< 1 Mose 10 >

1 Und dies ist die Geschlechterfolge der Söhne Noes: Noes Söhnen Sem, Cham und Japhet wurden nach der Flut Söhne geboren.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Japhets Söhne waren Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Mesek und Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Gomers Söhne waren Askenaz, Riphat und Togarma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Javans Söhne waren Elisa, Tarsis, Kittim und Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Von diesen hatten sich der Heiden Inseln abgezweigt nach ihren Ländern, ihren verschiedenen Sprachen, Stämmen und Völkerschaften.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Chams Söhne waren Kusch, Misraim, Put und Kanaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 Des Kusch Söhne waren Saba, Chavila, Sabta, Regma und Sabteka, und Regmas Söhne waren Scheba und Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Und Kusch hatte Nimrod gezeugt; dieser war zuerst ein Kriegsheld auf Erden gewesen.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 Er war ein gewaltiger Jäger vor dem Herrn; daher pflegt man zu sagen: "Gleich Nimrod ist er ein gewaltiger Jäger vor dem Herrn."
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Seine Herrschaft erstreckte sich anfangs auf Babel, Erech, Akkad und Kalne im Lande Sinear.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Von diesem Lande zog er nach Assur; da baute er Ninive - dazu Rechobot-Ir und Kelach
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 sowie Resen zwischen Ninive und Kelach -, das ist die große Stadt.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Und Misraim zeugte die Luditer, Anamiter, Lehabiter und Naphtuchiter
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 sowie die Patrusiter und Kasluchiter und die, von denen die Philister stammten, die Kaphtoriter.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kanaan zeugte Sidon, seinen Erstgeborenen, und Chet,
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 sowie die Jebusiter, Amoriter und Girgasiter,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Chiviter, Arkiter, Siniter,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Arvaditer, Semariter und Chamatiter; hernach breiteten sich die Kanaaniterstämme aus.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 Das Kanaanitergebiet erstreckte sich von Sidon bis nach Gerar, Gaza, Sodoma, Gomorrha, Adma. Seboim und Lesa.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Dies sind Chams Söhne nach ihren Stämmen, Sprachen, Ländern und Völkerschaften.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Auch Sem, dem Stammvater aller Söhne Ebers und ältesten Bruder Japhets, wurden Kinder geboren.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Sems Söhne waren Elam, Assur, Arpaksad, Lud und Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Arams Söhne waren Uz, Chul, Geter und Masch.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Und Arpaksad zeugte Selach und Selach den Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Dem Eber wurden zwei Söhne geboren; der eine hieß Peleg, weil sich zu seiner Zeit die Erde gespalten hatte; sein Bruder hieß Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Und Joktan zeugte Almodad, Seleph, Chasarmavet, Jerach,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Uzal, Dikla,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Scheba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Chavila und Jobab: dies alles sind Joktans Söhne.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Ihre Wohnsitze reichten von Mesa bis Sephar beim Ostgebirge.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Dies sind die Söhne Sems nach ihren Stämmen, Sprachen, Ländern und Völkerschaften.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Dies sind die Stämme der Noesöhne nach ihren Sippen und Völkerschaften; von ihnen haben sich nach der Flut die Völker auf Erden abgesondert.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< 1 Mose 10 >