< Genèse 46 >

1 Et Israël partit, avec tout ce qui lui appartenait, et vint à Béer-Shéba, et offrit des sacrifices au Dieu de son père Isaac.
Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
2 Et Dieu parla à Israël dans les visions de la nuit, et il dit: Jacob, Jacob! Et il répondit: Me voici.
Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
3 Puis il dit: Je suis Dieu, le Dieu de ton père. Ne crains point de descendre en Égypte; car je t'y ferai devenir une grande nation.
Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
4 Je descendrai avec toi en Égypte, et je t'en ferai aussi infailliblement remonter; et Joseph mettra sa main sur tes yeux.
Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
5 Alors Jacob partit de Béer-Shéba, et les fils d'Israël mirent Jacob leur père, et leurs petits enfants, et leurs femmes, sur les chariots que Pharaon avait envoyés pour le porter.
Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
6 Ils emmenèrent aussi leur bétail et le bien qu'ils avaient acquis au pays de Canaan. Et Jacob et toute sa famille avec lui vinrent en Égypte.
Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
7 Il amena avec lui en Égypte ses fils et les fils de ses fils, ses filles et les filles de ses fils, et toute sa famille.
Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
8 Et voici les noms des fils d'Israël qui vinrent en Égypte: Jacob et ses fils. Le premier-né de Jacob, Ruben.
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
9 Les fils de Ruben: Hénoc, Pallu, Hetsron et Carmi.
Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
10 Les fils de Siméon: Jémuël, Jamin, Ohad, Jakin, Tsohar, et Saül, fils de la Cananéenne.
Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
11 Les fils de Lévi: Guershon, Kéhath et Mérari.
Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
12 Les fils de Juda: Er, Onan, Shéla, Pharets et Zarach. Mais Er et Onan moururent au pays de Canaan. Et les fils de Pharets furent Hetsron et Hamul.
Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
13 Les fils d'Issacar: Thola, Puva, Job et Shimron.
Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
14 Les fils de Zabulon: Séred, Élon et Jahléel.
Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
15 Voilà les fils de Léa, qu'elle enfanta à Jacob, à Paddan-Aram, avec Dina sa fille; ses fils et ses filles étaient en tout trente-trois personnes.
Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
16 Les fils de Gad: Tsiphjon et Haggi, Shuni et Etsbon, Eri, Arodi et Aréli.
Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
17 Les fils d'Asser: Jimna, Jishva, Jishvi, Béria, et Sérach leur sœur. Et les enfants de Béria: Héber et Malkiel.
Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
18 Voilà les fils de Zilpa, que Laban avait donnée à Léa, sa fille; et elle les enfanta à Jacob: seize personnes.
Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
19 Les fils de Rachel, femme de Jacob: Joseph et Benjamin.
Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
20 Et Joseph eut des fils au pays d'Égypte: Manassé et Éphraïm qu'Asnath, fille de Potiphéra, prêtre d'On, lui enfanta.
Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
21 Les fils de Benjamin: Béla, Béker et Ashbel, Guéra et Naaman, Ehi et Rosh, Muppim et Huppim, et Ard.
Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
22 Voilà les fils de Rachel, qui naquirent à Jacob; en tout quatorze personnes.
Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
23 Les fils de Dan: Hushim.
Mwana wa Dani ni: Hushimu.
24 Les fils de Nephthali: Jahtséel, Guni, Jetser et Shillem.
Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
25 Voilà les fils de Bilha, que Laban avait donnée à Rachel, sa fille, et elle les enfanta à Jacob; en tout sept personnes.
Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
26 Toutes les personnes appartenant à Jacob et nées de lui, qui vinrent en Égypte (sans les femmes des fils de Jacob), étaient en tout soixante-six.
Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
27 Et les fils de Joseph, qui lui étaient nés en Égypte, étaient deux personnes. Toutes les personnes de la maison de Jacob, qui vinrent en Égypte, étaient soixante et dix.
Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
28 Or, Jacob envoya Juda devant lui vers Joseph, pour qu'il lui montrât la route de Gossen. Ils vinrent donc au pays de Gossen.
Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
29 Et Joseph attela son chariot, et monta à la rencontre d'Israël son père vers Gossen; et il se fit voir à lui, et se jeta à son cou, et pleura longtemps sur son cou.
gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
30 Et Israël dit à Joseph: Que je meure à présent, puisque j'ai vu ton visage, et que tu vis encore.
Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
31 Puis Joseph dit à ses frères et à la famille de son père: Je monterai, pour informer Pharaon, et je lui dirai: Mes frères et la famille de mon père, qui étaient au pays du Canaan, sont venus vers moi;
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
32 Et ces hommes sont bergers, car ils se sont toujours occupés de bétail; et ils ont amené leurs brebis et leurs bœufs, et tout ce qui est à eux.
Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
33 Et quand Pharaon vous fera appeler, et dira: Quel est votre métier?
Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
34 Vous direz: Tes serviteurs se sont toujours occupés de bétail, depuis notre jeunesse et jusqu'à maintenant, et nous et nos pères; afin que vous demeuriez dans le pays de Gossen; car les Égyptiens ont en abomination tous les bergers.
Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”

< Genèse 46 >