< Lévitique 9 >

1 Le huitième jour, Moïse appela Aaron et ses fils, et les anciens d'Israël;
Katika siku ya nane, Musa akawaita Aroni na wanawe pamoja na wazee wa Israeli.
2 Et il dit à Aaron: Prends un jeune veau pour le sacrifice pour le péché, et un bélier pour l'holocauste, l'un et l'autre sans défaut, et offre-les devant l'Éternel.
Akamwambia Aroni, “Twaa ndama dume kutoka kundini kwa ajili ya sadaka ya dhambi zako, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, na uwatoe mbele za Yahweh.
3 Et tu parleras aux enfants d'Israël, en disant: Prenez un bouc pour le sacrifice pour le péché; un veau et un agneau sans défaut, âgés d'un an, pour l'holocauste;
Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Twaeni beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi na ndama na mwana-kondoo, hawa wawili wawe na umri wa mwaka mmoja na bila dosari, ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
4 Un taureau et un bélier pour le sacrifice de prospérités, pour sacrifier devant l'Éternel, et une offrande arrosée d'huile; car aujourd'hui l'Éternel vous apparaîtra.
pia twaeni fahali na kondoo dume kwa sadaka za amani ili kuwatoa mbele za Yahweh, na sadaka za nafaka iliyochanganywa na mafuta, kwa sababu leo Yahweh atajidhihirisha kwenu.
5 Ils amenèrent donc devant le tabernacle d'assignation ce que Moïse avait commandé; et toute l'assemblée s'approcha, et se tint devant l'Éternel.
Kwa hiyo wakaleta kwenye hema la kukutania vyote ambavyo Musa aliagiza, nalo kusanyiko lote la Israeli likakaribia na kusimama mbele za Yahweh.
6 Et Moïse dit: Voici ce que l'Éternel a commandé, faites-le, et la gloire de l'Éternel vous apparaîtra.
Kisha Musa akasema, “Hivi ndivyo Yahweh amewaamru nyinyi mfanye, ili kwamba utukufu wake uweze kuonekana kwenu.
7 Puis Moïse dit à Aaron: Approche-toi de l'autel; fais ton sacrifice pour le péché et ton holocauste, et fais l'expiation pour toi et pour le peuple; présente aussi l'offrande du peuple, et fais l'expiation pour lui, comme l'Éternel l'a commandé.
“Musa akamwambia Aroni, “Njoo karibu na Madhabahu na uteo sadaka yako ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, na kufanya upatanisho kwa ajili ya watu ili kufanya upatanisho kwa ajili yao kama vile ambavyo Yahweh amekwishaamru.”
8 Alors Aaron s'approcha de l'autel, et égorgea le veau de son sacrifice pour le péché.
Kwa hiyo Aroni akaikaribia madhabahu na akamchinja yule ndama kwa ajili ya sadaka ya dhambi, ambayo ilikuwa kwa ajili yake mwenyewe.
9 Et les fils d'Aaron lui présentèrent le sang; il trempa son doigt dans le sang, en mit sur les cornes de l'autel, et répandit le sang au pied de l'autel.
Nao wana wa Aroni wakamletea hiyo damu, naye akakichofya kidole chake kwenye damu na kuiweka kwenye pembe za madhabahu, kisha akaimwaga damu chini ya kitako cha madhabahu.
10 Et il fit fumer sur l'autel la graisse, les rognons, et la membrane qui recouvre le foie de la victime pour le péché, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
Hata hivyo, aliyateketeza hayo mafuta, figo, na mafuta yanafunika ini juu ya madhabahu kuwa sadaka ya dhambi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
11 Mais il brûla au feu, hors du camp, la chair et la peau.
Na akaiteketeza hiyo nyama pamoja na ngozi nje ya kambi
12 Ensuite il égorgea l'holocauste. Les fils d'Aaron lui présentèrent le sang, et il le répandit sur l'autel tout autour.
