< Sprueche 24 >

1 Verlange nicht nach Boshaften! Trag kein Gelüst, mit ihnen zu verkehren!
Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 Denn nur Gewalttat sinnt ihr Herz, und Unheil reden ihre Lippen.
kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Durch Weisheit wird allein ein Haus erbaut, und durch verständig Wesen wird es fest gegründet.
Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Durch Einsicht füllen sich die Kammern mit seltener und wohlverdienter Habe.
Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 Ein weiser Mann ist mächtig, ein Kluger voller Kraft.
Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 Mit Kunst fuhrst glücklich du den Krieg; der Sieg ist da, wo viele Ratgeber.
maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Dem Toren ist die Weisheit unerreichbar; er fragt nicht auf dem Markt danach.
Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Wer Schlechtigkeit zu tun sich vornimmt, den heißt man einen abgefeimten Schurken.
Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 Das Dichten und das Trachten eines Toren ist das Laster, und das des Spötters sind Abscheulichkeiten.
Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 Wenn du dich schlaff an schlimmen Tagen zeigst, wird deine Kraft sich mindern.
Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 Die man zum Tode führt, die suche zu befreien; verlaß nicht, die man führt zur Hinrichtung hinaus!
Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 Denn, wenn du sagst: "Wir haben's nicht gekonnt", durchschaut's nicht der, der alle Herzen wägt, und wird's nicht inne, der auf deine Seele achtet? Wird nicht dem Mann nach seinem Tun vergolten?
Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13 Mein Sohn iß Honig! Er ist gut. Und Honigseim! Süß ist er deinem Gaumen.
Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 So schätze auch die Weisheit ein für deine Seele! Wenn du sie findest, gibt es eine Zukunft, und deine Hoffnung wird nicht mehr zuschanden.
Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 Belaure, Frevler, nicht des Frommen Ruhestätte! Dir soll es nicht gelingen, seine Lagerstätte zu zerstören.
Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 Denn fällt auch siebenmal der Fromme, steht er doch immer wieder auf; die Frevler aber sinken in das Unglück.
Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Nicht juble über deines Feindes Fall, und über seinen Sturz frohlocke nicht dein Herz!
Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 Sonst sieht mit Mißbehagen es der Herr und wendet seinen Zorn von jenem.
au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 Erhitze dich nicht über Bösewichte! Ereifere dich nicht über Frevler!
Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 Denn keine Zukunft hat der Böse; des Bösewichtes Leuchte wird erlöschen.
maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Mein Sohn! Fürchte den Herrn und fürcht den König! Mit Aufrührern verkehre nicht!
Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 Denn plötzlich kommt ihr Unheil, und dem Mißgeschicke, das von beiden kommt, wer weiß ihm zu begegnen?
maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 Auch das sind Aussprüche von Weisen: Bei Gericht Parteilichkeit: ein übel Ding.
Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 Wer zu dem Schuldigen spricht: "Du bist im Recht", ja, den verwünschen Völker und verfluchen Nationen.
Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 Doch denen, die gebührend strafen, ergeht es wohl, und über sie kommt Glück und Segen.
Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 Die Lippen schließt, wer immer rechte Antwort gibt.
Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27 Besorge draußen dein Geschäft! Bestell den Acker dir! Setz dein Gebäude gut instand!
Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28 Sei gegen deinen Nächsten niemals Zeuge ohne Grund! Täusch mit den Lippen nicht!
Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29 Sprich nicht: "So wie er mir getan, so will auch ich ihm tun; ich will dem Mann nach seinem Tun vergelten!"
Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30 Den Acker eines faulen Mannes habe ich betrachtet, den Weinberg eines unverständigen Menschen.
Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31 Da war er ganz in Wicken aufgegangen; das Unkraut deckte seine Fläche, und seine Steinmauer war eingerissen.
Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Ich habe hingeschaut und es beherzigt; ich habe hingeblickt und eine Warnung mir daraus genommen.
Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33 "Ach noch ein wenig Schlaf, ein wenig Schlummer, ein wenig noch die Hände ineinander legen, um zu ruhen!"
Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
34 Schon kommt die Armut über dich gleich der des Strolches, und Mangel gleich dem eines Bettlers.
na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.

< Sprueche 24 >