< 1 Chronik 8 >

1 Benjamin zeugte als seinen Erstgeborenen Bela, als zweiten Asbel, als dritten Achrach,
Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu,
2 als vierten Nocha und als fünften Rapha.
Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano.
3 Bela hatte zu Söhnen Addar, Gera, Abihud,
Wana wa Bela walikuwa: Adari, Gera, Abihudi,
4 Abisu, Naaman, Achoch,
Abishua, Naamani, Ahoa,
5 Gera, Sephuphan und Churam.
Gera, Shefufani na Huramu.
6 Dies sind Achuds Söhne. Diese sind die Familienhäupter der Einwohner Gebas. Man führte sie gefangen nach Manachat.
Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi:
7 Naaman, Achia und Gera hat er fortgeführt, nachdem jener Uzza und Achichud gezeugt hatte.
Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliwaongoza kwenda uhamishoni.
8 Sacharaim zeugte in Moabs Gefilde, nachdem er seine Weiber Chusim und Baara entlassen hatte.
Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara.
9 Er zeugte mit seinem Weibe Chodes den Jobab, Sibja, Mesa, Malkam,
Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu,
10 Jëus, Sokja und Mirma. Dies sind seine Söhne, Familienhäupter.
Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao.
11 Mit Chusim hatte er Abitub und Elpaal gezeugt.
Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali.
12 Elpaals Söhne sind Eber, Misam und Semer. Dieser baute Ono, ebenso Lod mit seinen Tochterorten.
Wana wa Elpaali walikuwa: Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyeijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka),
13 Beria und Sema sind die Familienhäupter der Einwohner Ajjalons. Sie haben die Bewohner von Gat vertrieben.
na Beria na Shema, waliokuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi.
14 Berias Söhne sind Achjo, Sasak, Jeremot,
Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yeremothi,
15 Zebadja, Arad, Ader,
Zebadia, Aradi, Ederi,
16 Mikael, Ispa und Jocha.
Mikaeli, Ishpa, na Yoha.
17 Elpaals Söhne sind Zebadja, Mesullam, Chizki, Cheber,
Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,
18 Ismere, Izlia und Jobab.
Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Elpaali.
19 Simeis Söhne sind Jakim, Zikri, Zabdi,
Yakimu, Zikri, Zabdi,
20 Elienai, Silletai, Eliel,
Elienai, Silethai, Elieli,
21 Adaja, Beraja und Simrat.
Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wana wa Shimei.
22 Sasaks Söhne sind Ispan, Eber, Eliel,
Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli,
23 Abdon, Zikri, Chanan,
Abdoni, Zikri, Hanani,
24 Chananja, Elam, Antotia,
Hanania, Elamu, Anthothiya,
25 lphdaja und Penuel.
Ifdeya na Penueli.
26 Jerochams Söhne sind Samserai, Secharja, Atalja,
Shamsherai, Sheharia, Athalia,
27 Jaaresja, Elia und Zikri.
Yaareshia, Eliya na Zikri walikuwa wana wa Yerohamu.
28 Dies sind in ihren Sippen die Familienhäupter. Als Häupter haben sie zu Jerusalem gewohnt.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
29 Zu Gibeon wohnten der Vater Gibeons und sein Weib namens Maaka.
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka.
30 Sein erstgeborener Sohn ist Abdon, dann Sur, Kis, Baal, Nadab,
Mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
31 Gedor, Achjo und Zeker.
Gedori, Ahio, Zekeri,
32 Miklot hat Sima gezeugt. Auch sie wohnten in Jerusalem bei ihren Brüdern, diesen gegenüber.
na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
33 Ner zeugte Kis und Kis den Saul und Saul den Jonatan, Malkisua, Abinadab und Esbaal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
34 Jonatans Sohn ist Meribbaal, und Meribbaal zeugte Mika.
Yonathani akamzaa: Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
35 Mikas Söhne sind Piton, Melek, Tare und Achaz.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.
36 Achaz zeugte Joadda und Joadda den Alemet, Azmavet und Zimri und Zimri den Mosa.
Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
37 Mosa zeugte den Bina. Dessen Sohn ist Rapha, dessen Sohn Elasa und dessen Sohn Asel.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
38 Asel hatte sechs Söhne. Dies sind ihre Namen: Azrikam, sein Erstgeborener, Ismael und Searja, Obadja und Chanan. Alle diese waren Söhne Asels.
Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli.
39 Seines Bruders Esek Söhne sind sein Erstgeborener Ulam, der zweite Jëus und der dritte Eliphelet.
Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.
40 Ulams Söhne waren kriegstüchtige Männer, die den Bogen spannen konnten. Sie hatten auch zahlreiche Söhne und Enkel, 150. Alle diese gehören zu den Söhnen Benjamins.
Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150. Hawa wote ndio walikuwa wazao wa Benyamini.

< 1 Chronik 8 >