< Luc 5 >

1 Comme Jésus était sur le bord du lac de Génézareth, la foule se pressait autour de lui pour entendre la parole de Dieu.
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 Il vit deux barques arrêtées près du rivage; les pêcheurs en étaient descendus pour laver leurs filets.
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 Il monta dans l'une de ces barques, qui appartenait à Simon, et il le pria de s'éloigner un peu du bord; puis il s'assit, et de là il enseignait la foule.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 Quand il eut cessé de parler, il dit à Simon: Avance en pleine eau, et jetez vos filets pour pêcher.
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 Simon lui répondit: Maître, nous avons travaillé toute la nuit sans rien prendre; mais, sur ta parole, je jetterai le filet.
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 L'ayant jeté, ils prirent une si grande quantité de poissons que leur filet se rompait.
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 Alors ils firent signe à leurs compagnons, qui étaient dans l'autre barque, de venir les aider; ceux-ci vinrent, et ils remplirent les deux barques, tellement qu'elles enfonçaient.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 Simon Pierre, ayant vu cela, se jeta aux genoux de Jésus, et il lui dit: Seigneur, retire-toi de moi; car je suis un homme pécheur.
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 En effet, la frayeur l'avait saisi, ainsi que tous ceux qui étaient avec lui, à cause de la pêche qu'ils avaient faite et des poissons qu'ils avaient pris.
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 Il en était de même de Jacques et de Jean, fils de Zébédée, qui étaient compagnons de Simon. Alors Jésus dit à Simon: Ne crains point; désormais, tu seras pêcheur d'hommes.
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 Puis, après avoir ramené les barques à terre, ils quittèrent tout et le suivirent.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 Comme Jésus était dans une ville, un homme tout couvert de lèpre, l'ayant vu, se jeta le visage contre terre et lui adressa, tout suppliant, ces paroles: Seigneur, si tu le veux, tu peux me rendre net!
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 Jésus étendit la main, le toucha et dit: Je le veux, sois net! Au même instant, la lèpre le quitta.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 Jésus lui défendit de le dire à personne. Mais va, — lui dit-il, — montre-toi au sacrificateur, et offre pour ta purification ce que Moïse a prescrit, afin que cela leur serve de témoignage.
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 Sa renommée se répandait de plus en plus, et une foule de gens se rassemblaient pour l'entendre et pour être guéris de leurs maladies.
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 Mais lui se retirait dans les déserts, et il priait.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 Un jour que Jésus enseignait, des pharisiens et des docteurs de la loi, venus de tous les villages de la Galilée, de la Judée et de Jérusalem, s'étaient assis près de lui; et la puissance du Seigneur lui faisait opérer des guérisons.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 Alors il survint des gens qui portaient sur un lit un paralytique, et ils cherchaient à le faire entrer et à le mettre devant Jésus.
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 Comme ils ne savaient par où le faire passer, à cause de la foule, ils montèrent sur le toit; et, ayant enlevé les tuiles, ils le descendirent avec son petit lit, au milieu de l'assemblée, devant Jésus.
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 Voyant leur foi, Jésus dit: Mon ami, tes péchés te sont pardonnés!
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 Alors les scribes et les pharisiens se mirent à raisonner et à dire: Quel est celui-ci, qui profère des blasphèmes? Qui peut pardonner les péchés, que Dieu seul?
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 Mais Jésus, connaissant leurs pensées, prit la parole et leur dit: Quel raisonnement faites-vous dans vos coeurs?
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 Lequel est le plus aisé, de dire: Tes péchés te sont pardonnés; ou de dire: Lève-toi et marche?
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 Or, afin que vous sachiez que le Fils de l'homme a sur la terre le pouvoir de pardonner les péchés: Je te l'ordonne, — dit-il au paralytique, — lève-toi, emporte ton lit, et va dans ta maison.
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 Et à l'instant, le paralytique se leva en leur présence. Il emporta le lit sur lequel il avait été couché et s'en alla dans sa maison, donnant gloire à Dieu.
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 Tous furent transportés d'enthousiasme; ils glorifiaient Dieu, et, remplis de crainte, ils disaient: Nous avons vu aujourd'hui des choses extraordinaires!
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 Après cela, Jésus sortit; et il vit un péager, nommé Lévi, assis au bureau du péage. Il lui dit: Suis-moi!
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 Et Lévi, quittant tout, se leva et le suivit.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 Lévi lui donna un grand festin dans sa maison, et un grand nombre de péagers et d'autres personnes étaient à table avec eux.
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 Les pharisiens et leurs scribes murmuraient et disaient à ses disciples: Pourquoi mangez-vous et buvez-vous avec des péagers et des pécheurs?
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 Jésus, prenant la parole, leur dit: Ce ne sont pas ceux qui sont en bonne santé qui ont besoin de médecin, mais ceux qui se portent mal.
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 Je ne suis pas venu appeler à la repentance les justes, mais les pécheurs.
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 Ils lui dirent: Les disciples de Jean jeûnent souvent et font des prières, de même que ceux des pharisiens, au lieu que les tiens mangent et boivent.
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 Il leur répondit: Pouvez-vous faire jeûner les amis de l'époux, pendant que l'époux est avec eux?
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 Les jours viendront où l'époux leur sera ôté; alors ils jeûneront dans ces jours-là!
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 Il leur dit encore cette parabole: Personne n'enlève une pièce à un vêtement neuf pour la mettre à un vieux vêtement. Autrement, on déchire le vêtement neuf sans que la pièce neuve s'accorde avec le vêtement vieux.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 De même, personne ne met du vin nouveau dans de vieilles outres; autrement, le vin nouveau rompra les outres; il se répandra, et les outres seront perdues.
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 Mais le vin nouveau doit être mis dans des outres neuves.
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 De même aussi, celui qui boit du vin vieux ne demande pas du vin nouveau; car il dit: C'est le vieux qui est bon.
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luc 5 >