< Luc 18 >

1 Il leur montra encore par une parabole, qu'il faut toujours prier, sans se lasser jamais.
Kisha akawaambia mfano wa namna wanavyopaswa kuomba daima, na wasikate tamaa.
2 Il leur dit: «Il y avait dans une ville un juge qui ne craignait point Dieu et qui ne respectait personne.
akaisema, 'Kulikuwa na hakimu katika mji fulani, ambaye hakuwa anamwogopa Mungu na hakuwaheshimu watu.
3 Il y avait aussi dans cette ville une veuve qui venait lui dire: «Fais-moi justice de ma partie adverse.»
Kulikuwa na mjane katika jiji hilo, naye alimwendea mara nyingi, akisema, 'Nisaidie kupata haki dhidi ya mpinzani wangu.'
4 Pendant longtemps il s'y refusa; mais ensuite il dit en lui-même: «Encore que je ne craigne point Dieu et que je ne respecte personne,
Kwa muda mrefu hakuwa tayari kumsaidia, lakini baada ya muda akasema moyoni mwake, `Ingawa mimi simwogopi Mungu au kuheshimu mtu,
5 toutefois, parce que cette veuve m'importune, je lui rendrai justice, afin qu'elle ne vienne pas éternellement me rompre la tête.»
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua nitamsaidia kupata haki yake, ili asije akanichosha kwa kunijia mara kwa mara. ''
6 Le Seigneur dit: «Entendez-vous ce que dit ce juge inique?...
Kisha Bwana akasema, 'Sikiliza alivyosema huyo hakimu dhalimu.
7 Et Dieu ne rendrait pas justice à ses élus, qui crient à lui jour et nuit!... et il tarde à le faire!
Je Mungu pia hataleta haki kwa wateule wake ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, yeye hatakuwa mvumilivu kwao?
8 Je vous dis qu'il leur rendra prompte justice; seulement, quand le Fils de l'homme viendra trouvera-t-il la foi sur la terre?»
Nawaambia kwamba ataleta haki kwao upesi. Lakini wakati Mwana wa Adamu atakapokuja, je, atakuta imani duniani? '
9 Il ajouta cette parabole, en vue de certaines personnes qui se flattent d'être justes, et qui méprisent les autres:
Ndipo akawaambia mfano huu kwa baadhi ya watu ambao wanajiona wenyewe kuwa wenye haki na kuwadharau watu wengine,
10 «Deux hommes montèrent au temple pour prier; l'un était pharisien, l'autre publicain.
'Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo mwingine mtoza ushuru.
11 Le pharisien, la tête haute, priait ainsi en lui-même: «Dieu, je te rends grâce de ce que je ne suis pas comme le reste des hommes, qui sont ravisseurs, injustes, adultères, ni même comme ce publicain:
Farisayo akasimama akaomba mambo haya juu yake mwenyewe, 'Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine ambao ni wanyang'anyi, watu wasio waadilifu, wazinzi, au kama huyu mtoza ushuru.
12 je jeûne deux fois la semaine; je donne la dîme de tous mes revenus.»
Nafunga mara mbili kila wiki. Natoa zaka katika mapato yote ninayopata. '
13 Et le publicain, se tenant à distance, ne se permettait pas même de lever les yeux au ciel; mais il se frappait la poitrine, en disant: «Dieu, sois apaisé envers moi, qui suis un pécheur.»
Lakini yule mtoza ushuru, alisimama mbali, bila hakuweza hata kuinua macho yake mbinguni, akagonga kifua chake akisema, 'Mungu, nirehemu mimi mwenye dhambi.'
14 Je vous déclare que celui-ci s'en alla justifié dans sa maison, plutôt que celui-là; car quiconque s'élève sera abaissé, et celui qui s'abaisse sera élevé.»
Nawaambia, mtu huyu alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki kuliko yule mwingine, kwa sababu kila ajikwezaye atashushwa, lakini kila mtu anayejinyenyekeza atainuliwa. '
15 Quelques personnes lui amenèrent aussi leurs petits enfants, afin qu'il les touchât. Ses disciples l'ayant vu, reprenaient ces gens;
Watu walimletea watoto wao wachanga, ili aweze kuwagusa, lakini wanafunzi wake walipoona hayo, wakawazuia.
16 mais Jésus appela les enfants, et dit: «Laissez venir vers moi ces petits enfants, et ne les en empêchez pas, car le royaume de Dieu est à ceux qui leur ressemblent.
Lakini Yesu akawaita kwake akisema, 'Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie. Maana ufalme wa Mungu ni wa watu kama hao.
17 En vérité, je vous dis que si l'on ne reçoit pas le royaume de Dieu avec les dispositions d'un petit enfant, l’on n'y entre point.»
Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto ni dhahiri hatauingia. '
18 Alors un président de synagogue lui adressa cette question: «Bon Maître, que dois-je faire pour hériter la vie éternelle?» (aiōnios g166)
Mtawala mmoja akamwuliza, akisema, 'Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?' (aiōnios g166)
19 Jésus lui dit: «Pourquoi m'appelles-tu bon? Dieu seul est bon.
Yesu akamwambia, 'Kwa nini unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema, ila Mungu peke yake.
20 Tu connais les commandements: «Ne commets point adultère; ne tue point; ne dérobe point; ne porte point de faux témoignage; honore ton père et ta mère»
Unazijua amri- usizini, usiue, Usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako.
