< Isaïe 30 >

1 Malheur aux enfants revêches, dit l'Eternel, qui prennent conseil, et non pas de moi; et qui se forgent des idoles, où mon esprit n'est point, afin d'ajouter péché sur péché.
Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
2 Qui sans avoir interrogé ma bouche marchent pour descendre en Egypte, afin de se fortifier de la force de Pharaon, et se retirer sous l'ombre d'Egypte.
wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
3 Car la force de Pharaon vous tournera à honte, et la retraite sous l'ombre d'Egypte [vous tournera] à confusion.
Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
4 Car les principaux de son peuple ont été à Tsohan, et ses messagers sont parvenus jusques à Hanès.
Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
5 Tous seront rendus honteux par un peuple qui ne leur profitera de rien, ils n'en recevront aucun secours ni aucun avantage, mais il sera leur honte, et leur opprobre.
kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
6 Les bêtes seront chargées pour aller au Midi; ils porteront leurs richesses sur les dos des ânons, et leurs trésors sur la bosse des chameaux, vers le peuple qui ne leur profitera point, au pays de détresse et d'angoisse, d'où viennent le vieux lion, et le lion, la vipère, et le serpent brûlant qui vole.
Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
7 Car le secours que les Egyptiens leur donneront ne sera que vanité, et qu'un néant; c'est pourquoi j'ai crié ceci; leur force est de se tenir tranquilles.
kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
8 Entre [donc] maintenant, et l'écris en leur présence sur une table, et rédige-le par écrit dans un livre, afin que cela demeure pour le temps à venir, à perpétuité, à jamais;
Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
9 Que c'est ici un peuple rebelle, des enfants menteurs, des enfants qui ne veulent point écouter la Loi de l'Eternel;
Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
10 Qui ont dit aux Voyants; ne voyez point; et à ceux qui voient [des visions]; ne voyez point de visions de justice, mais dites-nous des choses agréables, voyez [des visions] trompeuses.
Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
11 Retirez-vous du chemin, détournez-vous du sentier, faites cesser le Saint d'Israël de devant nous.
Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
12 C'est pourquoi ainsi a dit le Saint d'Israël; parce que vous avez rejeté cette parole, et que vous vous êtes confiés en l'oppression, et en vos moyens obliques, et que vous vous êtes appuyés sur ces choses;
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
13 A cause de cela cette iniquité vous sera comme la fente d'une muraille qui s'en va tomber, faisant ventre jusques au haut, de laquelle la ruine vient soudainement, et en un moment.
dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
14 Il la brisera donc comme on brise une bouteille d'un potier de terre qui est cassée, laquelle on n'épargne point, et des pièces de laquelle ne se trouverait pas un têt pour prendre du feu du foyer, ou pour puiser de l'eau d'une fosse.
Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
15 Car ainsi avait dit le Seigneur, l'Eternel, le Saint d'Israël; en vous tenant tranquilles et en repos vous serez délivrés, votre force sera en vous tenant en repos et en espérance; mais vous ne l'avez point agréé.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
16 Et vous avez dit; non, mais nous nous enfuirons sur des chevaux; à cause de cela vous vous enfuirez. Et [vous avez dit]; nous monterons sur [des chevaux] légers; à cause de cela ceux qui vous poursuivront seront légers.
Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
17 Mille d'entre vous s'enfuiront à la menace d'un seul; vous vous enfuirez à la menace de cinq; jusqu'à ce que vous soyez abandonnés comme un arbre tout ébranché au sommet d'une montagne, et comme un étendard sur un coteau.
Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
18 Et cependant l'Eternel attend pour vous faire grâce, et ainsi il sera exalté en ayant pitié de vous; car l'Eternel est le Dieu de jugement; ô que bienheureux sont tous ceux qui se confient en lui!
Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
19 Car le peuple demeurera dans Sion, et dans Jérusalem; tu ne pleureras point; certes il te fera grâce sitôt qu'il aura ouï ton cri; sitôt qu'il t'aura ouï, il t'exaucera.
Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
20 Le Seigneur vous donnera du pain de détresse, et de l'eau d'angoisse, mais tes Docteurs ne s'envoleront plus, et tes yeux verront tes Docteurs.
Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
21 Et tes oreilles entendront la parole de celui qui sera derrière toi, disant; c'est ici le chemin, marchez-y; soit que vous tiriez à droite, soit que vous tiriez à gauche.
Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
22 Et vous tiendrez pour souillés les chapiteaux des images taillées, faites de l'argent d'un chacun de vous, et les ornements faits de l'or fondu d'un chacun de vous; tu les jetteras au loin, comme un sang impur; et tu diras; videz-le dehors.
Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
23 Et il donnera la pluie sur tes semailles, quand tu auras semé en la terre; et le grain du revenu de la terre sera abondant, et bien nourri; en ce jour-là ton bétail paîtra dans une campagne spacieuse.
Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
24 Et les bœufs et les ânes qui labourent la terre mangeront le pur fourrage de ce qui aura été vanné avec la pelle et le van.
Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
25 Et il y aura des ruisseaux d'eaux courantes sur toute haute montagne, et sur tout coteau haut élevé, au jour de la grande tuerie, quand les tours tomberont.
Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
26 Et la lumière de la lune sera comme la lumière du soleil; et la lumière du soleil sera sept fois aussi grande, comme [si c'était] la lumière de sept jours, au jour que l'Eternel aura bandé la froissure de son peuple, et qu'il aura guéri la blessure de sa plaie.
Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
27 Voici, le Nom de l'Eternel vient de loin, sa colère est ardente, et une pesante charge; ses lèvres sont remplies d'indignation, et sa langue est comme un feu dévorant.
Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
28 Et son Esprit est comme un torrent débordé, qui atteint jusques au milieu du cou, pour disperser les nations, d'une telle dispersion, qu'elles seront réduites à néant; et il est [comme] une bride aux mâchoires des peuples, qui les fera aller à travers champs.
Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
29 Vous aurez un cantique tel que celui de la nuit en laquelle on se prépare à célébrer une fête solennelle; et vous aurez une allégresse de cœur telle qu'a celui qui marche avec la flûte, pour venir en la montagne de l'Eternel, vers le rocher d'Israël.
Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
30 Et l'Eternel fera entendre sa voix, pleine de majesté, et il fera voir où aura assené son bras dans l'indignation de sa colère, avec une flamme de feu dévorant, avec éclat, tempête, et pierres de grêle.
Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
31 Car l'Assyrien, qui frappait du bâton, sera effrayé par la voix de l'Eternel.
Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
32 Et partout ou passera le bâton enfoncé dont l'Eternel l'aura assené, et par lequel il aura combattu dans les batailles à bras élevé, [on y entendra des] tambours et des harpes.
Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
33 Car Topheth est déjà préparée, et même elle est apprêtée pour le Roi; il l'a faite profonde et large; son bûcher c'est du feu, et force bois; le souffle de l'Eternel l'allumant comme un torrent de soufre.
Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.

< Isaïe 30 >