< Psaumes 48 >

1 Cantique de Psaume, des enfants de Coré. L'Eternel est grand, et fort louable en la ville de notre Dieu, en la montagne de sa Sainteté.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Le plus beau de la contrée, la joie de toute la terre, c'est la montagne de Sion au fond de l'Aquilon; c'est la ville du grand Roi.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Dieu est connu en ses palais pour une haute retraite.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Car voici, les Rois s'étaient donné assignation, ils avaient passé outre tous ensemble.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 L'ont-ils vue? ils en ont été aussitôt étonnés; ils ont été tout troublés, ils s'en sont fuis à l'étourdie.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Là le tremblement les a saisis, [et] une douleur comme de celle qui enfante.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 [Ils ont été chassés comme] par le vent d'Orient [qui] brise les navires de Tarsis.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Comme nous l'avions entendu, ainsi l'avons-nous vu dans la ville de l'Eternel des armées, dans la ville de notre Dieu, laquelle Dieu maintiendra à toujours; (Sélah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 Ô Dieu! nous avons entendu ta gratuité au milieu de ton Temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Ô Dieu! tel qu'est ton Nom, telle [est] ta louange jusqu'aux bouts de la terre; ta droite est pleine de justice.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 La montagne de Sion se réjouira, et les filles de Juda auront de la joie, à cause de tes jugements.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Environnez Sion, et l'entourez, [et] comptez ses tours.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Prenez bien garde à son avant-mur, et considérez ses palais; afin que vous le racontiez à la génération à venir.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 Car c'est le Dieu qui est notre Dieu à toujours et à perpétuité; il nous accompagnera jusques à la mort.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psaumes 48 >