21 Cet homme répondit: «J'ai gardé tous ces commandements dès ma jeunesse.
Yule mtawala akasema, 'Mambo haya yote nimeyashika tangu nilipokuwa kijana.'
22 Jésus, entendant cette déclaration, lui dit: «Il te manque encore une chose: vends tout ce que tu as, distribue-le aux pauvres, et tu auras un trésor dans les cieux; puis viens, et suis-moi.
Yesu alipoyasikia hayo akamwambia, '“Umepungukiwa jambo moja. Lazima uuze vyote ulivyonavyo na uwagawie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni -kisha njoo, unifuate. '
23 Cet homme ayant entendu ces paroles, devint tout triste, car il était très-riche.
Lakini tajiri aliposikia hayo, alihuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 Jésus, voyant qu'il était devenu fort triste, se mit à dire: «Qu'il est difficile à ceux qui possèdent les richesses d'entrer dans le royaume de Dieu!
Kisha Yesu, akamwona alivyohuzunika sana akasema, 'Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 Car il est plus aisé qu'un chameau passe par un trou d'aiguille, qu'il ne l'est à un riche d'entrer dans le royaume de Dieu.»
Maana ni rahisi sana kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu. '
26 Ceux qui l'écoutaient dirent: «Et qui peut être sauvé?»
Wale waliosikia hayo, wakasema, 'Nani basi, atakayeweza kuokolewa?'
27 Jésus repartit: «Ce qui est impossible aux hommes est possible à Dieu.»
Yesu akajibu, 'Mambo yasiyowezekana kwa mwanadamu kwa Mungu yanawezekana.”
28 — «Pour nous, dit Pierre, tu le vois, nous avons quitté nos propres affaires pour te suivre.»
Petro akasema, 'Naam, sisi tumeacha kila kitu na tumekufuata wewe. '
29 Jésus leur dit: «En vérité, je vous le dis, personne ne quittera maison, ou femme, ou frères, ou parents, ou enfants pour le royaume de Dieu,
Kisha Yesu akawaambia, Amin, nawaambia kwamba hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi au watoto, kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 qu'il ne reçoive beaucoup plus dans le temps présent, et dans le siècle à venir, la vie éternelle.» (aiōn g165, aiōnios g166)
ambaye hatapokea mengi zaidi katika ulimwengu huu, na katika ulimwengu ujao, uzima wa milele. ' (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Jésus prit les Douze près de lui, et leur dit: «Voici que nous montons à Jérusalem, et tout ce que les prophètes ont dit du Fils de l'homme va s'accomplir:
Baada ya kuwakusanya wale kumi na wawibili, akawaambia, 'Tazama, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote ambayo yameandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Adamu yatakamilishwa.
32 on le livrera aux Gentils, on le bafouera, on l'outragera, on crachera sur lui,
Kwa maana atatiwa mikononi mwa watu wa Mataifa na atatendewa dhihaka na jeuri, na kutemewa mate.
33 et, après l'avoir battu de verges, on le mettra à mort; et, le troisième jour, il ressuscitera.»
Baada ya kumchapa viboko watamwua na siku ya tatu atafufuka. '
34 Mais ils n'entendirent rien à tout cela: cette parole était complètement obscure pour eux, et ils ne comprenaient pas ce qu'il leur disait.
Hawakuelewa mambo haya, na neno hili lilikuwa limefichwa kwao, na hawakuelewa mambo yaliyosemwa.
35 Comme il approchait de Jéricho, un aveugle qui était assis au bord de la route, pour mendier,
Ikawa Yesu ulipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya barabara akiomba msaada,
36 entendit la foule passer, et demanda ce que c'était.
aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza nini kinatokea.
37 On lui dit: «C'est Jésus de Nazareth qui passe; »
Wakamwambia kwamba Yesu wa Nazareti anapita.
38 et il cria: «Jésus, fils de David, aie pitié de moi.»
Hivyo yule kipofu akalia kwa sauti, akisema, 'Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.'
39 Ceux qui marchaient en tête, le reprenaient pour lui imposer silence, mais il criait encore plus fort: «Fils de David, aie pitié de moi.»
wale waliokuwa wakitembea walimkemea huyo kipofu, wakamwambia anyamaze. Lakini yeye akazidi kulia kwa sauti, 'Mwana wa Daudi, unirehemu.
40 Jésus s'étant arrêté, ordonna qu'on le lui amenât, et quand l'aveugle se fut approché, il lui demanda:
Yesu akasimama akaamuru mtu yule aletwe kwake. Kisha yule kipofu alipomkaribia, Yesu akamwuliza,
41 «Que veux-tu que je fasse pour toi?» — «Seigneur, dit-il, que je recouvre la vue.»
'Unataka nikufanyie nini?' Akasema, 'Bwana, nataka kuona.'
42 Et Jésus lui dit: «Recouvre la vue, ta foi t'a guéri.»
Yesu akamwambia, 'Upate kuona. Imani yako imekuponya. '
43 A l'instant il recouvra la vue; et il suivit Jésus en glorifiant Dieu. Tout le peuple témoin de cette guérison, se mit à louer Dieu.
Mara hiyo akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Walipoona hili, watu wote wakamsifu Mungu.

< Luc 18 >