< Job 40 >

1 Der Herr erwiderte dem Job und sprach:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 "Ist nun der Streit mit dem Allmächtigen zu Ende? Wer Gott anklagt, antworte drauf!"
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Und Job erwiderte dem Herrn und sprach:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 "Ich bin doch zu gering, daß ich Dir Antwort gebe; ich lege meine Hand auf meinen Mund.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Einmal hab ich geredet; ich widerspreche nimmer. Ein zweitesmal tu ich's nicht wieder."
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Der Herr erwiderte dem Job nach diesem Wettersturm und sprach:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 "Auf, gürte deine Lenden wie ein Mann! Ich will dich fragen; du belehre mich!
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Willst du mein Recht vielleicht zunichte machen und mich verdammen, daß du Recht behältst?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Hast du denn einen Arm wie Gott? Kannst du gleich diesem donnern lassen?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Mit Hoheit schmücke dich und mit Erhabenheit. Umkleide dich mit Glanz und Herrlichkeit!
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Laß deines Zornes Gluten sich ergießen! Und wirf mit deinen Blicken jeden Stolzen nieder!
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Mit einem Blick demütige jeden Stolzen! An ihrem Orte wirf die Frevler nieder!
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Verbirg im Staube sie zumal. Und steck ihr Angesicht an den verborgenen Ort!
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Dann will auch ich dich loben, wenn du dir selber hilfst.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Das Nilpferd sieh dir an, das ich geschaffen, im Vergleich zu dir! Gleich einem Rinde frißt es Gras.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Betrachte aber doch die Kraft in seinen Lenden und seine Stärke in den Muskeln seines Leibes!
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Gleich einer Zeder streckt es seinen Schweif hinaus. Die Sehnen seiner Schenkel, dicht verschlungen,
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 und seine Knochen sind wie eherne Röhren, und seine Beine sind wie Eisenstäbe.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Es ist dies Gottes Meisterwerk; sein Schöpfer gab ihm eine Sichel.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Die Berge liefern ihm das Futter; es spottet aller wilden Tiere.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Und unter Lotosbüschen lagert's dort in dem Versteck von Rohr und Schilf.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Und Lotosbüschel überdachen es als Schattenspender; des Baches Weiden halten es umfangen.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Wenn sich ein Strom ergießt, wird ihm nicht bange. Es bleibt getrost, ergösse sich ein Jordan ihm ins Maul.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Kann man's mit seinen Augen bannen? Will man mit Stricken wohl die Nase ihm durchbohren?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >