< Job 33 >

1 C'est pourquoi, Job, écoute, je te prie, mon discours, et prête l'oreille à toutes mes paroles.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Voici maintenant, j'ouvre ma bouche, ma langue parle dans mon palais.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Mes paroles [répondront à la] droiture de mon cœur, et mes lèvres prononceront une doctrine pure.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 L'esprit du [Dieu] Fort m'a fait, et le souffle du Tout-puissant m'a donné la vie.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Si tu peux, réponds-moi, dresse-toi contre moi, demeure ferme.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Voici, je suis pour le [Dieu] Fort; selon que tu en as parlé; j'ai aussi été formé de la terre [tout comme toi].
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Voici, ma frayeur ne te troublera point, et ma main ne s'appesantira point sur toi.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Quoi qu'il en soit, tu as dit, moi l'entendant, et j'ai ouï la voix de tes discours, [disant]:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 Je suis pur, [et] sans péché; je suis net, et il n'y a point d'iniquité en moi.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Voici, il a cherché à rompre avec moi, il me tient pour son ennemi.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Il a mis mes pieds aux ceps, il épie tous mes chemins.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Voici, je te réponds qu'en cela tu n'as pas été juste; car Dieu sera toujours plus grand que l'homme [mortel].
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Pourquoi donc as-tu plaidé contre lui? car il ne rend pas compte de toutes ses actions.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Bien que le [Dieu] Fort parle une première fois, et une seconde fois à celui qui n'aura pas pris garde à la première;
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Par des songes, par des visions de nuit, quand un profond sommeil tombe sur les hommes, et lorsqu'ils dorment dans leur lit;
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Alors il ouvre l'oreille aux hommes, et scelle leur châtiment.
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 Afin de détourner l'homme d'une [mauvaise] action, et de rabaisser la fierté de l'homme.
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 [Ainsi] il garantit son âme de la fosse, et sa vie, de l'épée.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 L'homme est aussi châtié par des douleurs dans son lit, et tous ses os [sont brisés].
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 Alors sa vie lui fait avoir en horreur le pain, et son âme la viande désirable.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Sa chair est tellement consumée qu'elle ne paraît plus; et ses os sont tellement brisés, qu'on n'y connaît plus rien.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Son âme approche de la fosse, et sa vie, des choses qui font mourir.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Que s'il y a pour cet homme-là un messager, qui parle pour lui, (un d'entre mille) qui manifeste à cet homme son devoir,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 Alors il aura pitié de lui, et il dira: Garantis-le, afin qu'il ne descende pas dans la fosse; j'ai trouvé la propitiation.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 Sa chair deviendra plus délicate qu'elle n'était dans son enfance, et il sera rajeuni.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Il fléchira Dieu par ses prières, et Dieu s'apaisera envers lui, et lui fera voir sa face avec joie, et lui rendra sa justice.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Il regardera vers les hommes, et dira: J'avais péché, j'avais renversé le droit, et cela ne m'avait point profité.
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 [Mais Dieu] a garanti mon âme, afin qu'elle ne passât point par la fosse, et ma vie voit la lumière.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Voilà, le [Dieu] Fort fait toutes ces choses, deux [et] trois fois envers l'homme;
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 Pour retirer son âme de la fosse, afin qu'elle soit éclairée de la lumière des vivants.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Sois attentif, Job, écoute-moi; tais-toi, et je parlerai.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Et si tu as de quoi parler, réponds-moi, parle; car je désire de te justifier.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 Sinon, écoute-moi, tais-toi, et je t'enseignerai la sagesse.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >