< Josué 15 >

1 Ce fut ici le sort de la Tribu des enfants de Juda selon leurs familles. Aux confins d'Edom, le désert de Tsin vers le Midi, fut le dernier bout [de leurs pays] vers le Midi.
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
2 Tellement que leur frontière du côté du Midi fut le dernier bout de la mer salée, depuis le bras qui regarde vers le Midi.
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
3 Et elle devait sortir vers le Midi de la montée de Hakrabbim, et passer à Tsin; et, montant du Midi de Kadès-barné passer à Hetsron; puis montant vers Addar se tourner vers Karkah;
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
4 Puis passant vers Hatsmon, sortir au torrent d'Egypte; tellement que les extrémités, de cette frontière devaient se rendre à la mer. Ce sera là, [dit Josué], votre frontière du côté du Midi.
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
5 Et la frontière vers l'Orient sera la mer salée jusqu'au bout du Jourdain; et la frontière du côté du Septentrion sera depuis le bras de la mer, qui est au bout du Jourdain.
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
6 Et cette frontière montera jusqu'à Bethhogla, et passera du côté du Septentrion de Bethharaba; et cette frontière montera jusqu'à la pierre de Bohan, fils de Ruben.
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
7 Puis cette frontière montera vers Débir, depuis la vallée de Hacor, même vers le Septentrion, regardant Guilgal; laquelle est vis-à-vis de la montée d Adummim, qui est au Midi du torrent; puis cette frontière passera vers les eaux de Hen-semès, et ses extrémités se rendront à Hen-roguel.
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
8 Puis cette frontière montera par la vallée du fils de Hinnom, jusqu'au côté de Jébusi vers le Midi, qui est Jérusalem; puis cette frontière montera jusqu'au sommet de la montagne, qui est vis-à-vis de la vallée de Hinnom, vers l'Occident, [et] qui est au bout de la vallée des Réphaïms, vers le Septentrion.
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
9 Et cette frontière s'alignera depuis le sommet de la montagne jusqu'à la fontaine des eaux de Nephtoah, et sortira vers les villes de la montagne de Héphron; puis cette frontière s'alignera à Bahala, qui est Kirjath-jéharim.
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
10 Et cette frontière se tournera depuis Bahala vers l'Occident, jusqu'à la montagne de Séhir; puis elle passera jusqu'au côté de la montagne de Jeharim vers le Septentrion, qui [est] Késalon; puis descendant à Beth-semes, elle passera à Timna.
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
11 Et cette frontière sortira jusqu'au côté de Hekron, vers le Septentrion, et cette frontière s'alignera vers Sikkeron; puis ayant passé la montagne de Bahala, elle sortira à Jabnéël; tellement que les extrémités de cette frontière se rendront à la mer.
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
12 Or la frontière du côté de l'Occident sera ce qui est vers la grande mer, et ses limites. Ce furent les frontières des enfants de Juda de tous les côtés, selon leurs familles.
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
13 Au reste on avait donné à Caleb, fils de Jéphunné, une portion au milieu des enfants de Juda, suivant le commandement de l'Eternel fait à Josué, [savoir] Kirjath-Arbah, [or Arbah était] père de Hanak; [et Kirjath-Arbah] c'est Hébron.
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
14 Et Caleb déposséda de là les trois fils de Hanak, [savoir] Sesaï, Ahiman, et Talmaï, enfants de Hanak.
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
15 Et de là il monta vers les habitants de Débir, dont le nom était auparavant Kirjath-sépher.
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
16 Et Caleb dit: Je donnerai ma fille Hacsa pour femme à celui qui battra Kirjath-sépher, et la prendra.
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
17 Et Hothniel fils de Kénaz, frère de Caleb, la prit; et [Caleb] lui donna sa fille Hacsa pour femme.
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
18 Et il arriva que comme elle s'en allait, elle l'incita à demander à son père un champ; puis elle descendit impétueusement de dessus son âne, et Caleb lui dit: Qu'as-tu?
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
19 Et elle répondit: Donne-moi un présent; puisque tu m'as donné une terre sèche, donne-moi aussi des sources d'eau. Et il lui donna les fontaines de dessus et les fontaines de dessous.
