< Josué 1 >

1 Or il arriva après la mort de Moïse, serviteur de l'Eternel, que l'Eternel parla à Josué, fils de Nun, qui avait servi Moïse, en disant:
Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
2 Moïse mon serviteur est mort; maintenant donc lève-toi, passe ce Jourdain, toi et tout ce peuple, pour entrer au pays que je donne aux enfants d'Israël.
“Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
3 Je vous ai donné tout lieu où vous aurez mis la plante de votre pied, selon que je l'ai dit à Moïse.
Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
4 Vos frontières seront depuis ce désert et ce Liban-là, jusqu'à ce grand fleuve, le fleuve d'Euphrate; tout le pays des Héthiens jusqu'à la grande mer, au soleil couchant.
kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
5 Nul ne pourra subsister devant toi tous les jours de ta vie; je serai avec toi comme j'ai été avec Moïse; je ne te délaisserai point, et je ne t'abandonnerai point.
Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
6 Fortifie-toi et te renforce; car c'est toi qui mettras ce peuple en possession du pays dont j'ai juré à leurs pères que je le leur donnerais.
Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
7 Seulement fortifie-toi et te renforce de plus en plus, afin que tu prennes garde de faire selon toute la Loi que Moïse mon serviteur t'a ordonnée; ne t'en détourne point ni à droite ni à gauche, afin que tu prospères partout où tu iras.
Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
8 Que ce livre de la Loi ne s'éloigne point de ta bouche, mais médites-y jour et nuit, afin que tu prennes garde de faire tout ce qui y est écrit; car alors tu rendras heureuses tes entreprises, et alors tu prospéreras.
Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
9 Ne t'ai-je pas commandé, [et dit], fortifie-toi et te renforce? Ne t'épouvante point, et ne t'effraye de rien; car l'Eternel ton Dieu est avec toi partout où tu iras.
Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
10 Après cela Josué commanda aux officiers du peuple, en disant:
Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
11 Passez par le camp, et commandez au peuple, et lui dites: Apprêtez-vous de la provision; car dans trois jours vous passerez ce Jourdain, pour aller posséder le pays que l'Eternel votre Dieu vous donne, afin que vous le possédiez.
“Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
12 Josué parla aussi aux Rubénites, et aux Gadites, et à la demi-Tribu de Manassé, en disant:
Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
13 Souvenez-vous de la parole que Moïse, serviteur de l'Eternel, vous a commandée, en disant: L'Eternel votre Dieu vous met en repos, et vous a donné ce pays.
“Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
14 Vos femmes [donc], vos petits enfants, et vos bêtes demeureront dans le pays que Moïse vous a donné au deçà du Jourdain; mais vous passerez en armes devant vos frères, vous tous qui êtes forts et vaillants, et vous leur serez en secours;
Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
15 Jusqu'à ce que l'Eternel ait mis vos frères en repos, comme vous, et qu'eux aussi possèdent le pays que l'Eternel votre Dieu leur donne; puis vous retournerez au pays de votre possession, et vous le posséderez; [savoir] celui que Moïse serviteur de l'Eternel vous a donné au deçà du Jourdain, vers le soleil levant.
Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
16 Et ils répondirent à Josué, en disant: Nous ferons tout ce que tu nous as commandé, et nous irons partout où tu nous enverras.
Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
17 Nous t'obéirons comme nous avons obéi à Moïse; seulement que l'Eternel ton Dieu soit avec toi, comme il a été avec Moïse.
Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
18 Tout homme qui sera rebelle à ton commandement, et qui n'obéira point à tes paroles en tout ce que tu commanderas, sera mis à mort; seulement fortifie-toi, et te renforce.
Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.

< Josué 1 >