< Romains 9 >

1 Je dis la vérité en Christ, je ne mens point, et ma conscience m'en rend témoignage par le Saint-Esprit:
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 j'ai une grande tristesse et un continuel tourment dans le coeur.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Car je souhaiterais d'être moi-même anathème, séparé de Christ, pour mes frères, mes parents selon la chair,
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 qui sont Israélites, à qui appartiennent l'adoption, la gloire, les alliances, la loi, le culte, les promesses;
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 qui descendent des patriarches, et desquels est issu selon la chair le Christ, qui est au-dessus de tous. Dieu béni éternellement. Amen! (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Ce n'est pas que la parole de Dieu soit restée sans effet. Car tous ceux qui descendent d'Israël ne sont pas pour cela le vrai Israël.
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 Pour être la postérité d'Abraham, ils ne sont pas tous ses enfants; mais il est dit: «C'est en Isaac que tu auras une postérité appelée de ton nom»,
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 — c'est-à-dire que ce ne sont pas les enfants de la chair qui sont enfants de Dieu, mais ce sont les enfants de la promesse qui sont considérés comme la postérité d'Abraham.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 En effet, c'est une promesse que cette parole: «Je reviendrai en cette même saison, et Sara aura un fils»
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 Et d'autre part il en fut de même pour Rébecca, lorsqu'elle eut conçu deux jumeaux d'Isaac, notre père.
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 En effet, lorsque les enfants n'étaient pas encore nés et qu'il n'avaient fait ni bien, ni mal — afin que fût maintenu le dessein de Dieu, qui procède de son libre choix, et qui dépend non des oeuvres, mais de Celui qui appelle —
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 il fut dit à leur mère: «L'aîné sera assujetti au plus jeune»
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 — conformément à ce qui est écrit: , «J'ai aimé Jacob et j'ai haï Ésaü.»
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Que dirons-nous donc? Y a-t-il en Dieu de l'injustice?
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Non certes! Car il dit à Moïse: «Je ferai miséricorde à qui je ferai miséricorde, et j'aurai pitié de qui j'aurai pitié.»
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 Cela ne vient donc ni de celui qui veut, ni de celui qui court, mais de Dieu qui fait miséricorde.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Aussi l'Écriture dit-elle à Pharaon: «Voici pourquoi je t'ai suscité: c'est pour montrer en toi ma puissance, et afin que mon nom soit annoncé par toute la terre.»
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 Ainsi donc, il fait miséricorde à qui il veut, et il endurcit qui il veut.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Tu me diras: Pourquoi donc Dieu se plaint-il encore? Car qui peut résister à sa volonté?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 Mais plutôt, qui es-tu, toi, homme, pour contester avec Dieu? Le vase d'argile dira-t-il à celui qui l'a formé: Pourquoi m'as-tu fait ainsi?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Le potier n'est-il pas maître de l'argile, pour faire avec la même masse tel vase pour un usage honorable, et tel autre pour un usage vulgaire?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 Et qu'y a-t-il à dire, si Dieu, voulant montrer sa colère et faire connaître sa puissance, a supporté, avec une grande longanimité, des vases de colère destinés à la perdition,
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 afin de faire connaître aussi les richesses de sa gloire par les vases de miséricorde, qu'il a d'avance préparés pour la gloire?
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 Je parle de nous, qu'il a appelés non seulement du milieu des Juifs, mais aussi du milieu des Païens.
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 C'est ainsi qu'il dit dans Osée: «J'appellerai mon peuple celui qui n'était pas mon peuple, et bien-aimée celle qui n'était pas la bien-aimée.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 Et il arrivera que dans le lieu où il leur avait été dit: Vous n'êtes point mon peuple; là même ils seront appelés fils du Dieu vivant.»
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 Ésaïe, de son côté, s'écrie en parlant d'Israël: «Quand le nombre des enfants d'Israël serait comme le sable de la mer, un reste seulement sera sauvé;
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 car le Seigneur accomplira pleinement et promptement sa parole sur la terre.»
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 Et comme Ésaïe l'a prédit: «Si le Seigneur des armées ne nous eût laissé un germe de notre race, nous serions devenus comme Sodome; nous aurions été semblables à Gomorrhe.»
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Que dirons-nous donc? Que les Païens, qui ne cherchaient pas la justice, ont obtenu la justice, mais la justice qui vient de la foi;
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 tandis que les Israélites qui cherchaient la loi de la justice, ne sont point parvenus à cette loi.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Pourquoi? Parce qu'ils l'ont cherchée non par la foi, mais par les oeuvres; ils se sont heurtés contre la pierre d'achoppement,
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 ainsi qu'il est écrit: «Voici que je place en Sion une pierre d'achoppement, un rocher qui fait tomber; et celui qui croit en lui, ne sera pas couvert de confusion.»
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Romains 9 >