestraft.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 Verachtet man nicht einen Dieb, auch wenn er stiehlt, bloß um die Gier zu stillen, dieweil ihn hungert?
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 Wird er ertappt, dann muß er siebenfach ersetzen, muß seines Hauses Hab und Gut hingeben.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 Wer Ehebruch mit einem Weibe treibt, ist unsinnig; nur wer sich selber ins Verderben stürzen will, tut so etwas.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 Nur Schläge, Schande findet er, und seine Schmach ist unauslöschlich.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Des Ehemannes Grimm wird leidenschaftlich aufgeregt; er schont ihn nicht am Tag der Rache.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 Mit irgendeinem Reuegeld beruhigt er sich nicht; er gibt sich nicht zufrieden, auch wenn du noch soviel Geschenke gibst.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Sprueche 6 >