< Luc 3 >

1 La quinzième année du règne de Tibère César, lorsque Ponce Pilate était gouverneur de Judée, qu'Hérode était tétrarque de la Galilée, et Philippe, son frère, tétrarque de l'Iturie et delà Trachonite, et que Lysanias était tétrarque de l'Abilène,
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 du temps du souverain sacrificateur Anne, et de Caïphe, la parole de Dieu fut adressée dans le désert à Jean, fils de Zacharie.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 Il vint dans toute la contrée qui avoisine le Jourdain, prêchant le baptême de la repentance pour le pardon des péchés,
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 ainsi qu'il est écrit dans le livre des discours d'Esaïe, le prophète: «C'est une voix qui crie au désert: «Préparez le chemin du Seigneur, faites-lui des sentiers droits:
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 toute vallée, sera comblée, toute montagne et toute colline seront abaissées; ce qui est tortu sera redressé, et les chemins raboteux seront aplanis:
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 et toute chair verra le salut de Dieu.»
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Jean disait donc aux foules qui venaient se faire baptiser par lui: «Race de vipères, qui vous a appris à fuir la colère à venir?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Produisez donc des fruits dignes de la repentance, et ne vous mettez pas à dire en vous-mêmes: «Nous avons pour père Abraham; » car je vous dis que de ces pierres, Dieu peut susciter des enfants à Abraham.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 Déjà même la cognée est mise à la racine des arbres; tout arbre donc qui ne produit pas de bon fruit, va être coupé et jeté au feu.»
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 Et le peuple lui demanda: «Que faut-il donc faire?»
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 Il leur répondit: «Que celui qui a deux tuniques partage avec celui qui n'en a point; et que celui qui a de quoi manger fasse de même.»
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Des publicains vinrent aussi se faire baptiser, et lui dirent: «Maître, que devons-nous faire?»
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 Il leur dit: «N'exigez rien au delà de ce qui vous est commandé.»
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 Des militaires l'interrogèrent aussi: «Et nous, que devons-nous faire?» Il leur dit: «Ne commettez point d'extorsions, et ne faites de chicanes à personne; contentez- vous de votre paie.»
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 Comme le peuple était dans l'attente, et que chacun se demandait au dedans de soi, si Jean ne serait point le Messie,
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 Jean, s'adressant à tous, leur dit: «Pour moi, je vous baptise d'eau; mais il vient, celui qui est plus puissant que moi, et je ne suis pas digne de délier la courroie de ses sandales: c'est lui qui vous baptisera d'esprit saint et de feu.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Il a son van à la main, et il nettoiera son aire; il amassera le blé dans son grenier, mais il brûlera la paille dans un feu qui ne s'éteint point.»
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 Il annonçait donc la bonne nouvelle au peuple, tout en lui adressant beaucoup d'autres exhortations.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 Mais Hérode, le tétrarque, qu'il reprit au sujet d'Hérodiade, femme de son frère, et de toutes les mauvaises actions que lui, Hérode, avait commises,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 ajouta à tous ses crimes celui de faire jeter Jean en prison.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 Comme tout le peuple se faisait baptiser, Jésus se fit aussi baptiser; et au moment où il priait, le ciel s'ouvrit;
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 le Saint-Esprit descendit sur lui sous une forme corporelle, comme une colombe; et une voix sortit du ciel, disant: «Tu es mon Fils bien-aimé; c'est en toi que j'ai mis toute mon affection.»
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 Jésus avait environ trente ans, quand il commença son ministère. Il était, à ce que l'on croyait, fils de Joseph, fils d'Héli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 fils de Matthat, fils de Lévi, fils de Melchi, fils de Janné, fils de Joseph,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 fils de Mattathias, fils d'Anios, fils de Nahum, fils d'Hesli, fils de Naggé,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 fils de Maath, fils de Mattathias, fils de Semeï, fils de Joseph, fils de Juda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 fils de Johanna, fils de Rhésa, fils de Zorobabel, fils de Salathiel, fils de Néri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 fils de Melchi, fils d'Addi, fils de Cosam, fils d'Elmodain, fils de Her,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 fils de José; fils d'Eliézer, fils de Jorim, fils de Matthat, fils de Lévi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 fils de Syméon, fils de Juda, fils de Joseph, fils de Jônan, fils d'Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 fils de Méléa, fils de Maman, fils de Mattatha, fils de Nathan, fils de David,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 fils d'Issaï, fils de Jobed, fils de Booz, fils de Salmon, fils de Naasson,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 fils d'Aminadab, fils d'Admin, fils d'Ami, fils d'Esron, fils de Phares, fils de Juda,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 fils de Jacob, fils d'Isaac, fils d'Abraham, fils de Tharé, fils de Nachor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 fils de Seruch, fils de Ragan, fils de Phalez, fils d'Héber, fils de Sala,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 fils de Caïnan, fils d'Arpaxad, fils de Sem, fils de Noé, fils de Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 fils de Mathusalem, fils d'Hénoch, fils de Jared, fils de Maleèl, fils de Caïnan,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 fils d'Enos, fils de Seth, fils d'Adam, fils de Dieu.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luc 3 >