< Marc 3 >

1 Une autre fois, Jésus entra dans une synagogue, où se trouvait un homme qui avait la main desséchée.
Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
2 Les pharisiens l'observaient pour voir s'il le guérirait un jour de sabbat, afin de pouvoir l'accuser.
Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
3 Il dit à l'homme qui avait la main desséchée: Lève-toi et tiens-toi au milieu de nous.
Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
4 Puis il leur dit: Est-il permis, le jour du sabbat, de faire du bien ou de faire du mal; de sauver une personne ou de la tuer? Mais ils gardaient le silence.
Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
5 Alors, promenant sur eux ses regards avec indignation, et affligé de l'endurcissement de leur coeur, il dit à l'homme: Étends ta main. Il l'étendit, et sa main redevint saine.
Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
6 Les pharisiens, étant sortis, tinrent aussitôt conseil avec les hérodiens contre lui, pour le faire périr.
Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
7 Jésus se retira avec ses disciples du côté de la mer, et une grande multitude, venue de la Galilée, le suivit. De la Judée aussi,
Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
8 de Jérusalem, de l'Idumée, du pays au-delà du Jourdain, ainsi que des environs de Tyr et de Sidon, une grande multitude, ayant entendu parler de tout ce qu'il faisait, vint vers lui.
na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
9 Alors il dit à ses disciples de lui tenir une petite barque toute prête, à cause de la foule, pour ne pas être trop pressé par elle.
Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
10 Car il avait guéri plusieurs malades, de sorte que tous ceux qui avaient quelque mal se jetaient sur lui pour le toucher.
Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
11 Et quand les esprits impurs le voyaient, ils tombaient à ses pieds et s'écriaient: Tu es le Fils de Dieu!
Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
12 Mais il leur défendait sévèrement de le faire connaître.
Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
13 Il alla ensuite sur la montagne, et il appela ceux qu'il voulut choisir lui-même, et ils vinrent à lui.
Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
14 Il en désigna douze, qu'il nomma apôtres, pour les avoir avec lui et pour les envoyer prêcher,
Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
15 avec le pouvoir de chasser les démons.
na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
16 Voici les douze qu'il désigna: Simon, à qui il donna le nom de Pierre;
Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
17 Jacques, fils de Zébédée, et Jean, frère de Jacques, auxquels il donna le nom de Boanerges, c'est-à-dire fils du tonnerre;
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
18 André, Philippe, Barthélémy, Matthieu, Thomas, Jacques, fils d'Alphée, Thaddée, Simon le Cananéen,
na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 et Judas Iscariote, celui-là même qui le trahit.
na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
20 Jésus entra dans une maison avec ses disciples; et la foule s'y rassembla encore, de sorte qu'ils ne pouvaient pas même prendre leur repas.
Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
21 Quand ses proches l'eurent appris, ils vinrent pour s'emparer de lui; car ils disaient qu'il avait perdu l'esprit.
Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
22 Les scribes, descendus de Jérusalem, disaient: Il est possédé de Béelzébul, et il chasse les démons par le prince des démons!
Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
23 Mais Jésus, les ayant appelés, leur dit en paraboles: Comment Satan pourrait-il chasser Satan?
Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
24 Si un royaume est divisé contre lui-même, ce royaume-là ne peut subsister;
Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 et si une maison est divisée contre elle-même, cette maison-là ne saurait subsister.
Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 Si donc Satan s'élève contre lui-même, il est divisé et il ne peut subsister, mais il est près de sa fin.
Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
27 Nul ne peut entrer dans la maison de l'homme fort et piller son bien, s'il n'a auparavant lié cet homme fort; après cela, il pourra piller sa maison.
Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
28 En vérité, je vous le dis, tous les péchés seront pardonnés aux enfants des hommes, ainsi que tous les blasphèmes qu'ils auront proférés;
Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
29 mais tout homme qui aura blasphémé contre le Saint-Esprit, n'en obtiendra jamais le pardon; il est coupable d'un péché éternel. (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Jésus parla ainsi, parce qu'ils disaient: Il est possédé d'un esprit impur.
Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
31 La mère et les frères de Jésus arrivèrent; et, se tenant dehors, ils l'envoyèrent appeler.
Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
32 La foule était assise autour de lui. Et on lui dit: Voici que ta mère et tes frères sont là dehors, qui te cherchent.
Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
33 Mais il répondit: Qui est ma mère, et qui sont mes frères?
Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
34 Puis, jetant les yeux sur ceux qui étaient assis autour de lui, il dit: Voilà ma mère et mes frères!
Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
35 Quiconque fait la volonté de Dieu, celui-là est mon frère, et ma soeur, et ma mère.
Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.

< Marc 3 >