< Luc 4 >

1 Jésus, rempli du Saint-Esprit, revint du Jourdain, et fut poussé par un mouvement de l'Esprit au désert:
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 il y fut tenté par le diable pendant quarante jours. Il ne mangea rien dans ces jours-là, et, quand ils furent passés, il eut faim.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Le diable lui dit: «Si tu es Fils de Dieu, commande à cette pierre de se changer en pain.»
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Jésus lui répondit: «Il est écrit que l'homme ne vivra pas de pain seulement.»
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Le diable l'ayant emmené, lui fit voir en un instant tous les royaumes de la terre,
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 et lui dit: «Je te donnerai toute cette puissance et la gloire de ces royaumes; car elles m'ont été données, et je les donne à qui je veux.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Si donc tu te prosternes devant moi, elles t'appartiendront tout entières.»
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Jésus lui répondit: «Il est écrit: «Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu le serviras lui seul.»
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 Le diable le mena à Jérusalem, le posa à l'extrémité de l'aile du temple, et lui dit: «Si tu es Fils de Dieu, jette toi d'ici en bas;
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 car il est écrit qu'il ordonnera à ses anges de te garder,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 et qu'ils te porteront sur leurs bras, de peur que ton pied ne heurte contre une pierre.»
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Jésus lui répliqua qu'il est dit: «Tu ne tenteras point le Seigneur ton Dieu.»
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Et le diable ayant épuisé toute espèce de tentation, s'éloigna de lui jusqu’à nouvelle occasion.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Jésus, animé de la puissance de l'Esprit, s'en retourna en Galilée, et sa renommée se répandit dans tout le pays d'alentour.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Il enseignait dans les synagogues, et tout le monde le glorifiait.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Il vint à Nazareth, où il avait été élevé, et, suivant sa coutume, il entra le jour du sabbat dans la synagogue, et se leva pour faire la lecture.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 On lui remit le livre du prophète Ésaïe; et, l'ayant ouvert, il trouva l'endroit où il est écrit:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 L'Esprit du Seigneur est sur moi, parce qu'il m'a oint pour annoncer l'évangile aux pauvres:
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 il m'a envoyé pour annoncer la délivrance aux captifs, et aux aveugles le recouvrement de la vue; pour renvoyer en liberté les opprimés, et pour publier une année favorable du Seigneur.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Puis, il ferma le livre, le rendit au desservant, et s'assit; et tout le monde dans la synagogue avait les yeux fixés sur lui.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Il se mit à leur dire: Aujourd'hui est accomplie la parole de l'Écriture, comme vous venez de l'entendre de vos oreilles.»
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Et tous témoignaient en sa faveur; ils étaient étonnés des paroles pleines de grâce qui sortaient de sa bouche, et ils disaient: «N'est-ce pas là le fils de Joseph?»
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Alors il leur dit: «Sans doute, vous m'alléguerez le proverbe: «Médecin, guéris-toi toi-même, » et vous me direz, fais également ici, dans ta patrie, tout ce que nous avons appris que tu as fait pour Capernaoum.»
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Mais il ajouta: «En vérité, je vous dis qu'aucun prophète n'est bien venu dans son pays.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 Vraiment, je vous le dis, il y avait beaucoup de veuves en Israël au temps d'Élie, quand le ciel fut fermé durant trois ans et demi, et qu'il y eut une grande famine sur toute la terre,
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 et pourtant Élie ne fut envoyé à aucune d'elles, mais à une veuve de Sarepta, dans le pays de Sidon.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Il y avait de même beaucoup de lépreux en Israël au temps du prophète Élysée, et pourtant aucun d'eux ne fut guéri, mais Naaman le Syrien fut seul guéri.»
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Ces paroles remplirent de colère tous ceux qui étaient dans la synagogue;
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 ils se levèrent, entraînèrent Jésus hors de la ville, et l'emmenèrent jusqu'à un escarpement de la montagne sur laquelle leur ville était bâtie, pour le précipiter en bas;
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 mais il passa au milieu d'eux, et s'en alla.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Il descendit à Capernaoum, ville de Galilée, et là il enseignait les habitants les jours de sabbat;
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 et ils étaient frappés de son enseignement, parce que sa parole était pleine d'autorité.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Il y avait dans la synagogue un homme possédé d'un esprit, d'un démon impur; il poussa un grand cri, et dit
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 «Ah! Qu'y a-t-il entre nous et toi, Jésus de Nazareth? Tu es venu nous faire périr; je te connais, tu es le Saint de Dieu.»
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Jésus le tança: «Tais-toi, lui dit-il, et sors de cet homme.» Et le démon, ayant jeté cet homme par terre, au milieu de la synagogue, sortit de lui, sans lui avoir fait aucun mal.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Tous les assistants étaient dans la stupéfaction, et ils se disaient les uns aux autres: «Quelle parole est la sienne? Il commande avec autorité et puissance aux esprits impurs, et ils sortent!»
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 Et il n'était bruit que de Jésus dans tous les lieux d'alentour.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Étant sorti de la synagogue, il entra dans la maison de Simon. Or la belle-mère de Simon avait une grosse fièvre, et l'on pria Jésus de la guérir.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Il se pencha sur elle, tança la fièvre, et la fièvre la quitta. A l'instant cette femme se leva et se mit à les servir.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Quand le soleil fut couché, tous ceux qui avaient des malades atteints de divers maux, les lui amenèrent; et il les guérit en imposant les mains à chacun d'eux.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Des démons aussi sortaient de plusieurs malades, en criant: «Tu es le Fils de Dieu, » et Jésus les tançait pour leur imposer silence, parce qu'ils savaient qu'il était le Messie.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Quand le jour parut, il sortit et s'en alla dans un lieu désert. Une foule de gens vinrent le chercher jusqu'au lieu où il était, et ils le retenaient pour qu'il ne s'éloignât pas d'eux.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Mais il leur dit: «Il faut que je porte aussi à d'autres villes la bonne nouvelle du royaume de Dieu; car c'est dans ce but que j'ai été envoyé.»
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Et il prêchait dans les synagogues de la Galilée.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luc 4 >