< Proverbes 27 >

1 Ne te vante point du jour du lendemain; car tu ne sais pas ce que ce jour peut enfanter.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
2 Qu'un autre te loue, et non pas ta propre bouche; que ce soit un étranger, et non tes lèvres.
Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
3 La pierre est pesante, et le sable est lourd; mais la colère d'un insensé est plus pesante que l'un et l'autre.
Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
4 La colère est cruelle; et la fureur est comme une inondation; mais qui pourra subsister devant la jalousie?
Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
5 Une réprimande ouverte vaut mieux qu'une amitié cachée.
Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
6 Les blessures faites par celui qui aime, sont fidèles; mais les baisers de celui qui hait sont trompeurs.
Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
7 Celui qui est rassasié, foule aux pieds les rayons de miel; mais celui qui a faim trouve doux même ce qui est amer.
Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
8 Tel qu'est un oiseau qui erre loin de son nid, tel est l'homme qui s'éloigne de sa demeure.
Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
9 L'huile et le parfum réjouissent le cœur; telle est la douceur d'un ami dont le conseil vient du cœur.
Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
10 Ne quitte point ton ami, ni l'ami de ton père, et ne va point dans la maison de ton frère au jour de ta détresse; car un bon voisin qui est près, vaut mieux qu'un frère qui est loin.
Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
11 Mon fils, sois sage, et réjouis mon cœur, et je pourrai répondre à celui qui me fera des reproches.
Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
12 L'homme bien avisé prévoit le mal, et se met à l'abri; mais les simples passent outre et en portent la peine.
Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
13 Quand quelqu'un aura cautionné un étranger, prends son vêtement; exige de lui un gage, à cause des étrangers.
vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14 Celui qui bénit son ami à haute voix, de bon matin, sera considéré comme s'il le maudissait.
Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15 Une gouttière continuelle au temps d'une grosse pluie, et une femme querelleuse, c'est tout un.
Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16 Qui veut la retenir essaie d'arrêter le vent et de saisir de l'huile de sa main.
kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17 Comme le fer aiguise le fer, ainsi un homme en aiguise un autre.
Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18 Celui qui garde le figuier, mangera de son fruit; ainsi celui qui garde son maître sera honoré.
Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19 Comme dans l'eau le visage répond au visage, ainsi le cœur d'un homme répond à celui d'un autre homme.
Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20 Le Sépulcre et le gouffre ne sont jamais rassasiés; de même, les yeux de l'homme sont insatiables. (Sheol h7585)
Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
21 L'argent est éprouvé par le fourneau, l'or par le creuset; et l'homme est jugé d'après sa renommée.
Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22 Quand tu pilerais un insensé dans un mortier, parmi du grain, avec un pilon, sa folie ne se détacherait pas de lui.
Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23 Applique-toi à connaître l'état de tes brebis et donne tes soins à tes troupeaux.
Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24 Car les richesses ne durent pas toujours, et la couronne ne demeure pas d'âge en âge.
maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
25 Le foin se récolte, et la verdure paraît, et les herbes des montagnes sont recueillies.
Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
26 Les agneaux seront pour te vêtir, et les boucs pour payer le champ.
Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
27 Et l'abondance du lait des chèvres sera pour ta nourriture, pour la nourriture de ta maison, et pour la vie de tes servantes.
Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.

< Proverbes 27 >