< Luc 21 >

1 Ayant levé les yeux, Jésus vit des riches qui mettaient leurs offrandes dans le trésor du temple.
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 Il vit aussi une pauvre veuve qui y mettait deux pites.
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 Et il dit: Je vous dis en vérité, que cette pauvre veuve a plus mis que personne.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 Car tous ceux-là ont mis, dans les offrandes de Dieu, de leur superflu; mais celle-ci y a mis de son nécessaire tout ce qu'elle avait pour vivre.
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 Et comme quelques-uns disaient que le temple était orné de belles pierres et d'offrandes, il dit:
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 Vous contemplez ces choses! Des jours viendront où il n'y sera laissé pierre sur pierre, qui ne soit renversée.
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 Et ils lui demandèrent: Maître, quand donc ces choses arriveront-elles, et par quel signe connaîtra-t-on qu'elles sont sur le point d'arriver?
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 Et il dit: Prenez garde de ne pas être séduits; car plusieurs viendront en mon nom, disant: C'est moi qui suis le Christ, et le temps approche. Ne les suivez donc pas.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 Or quand vous entendrez parler de guerres et de séditions, ne vous épouvantez pas; car il faut que ces choses arrivent auparavant; mais ce ne sera pas si tôt la fin.
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Il leur dit aussi: Une nation s'élèvera contre une autre nation, et un royaume contre un autre royaume;
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 Et il y aura de grands tremblements de terre en divers lieux, et des famines et des pestes; et il paraîtra des choses épouvantables, et de grands signes dans le ciel.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 Mais, avant tout cela, ils mettront les mains sur vous, et vous persécuteront, vous livrant aux synagogues, et vous mettant en prison, et vous menant devant les rois et devant les gouverneurs, à cause de mon nom.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 Et cela sera pour vous une occasion de témoignage.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 Mettez-vous donc dans l'esprit de ne point préméditer votre défense.
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 Car je vous donnerai une bouche et une sagesse à laquelle tous vos adversaires ne pourront contredire, ni résister.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 Vous serez même livrés par vos parents, par vos frères, par vos proches et par vos amis; et ils feront mourir plusieurs d'entre vous.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 Et vous serez haïs de tout le monde, à cause de mon nom.
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 Mais il ne se perdra pas un cheveu de votre tête.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 Possédez vos âmes par votre patience.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 Et quand vous verrez Jérusalem environnée par les armées, sachez que sa désolation approche.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Alors, que ceux qui seront dans la Judée s'enfuient aux montagnes; que ceux qui seront au milieu de Jérusalem se retirent; et que ceux qui seront à la campagne ne rentrent point.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 Car ce seront des jours de châtiment, afin que toutes les choses qui sont écrites s'accomplissent.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 Malheur aux femmes enceintes, et à celles qui allaiteront en ces jours-là; car il y aura une grande calamité sur ce pays, et de la colère contre ce peuple.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 Ils tomberont sous le tranchant de l'épée, et ils seront menés captifs parmi toutes les nations, et Jérusalem sera foulée par les nations, jusqu'à ce que les temps des nations soient accomplis.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 Et il y aura des signes dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; et sur la terre, les peuples seront dans la consternation et ne sachant que devenir, la mer et les flots faisant un grand bruit.
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 Les hommes seront comme rendant l'âme de frayeur, dans l'attente des choses qui surviendront dans le monde; car les puissances des cieux seront ébranlées.
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 Et alors ils verront venir le Fils de l'homme sur une nuée, avec une grande puissance et une grande gloire.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 Or quand ces choses commenceront d'arriver, regardez en haut, et levez la tête, parce que votre délivrance approche.
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 Et il leur dit une similitude: Voyez le figuier et tous les arbres;
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 Quand ils poussent, vous jugez de vous-mêmes, en les voyant, que l'été est proche.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 De même, lorsque vous verrez arriver ces choses, sachez que le royaume de Dieu est proche.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Je vous dis en vérité, que cette génération ne passera point, que toutes ces choses n'arrivent.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront point.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 Prenez donc garde à vous-mêmes, de peur que vos cœurs ne soient appesantis par la débauche, par l'ivrognerie et par les inquiétudes de cette vie; et que ce jour-là ne vous surprenne subitement.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 Car il surprendra comme un filet tous ceux qui habitent sur la face de la terre.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 Veillez donc, et priez en tout temps, afin que vous soyez trouvés dignes d'éviter toutes ces choses qui doivent arriver, et de subsister devant le Fils de l'homme.
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 Or, Jésus enseignait dans le temple pendant le jour, et, la nuit, il sortait et se tenait sur la montagne appelée des Oliviers.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 Et, dès le point du jour, tout le peuple venait à lui dans le temple pour l'écouter.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< Luc 21 >