< Luc 4 >

1 Or Jésus rempli de l'Esprit saint revint d'auprès du Jourdain, et il était conduit par l'esprit dans le désert,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 étant pendant quarante jours tenté par le diable. Et il ne mangeait rien durant ces jours-là, et lorsqu'ils furent terminés il eut faim.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Mais le diable lui dit: « Si tu es fils de Dieu, dis à cette pierre-ci qu'elle devienne du pain. »
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Et Jésus lui répliqua: « Il est écrit que ce n'est pas de pain seulement que l'homme vivra. »
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Et l'ayant emmené, il lui montra tous les royaumes de la terre en un seul instant;
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 et le diable lui dit: « Je te donnerai toute cette puissance et leur gloire, car elle m'a été remise, et je la donne à qui je veux;
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 si donc tu te prosternes devant moi, elle sera toute à toi. »
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Et Jésus lui répliqua: « Il est écrit: C'est le Seigneur ton Dieu que tu adoreras, et c'est à Lui seul que tu rendras un culte. »
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 Et il le conduisit à Jérusalem et il le posa sur l'aile du temple, et il lui dit: « Si tu es fils de Dieu, jette-toi d'ici en bas,
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 car il est écrit que Il donnera pour toi des ordres à Ses anges, afin qu'ils te protègent,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 et que ils te porteront sur leurs mains, de peur que tu ne heurtes ton pied contre une pierre. »
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Et Jésus lui répliqua: « Il a été dit: Tu ne tenteras point le Seigneur ton Dieu. »
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Et le diable ayant épuisé toute espèce de tentation s'éloigna de lui jusques à une autre occasion.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Et Jésus, animé de la puissance de l'Esprit, revint en Galilée, et sa renommée se répandit dans toute la contrée voisine.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Et lui-même enseignait dans leurs synagogues, et il était loué de tous.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Et il vint à Nazareth, où il avait été élevé, et il entra selon sa coutume le jour du sabbat dans la synagogue, et il se leva pour faire la lecture.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 Et on lui remit le livre du prophète Ésaïe, et ayant ouvert le livre il trouva le passage où il était écrit:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 « L'esprit du Seigneur est sur moi; c'est pourquoi Il m'a oint afin d'annoncer une bonne nouvelle aux pauvres; Il m'a envoyé pour proclamer aux captifs l'élargissement, et aux aveugles le recouvrement de la vue, pour renvoyer les blessés soulagés,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 pour proclamer une favorable année du Seigneur. »
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Et ayant replié le livre, il le rendit à l'employé, et s'assit; et les regards de tous ceux qui se trouvaient dans la synagogue étaient fixés sur lui.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Et il commença à leur parler en ces termes: « Aujourd'hui ce passage s'est accompli à vos oreilles. »
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Et tous témoignaient en sa faveur, et s'émerveillaient des paroles pleines de grâce qui sortaient de sa bouche, et ils disaient: « Celui-ci n'est-il pas le fils de Joseph? »
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Mais il leur dit: « Sans doute vous m'appliquerez ce proverbe: Médecin, guéris-toi toi-même; fais aussi ici dans ta patrie tout ce que nous avons appris qui s'est fait à Capharnaoum. »
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Mais il ajouta: « En vérité je vous déclare qu'aucun prophète n'est bien reçu dans sa patrie;
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 mais c'est avec vérité que je vous dis que du temps d'Élie il y avait beaucoup de veuves en Israël, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et six mois, en sorte qu'une grande famine eut lieu sur toute la terre,
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 et Élie ne fut envoyé vers aucune d'elles, sauf auprès d'une veuve de Sarepta dans le pays de Sidon.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Et il y avait beaucoup de lépreux en Israël du temps d'Elisée le prophète, et aucun d'eux ne fut nettoyé, sauf Naaman le syrien. »
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Et ils furent tous remplis de courroux dans la synagogue en entendant ces paroles,
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 et s'étant levés, ils l'expulsèrent de la ville, et ils l'emmenèrent jusques au bord de la montagne sur laquelle leur ville était bâtie, de manière à le précipiter.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Mais lui, étant passé au milieu d'eux, poursuivait sa route.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Et il descendit à Capharnaoum, ville de Galilée, et il les enseignait le jour du sabbat;
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 et ils étaient stupéfaits de son enseignement, parce que sa parole était pleine d'autorité.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Et dans la synagogue se trouvait un homme possédé de l'esprit d'un démon impur, et il s'écria à voix haute:
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 « Ah! qu'y a-t-il de commun entre nous et toi, Jésus Nazarénien? Es-tu venu pour nous faire périr? Je sais qui tu es: le saint de Dieu. »
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Et Jésus le réprimanda en disant: « Tais-toi, et sors de lui! » Et le démon l'ayant jeté tout au milieu sortit de lui, sans lui avoir fait aucun mal.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Et tous furent saisis d'épouvante, et ils se disaient les uns aux autres: « Quelle est cette parole? Car il commande avec autorité et puissance aux esprits impurs, et ils sortent? »
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 Et le bruit de sa renommée se répandait dans tous les lieux d'alentour.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Mais ayant quitté la synagogue il entra dans la maison de Simon; or la belle-mère de Simon était prise d'une grosse fièvre, et ils le consultèrent à son sujet.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Et s'étant placé au-dessus d'elle, il réprimanda la fièvre et elle la quitta; or aussitôt s'étant levée, elle les servait.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Or, comme le soleil se couchait, tous ceux qui avaient des malades atteints de diverses maladies les lui amenèrent; et imposant les mains à chacun d'eux, il les guérit.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Mais des démons sortaient aussi de plusieurs d'entre eux, en criant et en disant: « Tu es le fils de Dieu. » Et les réprimandant, il ne leur permettait pas de parler, parce qu'ils savaient qu'il était le Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Mais quand le jour eut paru, il sortit pour se rendre dans un lieu désert, et la foule le cherchait, et elle vint jusques à lui, et elle le retenait pour qu'il ne s'éloignât pas d'eux.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Mais il leur dit: « Il faut que j'annonce aussi à d'autres villes la bonne nouvelle du royaume de Dieu, car c'est pour cela que j'ai été envoyé. »
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Et il prêchait dans les synagogues de la Judée.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luc 4 >