< Marc 3 >

1 Une autre fois, Jésus entra dans une synagogue, où se trouvait un homme qui avait la main desséchée.
Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
2 Les pharisiens l'observaient pour voir s'il le guérirait un jour de sabbat, afin de pouvoir l'accuser.
Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
3 Il dit à l'homme qui avait la main desséchée: Lève-toi et tiens-toi au milieu de nous.
Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
4 Puis il leur dit: Est-il permis, le jour du sabbat, de faire du bien ou de faire du mal; de sauver une personne ou de la tuer? Mais ils gardaient le silence.
Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
5 Alors, promenant sur eux ses regards avec indignation, et affligé de l'endurcissement de leur coeur, il dit à l'homme: Étends ta main. Il l'étendit, et sa main redevint saine.
Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
6 Les pharisiens, étant sortis, tinrent aussitôt conseil avec les hérodiens contre lui, pour le faire périr.
Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
7 Jésus se retira avec ses disciples du côté de la mer, et une grande multitude, venue de la Galilée, le suivit. De la Judée aussi,
Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
8 de Jérusalem, de l'Idumée, du pays au-delà du Jourdain, ainsi que des environs de Tyr et de Sidon, une grande multitude, ayant entendu parler de tout ce qu'il faisait, vint vers lui.
Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
9 Alors il dit à ses disciples de lui tenir une petite barque toute prête, à cause de la foule, pour ne pas être trop pressé par elle.
Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
10 Car il avait guéri plusieurs malades, de sorte que tous ceux qui avaient quelque mal se jetaient sur lui pour le toucher.
Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
11 Et quand les esprits impurs le voyaient, ils tombaient à ses pieds et s'écriaient: Tu es le Fils de Dieu!
Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
12 Mais il leur défendait sévèrement de le faire connaître.
Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
13 Il alla ensuite sur la montagne, et il appela ceux qu'il voulut choisir lui-même, et ils vinrent à lui.
Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
14 Il en désigna douze, qu'il nomma apôtres, pour les avoir avec lui et pour les envoyer prêcher,
Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
15 avec le pouvoir de chasser les démons.
na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
16 Voici les douze qu'il désigna: Simon, à qui il donna le nom de Pierre;
Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
17 Jacques, fils de Zébédée, et Jean, frère de Jacques, auxquels il donna le nom de Boanerges, c'est-à-dire fils du tonnerre;
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
18 André, Philippe, Barthélémy, Matthieu, Thomas, Jacques, fils d'Alphée, Thaddée, Simon le Cananéen,
Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 et Judas Iscariote, celui-là même qui le trahit.
na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
20 Jésus entra dans une maison avec ses disciples; et la foule s'y rassembla encore, de sorte qu'ils ne pouvaient pas même prendre leur repas.
Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
21 Quand ses proches l'eurent appris, ils vinrent pour s'emparer de lui; car ils disaient qu'il avait perdu l'esprit.
Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
22 Les scribes, descendus de Jérusalem, disaient: Il est possédé de Béelzébul, et il chasse les démons par le prince des démons!
Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
23 Mais Jésus, les ayant appelés, leur dit en paraboles: Comment Satan pourrait-il chasser Satan?
Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
24 Si un royaume est divisé contre lui-même, ce royaume-là ne peut subsister;
Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 et si une maison est divisée contre elle-même, cette maison-là ne saurait subsister.
Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 Si donc Satan s'élève contre lui-même, il est divisé et il ne peut subsister, mais il est près de sa fin.
Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
27 Nul ne peut entrer dans la maison de l'homme fort et piller son bien, s'il n'a auparavant lié cet homme fort; après cela, il pourra piller sa maison.
Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
28 En vérité, je vous le dis, tous les péchés seront pardonnés aux enfants des hommes, ainsi que tous les blasphèmes qu'ils auront proférés;
Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
29 mais tout homme qui aura blasphémé contre le Saint-Esprit, n'en obtiendra jamais le pardon; il est coupable d'un péché éternel. (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Jésus parla ainsi, parce qu'ils disaient: Il est possédé d'un esprit impur.
Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
31 La mère et les frères de Jésus arrivèrent; et, se tenant dehors, ils l'envoyèrent appeler.
Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
32 La foule était assise autour de lui. Et on lui dit: Voici que ta mère et tes frères sont là dehors, qui te cherchent.
Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
33 Mais il répondit: Qui est ma mère, et qui sont mes frères?
Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
34 Puis, jetant les yeux sur ceux qui étaient assis autour de lui, il dit: Voilà ma mère et mes frères!
Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 Quiconque fait la volonté de Dieu, celui-là est mon frère, et ma soeur, et ma mère.
Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

< Marc 3 >