< Luc 17 >

1 Il dit à ses disciples: «Il est impossible qu'il n'y ait pas de scandales; mais malheur à celui par qui ils arrivent!
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
2 Il vaudrait mieux pour lui, qu'on lui mît au cou une pierre de moulin, et qu'on le jetât dans la mer, que d'être une occasion de chute pour un seul de ces petits.
Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
3 Prenez donc garde à vous-mêmes. Si ton frère t'a offensé, reprends-le; et, s'il se repent pardonne-lui;
Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
4 et quand il t'offenserait sept fois en un jour, s'il revient sept fois te dire «je me repens, » tu lui pardonneras.»
Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
5 Les apôtres dirent au Seigneur: «Augmente-nous la foi.»
Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
6 Mais le Seigneur leur dit: «Si vous aviez de la foi gros comme un grain de moutarde, vous diriez à ce sycomore: «Déracine-toi, et va te planter dans la mer; » et il vous obéirait.
Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
7 «Qui de vous, ayant un serviteur occupé à labourer ou à paître ses troupeaux, lui dira, à son retour des champs: «Viens vite te mettre à table?»
“Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
8 Ne lui dira-t-il pas au contraire: «Prépare-moi à souper, et ceins-toi pour me servir, jusqu’à ce que j'aie mangé et bu; après quoi, tu mangeras et boiras?»
Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
9 A-t-il de l'obligation à son serviteur, parce qu'il a fait ce qui lui était commandé?
Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
10 Je ne le pense pas. Vous de même, quand vous aurez fait tout ce qui vous est commandé, dites: «Nous sommes des serviteurs inutiles; nous n'avons fait que ce que nous devions faire.»
Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
11 En se rendant à Jérusalem, il lui arriva de passer sur les confins de la Samarie et de la Galilée;
Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
12 et, comme il entrait dans un village, il rencontra dix lépreux qui se tenaient à distance,
Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
13 et qui lui crièrent: «Jésus, Maître, aie pitié de nous.»
wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
14 Jésus les ayant vus, leur dit: «Allez vous montrer aux sacrificateurs; » et, en y allant, ils furent nettoyés de leur lèpre.
Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
15 L'un d'eux, se voyant guéri, revint sur ses pas, glorifiant Dieu à haute voix;
Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
16 il se jeta aux pieds de Jésus, la face contre terre, et lui rendit grâces: c'était un Samaritain.
Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
17 Alors Jésus dit: «Les dix n'ont-ils pas tous été rendus nets? où sont les neuf autres?
Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
18 N'y a-t-il que cet étranger qu'on ait vu revenir donner gloire à Dieu?»
Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
19 Et il lui dit: » Lève-toi, va; ta foi t'a guéri.»
Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
20 Les pharisiens lui ayant demandé quand le royaume de Dieu devait venir, il leur répondit: «Le royaume de Dieu ne vient pas d'une manière qui frappe les regards,
Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
21 et l'on ne dira pas: «il est ici, » ou «il est là; » car voici, le royaume de Dieu est au dedans de vous.»
wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
22 Il dit à ses disciples: «Le temps viendra où vous souhaiterez de voir un jour, un seul des jours du Fils de l'homme, et vous ne le verrez pas.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
23 On vous dira: «Il est là; il est ici; » n'y allez pas, n'y courez pas;
Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
24 car comme l'éclair qui luit, brille d'un bout du ciel à l'autre, ainsi en sera-t-il du Fils de l'homme en son jour.
Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
25 Mais il faut auparavant qu'il souffre beaucoup, et qu'il soit rejeté par cette génération.
Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
26 «Et ce qui se passa au temps de Noé, se passera de même au temps du Fils de l'homme:
“Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
27 on mangeait, on buvait, on prenait et l'on donnait en mariage, jusqu'au jour où Noé entra dans l'arche; et le déluge vint qui les fit tous périr.
Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
28 Et comme au temps de Loth, on mangeait, on buvait, on achetait, on vendait, on plantait, on bâtissait,
“Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
29 mais le jour où Loth quitta Sodome, il tomba du ciel une pluie de feu et de soufre qui les fit tous périr,
Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
30 de même en sera-t-il le jour où le Fils de l'homme paraîtra.
“Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
31 «En ce jour-là, que celui qui sera sur le toit ne descende pas prendre ses effets qui sont dans la maison; de même, que celui qui est aux champs, ne revienne pas en arrière:
Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
32 souvenez- vous de la femme de Loth.
Mkumbukeni mke wa Loti!
33 Celui qui cherchera à conserver sa vie, la perdra; et celui qui l'aura perdue, la retrouvera.
Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
34 Je vous le dis, en cette nuit-là, de deux personnes qui seront dans un même lit, l’une sera prise, l'autre, laissée;
Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
35 de deux femmes qui moudront ensemble, l'une sera prise, l'autre, laissée.»
Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
36 [de deux hommes qui seront aux champs; l’un sera pris, l’autre laissé].
Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
37 Alors ses disciples prenant la parole, lui dirent: «où sera-ce, Seigneur?» Il leur répondit: «Là où sera le cadavre, là aussi s'assembleront les vautours.»
Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”

< Luc 17 >