< Proverbes 27 >

1 Ne te vante point du jour du lendemain; car tu ne sais pas ce que ce jour peut enfanter.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Qu'un autre te loue, et non pas ta propre bouche; que ce soit un étranger, et non tes lèvres.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 La pierre est pesante, et le sable est lourd; mais la colère d'un insensé est plus pesante que l'un et l'autre.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 La colère est cruelle; et la fureur est comme une inondation; mais qui pourra subsister devant la jalousie?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Une réprimande ouverte vaut mieux qu'une amitié cachée.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Les blessures faites par celui qui aime, sont fidèles; mais les baisers de celui qui hait sont trompeurs.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 Celui qui est rassasié, foule aux pieds les rayons de miel; mais celui qui a faim trouve doux même ce qui est amer.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Tel qu'est un oiseau qui erre loin de son nid, tel est l'homme qui s'éloigne de sa demeure.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 L'huile et le parfum réjouissent le cœur; telle est la douceur d'un ami dont le conseil vient du cœur.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Ne quitte point ton ami, ni l'ami de ton père, et ne va point dans la maison de ton frère au jour de ta détresse; car un bon voisin qui est près, vaut mieux qu'un frère qui est loin.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Mon fils, sois sage, et réjouis mon cœur, et je pourrai répondre à celui qui me fera des reproches.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 L'homme bien avisé prévoit le mal, et se met à l'abri; mais les simples passent outre et en portent la peine.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Quand quelqu'un aura cautionné un étranger, prends son vêtement; exige de lui un gage, à cause des étrangers.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 Celui qui bénit son ami à haute voix, de bon matin, sera considéré comme s'il le maudissait.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Une gouttière continuelle au temps d'une grosse pluie, et une femme querelleuse, c'est tout un.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 Qui veut la retenir essaie d'arrêter le vent et de saisir de l'huile de sa main.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Comme le fer aiguise le fer, ainsi un homme en aiguise un autre.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Celui qui garde le figuier, mangera de son fruit; ainsi celui qui garde son maître sera honoré.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Comme dans l'eau le visage répond au visage, ainsi le cœur d'un homme répond à celui d'un autre homme.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Le Sépulcre et le gouffre ne sont jamais rassasiés; de même, les yeux de l'homme sont insatiables. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 L'argent est éprouvé par le fourneau, l'or par le creuset; et l'homme est jugé d'après sa renommée.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Quand tu pilerais un insensé dans un mortier, parmi du grain, avec un pilon, sa folie ne se détacherait pas de lui.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Applique-toi à connaître l'état de tes brebis et donne tes soins à tes troupeaux.
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Car les richesses ne durent pas toujours, et la couronne ne demeure pas d'âge en âge.
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Le foin se récolte, et la verdure paraît, et les herbes des montagnes sont recueillies.
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 Les agneaux seront pour te vêtir, et les boucs pour payer le champ.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 Et l'abondance du lait des chèvres sera pour ta nourriture, pour la nourriture de ta maison, et pour la vie de tes servantes.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Proverbes 27 >