< Josué 9 >

1 Or dès que tous les Rois qui étaient au deçà du Jourdain, en la montagne, et en la plaine, et sur tout le rivage de la grande mer, jusques contre le Liban, [savoir] les Héthiens, les Amorrhéens, les Cananéens, les Phérésiens, les Héviens, et les Jébusiens, eurent appris [ces choses],
Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
2 Ils s'assemblèrent tous pour faire la guerre à Josué et à Israël, d'un commun accord.
wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
3 Mais les habitants de Gabaon ayant entendu ce que Josué avait fait à Jérico, et à Haï;
Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
4 Usèrent de finesse, car ils se mirent en chemin, et contrefirent les ambassadeurs, et prirent de vieux sacs sur leurs ânes, et de vieux outres de vin qui avaient été rompus, et qui étaient rapetassés.
nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
5 Et [ils avaient] en leurs pieds de vieux souliers raccommodés, et de vieux habits sur eux; et tout le pain de leur provision était sec, et moisi.
Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
6 Et étant venus à Josué au camp en Guilgal, ils lui dirent, et aux principaux d'Israël: Nous sommes venus d'un pays éloigné; maintenant donc traitez alliance avec nous.
Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
7 Et les principaux d'Israël répondirent à ces Héviens: Peut-être que vous habitez parmi nous; et comment traiterions-nous alliance avec vous?
Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
8 Mais ils dirent à Josué: Nous sommes tes serviteurs. Alors Josué leur dit: Qui êtes-vous? et d'où venez-vous?
Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
9 Ils lui répondirent: Tes serviteurs sont venus d'un pays fort éloigné, sur la renommée de l'Eternel ton Dieu; car nous avons entendu sa renommée, et toutes les choses qu'il a faites en Egypte;
Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
10 Et tout ce qu'il a fait aux deux Rois des Amorrhéens, qui étaient au delà du Jourdain, à Sihon Roi de Hesbon, et à Hog Roi de Basan qui [demeurait] à Hastaroth.
pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
11 Et nos anciens et tous les habitants de notre pays nous ont dit ces mêmes paroles-ci: Prenez avec vous de la provision pour le chemin, et allez au-devant d'eux, et leur dites: Nous sommes vos serviteurs, et maintenant traitez alliance avec nous.
Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
12 C'est ici notre pain. Nous le prîmes de nos maisons tout chaud pour notre provision, le jour que nous en sortîmes pour venir vers vous; mais maintenant voici, il est devenu sec, et moisi.
Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
13 Et ce sont ici les outres de vin que nous avions remplies tout neufs, et voici ils se sont rompus; et nos habits et nos souliers sont usés à cause du long chemin.
Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
14 Ces hommes donc avaient pris de la provision; mais on ne consulta point la bouche de l'Eternel.
Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
15 Car Josué fit la paix avec eux, et traita avec eux [cette] alliance, qu'il les laisserait vivre; et les principaux de l'assemblée leur en firent le serment.
Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
16 Mais il arriva trois jours après l'alliance traitée avec eux, qu'ils apprirent que c'étaient leurs voisins, et qu'ils habitaient parmi eux.
Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
17 Car les enfants d'Israël partirent, et vinrent en leurs villes le troisième jour. Or leurs villes étaient Gabaon, Képhira, Beeroth, et Kirjath-jéharim.
Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
18 Et les enfants d'Israël ne les frappèrent point, parce que les principaux de l'assemblée leur avaient fait serment par l'Eternel le Dieu d'Israël; mais toute l'assemblée murmura contre les principaux.
Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
19 Alors tous les principaux dirent à toute l'assemblée: Nous leur avons fait serment par l'Eternel le Dieu d'Israël; c'est pourquoi nous ne les pouvons pas maintenant toucher.
lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
20 Faisons leur ceci, et qu'on les laisse vivre, afin qu'il n'y ait point de colère contre nous, à cause du serment que nous leur avons fait.
Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
21 Les principaux donc leur dirent qu'ils vivraient; mais ils furent employés à couper le bois, et à puiser l'eau pour toute l'assemblée, comme les principaux [le] leur dirent.
Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
22 Car Josué les appela, et leur parla, en disant: Pourquoi nous avez-vous trompés, [en nous] disant: Nous sommes fort éloignés de vous; puisque vous habitez parmi nous?
Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
23 Maintenant donc vous êtes maudits, et il y aura toujours des esclaves d'entre vous, et des coupeurs de bois, et des puiseurs d'eau pour la maison de mon Dieu.
Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
24 Et ils répondirent à Josué, et dirent: Après qu'il a été exactement rapporté à tes serviteurs, que l'Eternel ton Dieu avait commandé à Moïse son serviteur qu'on vous donnât tout le pays, et qu'on exterminât tous les habitants du pays de devant vous, nous avons craint extrêmement pour nos personnes à cause de vous, et nous avons fait ceci.
Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
25 Et maintenant nous voici entre tes mains, fais nous comme il te semblera bon et juste de nous faire.
Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
26 Il leur fit donc ainsi, et il les délivra de la main des enfants d'Israël, tellement qu'ils ne les tuèrent point.
Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
27 Et en ce jour-là Josué les établit coupeurs de bois et puiseurs d'eau pour l'assemblée, et pour l'autel de l'Eternel, jusqu'à aujourd'hui dans le lieu qu'il choisirait.
Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.

< Josué 9 >