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
20 C'est ici l'héritage de la Tribu des enfants de Juda selon leurs familles.
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
21 Les villes de l'extrémité de la Tribu des enfants de Juda près des limites d'Edom, tirant vers le Midi, furent Kabtséel, Héder, Jagur,
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
22 Kina, Dimona, Hadhada,
Kina, Dimona, Adada,
23 Kedès, Hatsor, Jithnan,
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
24 Ziph, Télem, Béhaloth,
Zifu, Telemu, Bealothi.
25 Hatsor, Hadatta, Kérijoth, Hetsron qui [est] Hatsor,
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
26 Amam, Semah, Molada,
Amamu, shema, Molada,
27 Hatsar-gadda, Hesmon, Beth-pelet,
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
28 Hatsar-suhal, Béersebah, Bizjotheja,
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
29 Bahala, Hijim, Hetsem,
Baala, Limu, Ezemu,
30 Eltolad, Kesil, Hormah,
Eltoladi, Kesili, Horma,
31 Tsiklag, Madmanna, Sansanna,
Ziklagi, Madimana, Sansana,
32 Lebaoth, Silhim, Hajin et Rimmon; en tout vingt-neuf villes, et leurs villages.
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
33 Dans la plaine, Estaol, Tsorha, Asna,
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
34 Zanoah, Hengannim, Tappuah, Hénam,
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
35 Jarmuth, Hadullam, Soco, Hazeka,
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
36 Saharajim, Hadithajim, Guedera et Guederothajim; quatorze villes, et leurs villages.
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
37 Tsénan, Hedasa, Migdal-Gad,
Zena, Hadasha, Migidagadi,
38 Dilhan, Mitspé, Jokthéël,
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
39 Lakis, Botskath, Héglon,
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
40 Cabbon, Lahmas, Kithlis,
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
41 Guederoth, Beth-Dahon, Nahama, et Makkéda; seize villes, et leurs villages.
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
42 Libna, Hether, Hasan,
Libna, Etheri, Ashani,
43 Jiphtah, Asna, Netsib,
Ifuta, Ashina, Nezibu,
44 Kehila, Aczib et Maresa; neuf villes, et leurs villages.
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
45 Hekron, et les villes de son ressort, et ses villages.
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
46 Depuis Hekron, tirant même vers la mer, toutes celles qui [sont] joignant le ressort d'Asdod, et leurs villages.
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Asdod, les villes de son ressort, et ses villages, Gaza, les villes de son ressort, et ses villages, jusqu'au torrent d'Egypte; et la grande mer, et ses limites.
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
48 Et dans la montagne, Samir, Jattir, Soco,
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
49 Danna, Kirjath-sanna, qui est Débir,
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
50 Hanab, Estemo, Hanim,
Anabu, Eshitemo, Animu,
51 Gosen, Holon, et Guilo; onze villes et leurs villages.
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
52 Arab, Duma, Hesehan,
Arabu, Duma, Ehani,
53 Janum, Beth-tappuah, Apheka,
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
54 Humta, Kirjath-Arbah, qui est Hébron, et Tsihor; neuf villes, et leurs villages.
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
55 Mahon, Carmel, Ziph, Juta,
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
56 Jizrehel, Jokdeham, Zanoah,
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
57 Kajin, Guibha, et Timna; dix villes, et leurs villages.
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
58 Halhul, Beth-tsur, Guédor,
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
59 Maharath, Beth-hanoth, et Eltekon; six villes, et leurs villages.
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Kirjath-bahal, qui est Kirjath-jéharim, et Rabba; deux villes, et leurs villages.
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
61 Au désert, Beth-haraba, Middin, Secaca,
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
62 Nibsan, et la ville du sel, et Henguédi: six villes et leurs villages.
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
63 Au reste, les enfants de Juda ne purent point déposséder les Jébusiens qui habitaient à Jérusalem; c'est pourquoi le Jébusien a demeuré avec les enfants de Juda à Jérusalem jusqu'à ce jour.
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.

< Josué 15 >