< Job 38 >

1 Darauf antwortete der Herr dem Job nach dem Gewitter also:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 "Wer ist denn dieser, der mit einsichtslosen Worten so dunkel findet meine Pläne?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Auf, gürte deine Lenden wie ein Mann! Ich will dich fragen; du belehre mich!
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Wo warst du denn, als ich die Erde gründete? Vermelde es, wenn Einsicht dir bekannt.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Wer nur bestimmte ihre Maße? Du weißt es ja. Wer hat die Meßschnur über sie gespannt?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Worauf sind ihre Pfeiler eingesenkt? Wer hat für sie den Schlußstein eingesetzt?
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Wo warst du, als die Morgensterne jubelten, als alle Gottessöhne jauchzten?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Wer schloß das Meer mit Toren ein, als dies hervorbrach wie aus einem Mutterschoß,
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 als ich Gewölk zu seinem Kleide machte und dichte Finsternis zu seinen Windeln?
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Ich gab ihm mein Gesetz, versah mit Riegeln seine Tore
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 und sprach: 'Bis hierher und nicht weiter! Hier soll sich brechen deiner Wogen Überschwang!'
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Hast du in deinem Leben je dem Morgenrot geboten, dem Frührot seine Stätte angewiesen,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 der Erde Säume zu umfassen, damit die Frevler von ihr schwänden?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Sie wandelt sich gleich Siegelton; sie färbt sich gleichwie ein Gewand.
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Den Frevlern wird ihr Licht entzogen; zerschmettert wird der schon erhobene Arm.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Gelangtest du bis zu des Meeres Strudeln? Bist du gewandelt auf der Tiefe Grund?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Und öffneten sich dir des Todes Tore, und schautest du des tiefen Dunkels Hüter?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Hast du der Erde Breiten überschaut? Vermelde, wenn du dies alles weißt:
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Wo ist der Weg zur Wohnstätte des Lichtes,
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 wo ist der Ort der Finsternis, auf daß du jenes zum Gebiete dieser führen und ihrer Wohnung Wege zeigen kannst?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Du weißt es ja; denn damals wurdest du geboren, und deiner Tage Zahl ist groß.
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Bist du gekommen zu des Schnees Kammern? Hast du erblickt des Hagels Speicher,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 den für die Drangsalzeit ich aufgespart, für Kampf- und Fehdetage?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Wo ist der Weg dahin, wo sich der Sturm zerteilt, von wo der Ostwind auf die Erde sich verbreitet?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Wer hat Kanäle für den Regen hergestellt und einen Weg dem Wetterstrahl,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 um Regen menschenleerem Land zu geben, der Wüste, in der keine Leute wohnen,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 um öde Wildnis zu ersättigen, damit sie Pflanzen sprossen lasse?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Hat denn der Regen einen Vater? Wer hat die Tautropfen erzeugt?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Aus wessen Schoße kommt das Eis? Wer hat des Himmels Reif geboren?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Gleich dem Kristall verdichtet sich das Wasser; der Wasserfluten Fläche hält dann fest zusammen.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Verknüpfest du die Bande der Plejaden, oder lösest du die Fesseln des Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Führst du den Tierkreis aus zu seiner Zeit, und leitest den Bären du samt seinen Jungen?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Erkennst du die Gesetze der Himmelshöhn? Bestimmst du ihre Herrschaft für die Erde?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Erhebst du zu der Wolke deine Stimme? Bedeckt dich dann ein Wasserschwall?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Entsendest du die Blitze, daß sie gehen und zu dir sagen: 'Hier sind wir'?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Wer legte in die Wolken Weisheit? Oder wer verlieh der Wolkenmasse Klugheit?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Wer treibt die Wolken weise fort? Wer legt des Himmels Krüge um,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 auf daß zu Gußwerk fließt der Staub zusammen und fest die Schollen aneinanderkleben?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Erjagst du für die Löwin Beute? Und stillest du die Gier der jungen Leuen,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 wenn in den Lagerstätten sie sich ducken, im Dickicht auf der Lauer liegen?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Wer gibt dem Raben seine Atzung, wenn seine Jungen schrein zu Gott und ohne Nahrung flattern?"
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >