< Psaumes 71 >

1 Eternel! je me suis retiré vers toi, fais que je ne sois jamais confus.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Délivre-moi par ta justice, et me garantis: incline ton oreille vers moi, et me mets en sûreté.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Sois-moi pour un rocher de retraite, afin que je m'y puisse toujours retirer; tu as donné ordre de me mettre en sûreté; car tu es mon rocher, et ma forteresse.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Mon Dieu! délivre-moi de la main du méchant, de la main du pervers, et de l'oppresseur.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 Car tu es mon attente, Seigneur Eternel! [et] ma confiance dès ma jeunesse.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 J'ai été appuyé sur toi dès le ventre [de ma mère]; c'est toi qui m'as tiré hors des entrailles de ma mère; tu es le sujet continuel de mes louanges.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 J'ai été à plusieurs comme un monstre; mais tu es ma forte retraite.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Que ma bouche soit remplie de ta louange, et de ta magnificence chaque jour.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Ne me rejette point au temps de ma vieillesse; ne m'abandonne point maintenant que ma force est consumée.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 Car mes ennemis ont parlé de moi, et ceux qui épient mon âme ont pris conseil ensemble;
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Disant: Dieu l'a abandonné; poursuivez-le, et le saisissez; car il n'y a personne qui le délivre.
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 Ô Dieu! ne t'éloigne point de moi; mon Dieu hâte-toi de venir à mon secours.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Que ceux qui sont ennemis de mon âme soient honteux et défaits; et que ceux qui cherchent mon mal soient enveloppés d'opprobre et de honte.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 Mais moi je vivrai toujours en espérance en toi, et je te louerai tous les jours davantage.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 Ma bouche racontera chaque jour ta justice, [et] ta délivrance, bien que je n'en sache point le nombre.
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 Je marcherai par la force du Seigneur Eternel; je raconterai ta seule justice.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 Ô Dieu! tu m'as enseigné dès ma jeunesse, et j'ai annoncé jusques à présent tes merveilles.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 [Je les ai annoncées] jusqu’à la vieillesse, même jusques à la vieillesse toute blanche; ô Dieu! ne m'abandonne point jusqu’à ce que j'aie annoncé ton bras à cette génération, et ta puissance à tous ceux qui viendront après.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Car ta justice, ô Dieu! est haut élevée, parce que tu as fait de grandes choses. Ô Dieu qui est semblable à toi?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Qui m'ayant fait voir plusieurs détresses et plusieurs maux, m'as de nouveau rendu la vie, et m'as fait remonter hors des abîmes de la terre?
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Tu accroîtras ma grandeur, et tu me consoleras encore.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 Aussi, mon Dieu! je te célébrerai pour l'amour de ta vérité avec l'instrument de la musette; ô Saint d'Israël, je te psalmodierai avec la harpe.
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 Mes lèvres et mon âme, que tu auras rachetée, chanteront de joie, quand je te psalmodierai.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 Ma langue aussi discourra chaque jour de ta justice, parce que ceux qui cherchent mon mal seront honteux et rougiront.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Psaumes 71 >