Aroni akaichinja sadaka ya kuteketezwa, nao wanawe wakampa hiyo damu, ambayo aliinyunza pande zote za madhabahu.
13 Ils lui présentèrent aussi l'holocauste, coupé par morceaux, et la tête, et il les fit fumer sur l'autel.
Kisha wakampa ile sadaka ya kuteketezwa, kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
14 Puis il lava les entrailles et les jambes, et il les fit fumer sur l'holocauste à l'autel.
Akaziosha sehemu za ndani pamoja na miguu na kuziteketeza juu ya dhabihu ya kuteketezwa juu ya Madhabahu.
15 Il offrit aussi l'offrande du peuple. Il prit le bouc du sacrifice pour le péché qui était pour le peuple; il l'égorgea, et l'offrit pour le péché, comme le premier sacrifice;
Aroni akaleta dhabihu ya watu— mbuzi, kisha akamtoa kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi yao naye akamchinja, akaitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi, kama alivyofanya kwa yule mbuzi wa kwanza.
16 Et il offrit l'holocauste, et le fit selon l'ordonnance.
Akaileta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama Yahweh alivyokuwa ameamru.
17 Ensuite il présenta l'offrande; il en remplit la paume de sa main, et la fit fumer sur l'autel, outre l'holocauste du matin.
Akaileta sadaka ya nafaka; akakijaza kiganja chake nafaka na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa.
18 Il égorgea aussi le taureau et le bélier en sacrifice de prospérités pour le peuple. Les fils d'Aaron lui présentèrent le sang, et il le répandit sur l'autel tout autour.
Pia akamchinja fahali na yule kondoo dume, dhabihu kwa ajili ya sadaka ya amani, ambayo ilikuwa kwa ajili ya watu. Nao wana wa Aronni wakampa damu, ambayo aliinyunyiza kila upande wa mdhabahu.
19 Ils lui présentèrent aussi la graisse du taureau et du bélier, la queue, ce qui couvre les entrailles, les rognons, et la membrane qui recouvre le foie;
Hata hivyo, waliyakata mafuta ya fahali na ya yule kondoo dume, mafuta ya kwenye mkia, mafuta yafunikayo sehemu za ndani, figo, na yale mafuta yaliyofunika mapafu.
20 Et ils mirent les graisses sur les poitrines, et il fit fumer les graisses sur l'autel;
Wakazichukua hizi sehemu zilizokatwa wakaziweka juu ya vidari, na kisha Aroni akateketeza mafuta juu ya madhabahu.
21 Puis Aaron agita devant l'Éternel, en offrande, les poitrines et la jambe droite, comme Moïse l'avait commandé.
Naye Aroni akavitikisa vidari na paja la kulia kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh, kama vile Musa alivyokuwa ameamru,
22 Et Aaron éleva ses mains vers le peuple, et le bénit; et il descendit, après avoir offert le sacrifice pour le péché, l'holocauste et le sacrifice de prospérités.
Kisha Aroni akainua juu mikono yake mbele ya watu na kuwabariki, kisha akashuka chini kutoka mahali alipokuwa akitoa hiyo sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani.
23 Alors Moïse et Aaron entrèrent dans le tabernacle d'assignation, puis ils sortirent et bénirent le peuple; et la gloire de l'Éternel apparut à tout le peuple:
Musa na Aroni wakaingia ndani ya hema la kukutania, kisha wakatoka nje tena na kuwabariki watu, na utukufu wa Yahweh ukaonekana kwa watu wote.
24 Un feu sortit de devant l'Éternel, et consuma sur l'autel l'holocauste et les graisses; et tout le peuple le vit, et ils poussèrent des cris de joie, et se jetèrent sur leurs faces.
Moto ukashuka kutoka kwa Yahweh na ukairamba sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wlipoona jambo hili, wakapiga kelele na kulala chini.

< Lévitique 9 >