< Romains 10 >

1 Mes frères, quant à la bonne affection de mon cœur, et à la prière que je fais à Dieu pour Israël, c'est qu'ils soient sauvés.
Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.
2 Car je leur rends témoignage qu'ils ont du zèle pour Dieu, mais sans connaissance.
Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.
3 Parce que ne connaissant point la justice de Dieu, et cherchant d'établir leur propre justice, ils ne se sont point soumis à la justice de Dieu.
Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
4 Car Christ est la fin de la Loi, en justice à tout croyant.
Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.
5 Or Moïse décrit [ainsi] la justice qui est par la Loi, [savoir], que l'homme qui fera ces choses, vivra par elles.
Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
6 Mais la justice qui est par la foi, s'exprime ainsi: ne dis point en ton cœur: qui montera au Ciel? cela est ramener Christ d'en haut.
Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’” (yaani ili kumleta Kristo chini)
7 Ou: qui descendra dans l'abîme? cela est ramener Christ des morts. (Abyssos g12)
“au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos g12)
8 Mais que dit-elle? La parole est près de toi en ta bouche, et en ton cœur. [Or] c'est là la parole de la foi, laquelle nous prêchons.
Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.
9 C'est pourquoi, si tu confesses le Seigneur Jésus de ta bouche, et que tu croies en ton cœur que Dieu l'a ressuscité des morts, tu seras sauvé.
Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
10 Car de cœur on croit à justice, et de bouche on fait confession à salut.
Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
11 Car l'Ecriture dit: quiconque croit en lui ne sera point confus.
Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”
12 Parce qu'il n'y a point de différence du Juif et du Grec; car il y a un même Seigneur de tous, qui est riche envers tous ceux qui l'invoquent.
Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.
13 Car quiconque invoquera le nom du Seigneur sera sauvé.
Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
14 Mais comment invoqueront-ils celui en qui ils n'ont point cru? et comment croiront-ils en celui dont ils n'ont point entendu [parler]? et comment en entendront-ils parler s'il n'y a quelqu'un qui leur prêche?
Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
15 Et comment prêchera-t-on sinon qu'il y en ait qui soient envoyés? ainsi qu'il est écrit: ô que les pieds de ceux qui annoncent la paix sont beaux, [les pieds, dis-je], de ceux qui annoncent de bonnes choses!
Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”
16 Mais tous n'ont pas obéi à l'Evangile; car Esaïe dit: Seigneur, qui est-ce qui a cru à notre prédication.
Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
17 La foi donc est de l'ouïe; et l'ouïe par la parole de Dieu.
Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
18 Mais je demande: ne l'ont-ils point ouï? au contraire, leur voix est allée par toute la terre, et leur parole jusques aux bouts du monde.
Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”
19 Mais je demande: Israël ne l'a-t-il point connu? Moïse le premier dit: je vous exciterai à la jalousie par celui qui n'est point peuple; je vous exciterai à la colère par une nation destituée d'intelligence.
Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”
20 Et Esaïe s'enhardit tout à fait, et dit: j'ai été trouvé de ceux qui ne me cherchaient point, et je me suis clairement manifesté à ceux qui ne s'enquéraient point de moi.
Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”
21 Mais quant à Israël, il dit: j'ai tout le jour étendu mes mains vers un peuple rebelle et contredisant.
Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”

< Romains 10 >