< Isaïe 17 >

1 La charge de Damas; voici, Damas est détruite pour n'être plus ville, et elle ne sera qu'un monceau de ruines.
Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
2 Les villes de Haroher seront abandonnées, elles deviendront des parcs de brebis qui y reposeront, et il n'y aura personne qui les épouvante.
Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 Il n'y aura point de forteresse en Ephraïm, ni de Royaume à Damas, ni dans le reste de la Syrie; ils seront comme la gloire des enfants d'Israël, dit l'Eternel des armées.
Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Et il arrivera en ce jour-là, que la gloire de Jacob sera diminuée, et que la graisse de sa chair sera fondue.
“Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
5 Et il [en] arrivera comme quand le moissonneur cueille les blés, et qu'il moissonne les épis avec son bras; il [en] arrivera, dis-je, comme quand on ramasse les épis dans la vallée des Réphaïns.
Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
6 Mais il y demeurera quelques grappillages, comme quand on secoue l'olivier, et qu'il reste deux ou trois olives au bout des plus hautes branches, et qu'il y en a quatre ou cinq que l'olivier a produites dans ses branches fruitières, dit l'Eternel, le Dieu d'Israël.
Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
7 En ce jour-là, l'homme tournera sa vue vers celui qui l'a fait, et ses yeux regarderont vers le Saint d'Israël.
Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 Et il ne jettera plus sa vue vers les autels qui sont l'ouvrage de ses mains, et ne regardera plus ce que ses doigts auront fait, ni les bocages, ni les tabernacles.
Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
9 En ce jour-là, les villes de sa force, qui auront été abandonnées à cause des enfants d'Israël, seront comme un bois taillis et des rameaux abandonnés, et il y aura désolation.
Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
10 Parce que tu as oublié le Dieu de ton salut, et que tu ne t'es point souvenue du rocher de ta force, à cause de cela tu as transplanté des plantes [tirées des lieux] de plaisance, et tu as planté des provins d'un pays étranger.
Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
11 De jour tu auras fait croître ce que tu auras planté, et le matin tu auras fait lever ta semence; [mais] la moisson sera enlevée au jour que l'on voulait en jouir, et il y aura une douleur désespérée.
hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
12 Malheur à la multitude de plusieurs peuples qui bruient comme bruient les mers; et à la tempête éclatante des nations, qui font du bruit comme une tempête éclatante d'eaux impétueuses.
Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
13 Les nations bruient comme une tempête éclatante de grosses eaux, mais il la menacera, et elle s'enfuira loin; elle sera poursuivie comme la balle des montagnes, chassée par le vent, et comme une boule poussée par un tourbillon.
Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
14 Au temps du soir voici l'épouvante, mais avant le matin il ne sera plus; c'est là la portion de ceux qui nous auront fourragés, et le lot de ceux qui nous auront pillés.
Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.

< Isaïe 17 >