< Osée 9 >

1 Israël ne te réjouis point jusqu'à t'égayer comme les [autres] peuples, de ce que tu as commis adultère, [te retirant] loin de ton Dieu. Tu as aimé le salaire [de la fornication] dans toutes les aires de froment.
Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
2 L'aire et la cuve ne les repaîtra point, et le vin doux leur mentira.
Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
3 Ils ne demeureront point en la terre de l'Eternel, mais Ephraïm retournera en Egypte, et ils mangeront en Assyrie la viande souillée.
Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
4 Ils ne feront point aspersion de vin à l'Eternel, et leurs sacrifices ne lui plairont point; [mais ils] leur seront comme le pain de deuil; tous ceux qui en mangeront seront souillés; parce que leur pain est pour leurs trépassés, il n'entrera point dans la maison de l'Eternel.
Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
5 Que ferez-vous aux jours des fêtes solennelles, et aux jours des fêtes de l'Eternel?
Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
6 Car voici, ils s'en sont allés à cause du dégât; l'Egypte les serrera, Memphis les ensevelira; on ne désirera que leur argent; le chardon sera leur héritier, et l'épine sera dans leurs tabernacles.
Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
7 Les jours de la visitation sont venus, les jours de la rétribution sont venus, et Israël le saura. Les Prophètes sont fous, les hommes de révélation sont insensés à cause de la grandeur de ton iniquité, et de [ta] grande aversion.
Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
8 La sentinelle d'Ephraïm est avec mon Dieu; [mais] le Prophète est un filet d'oiseleur dans tous les chemins d'Ephraïm, il [est] l'aversion contre la maison de son Dieu.
Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
9 Ils se sont extrêmement corrompus, comme aux jours de Guibha; il se souviendra de leur iniquité, il punira leurs péchés.
Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
10 J'avais, [dira-t-il], trouvé Israël comme des grappes dans un désert; j'avais vu vos pères comme un premier fruit en un figuier dans son commencement; [mais] ils sont entrés vers Bahal-péhor, et se sont séparés pour aller après une chose honteuse, et se sont rendus abominables comme ce qu'ils ont aimé.
“Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
11 La gloire d'Ephraïm s'envolera aussi vite qu'un oiseau, dès la naissance, dès le ventre, et dès la conception.
Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
12 Que s'ils élèvent leurs enfants, je les en priverai, [tellement que pas un d'entre eux] ne deviendra homme; car aussi, malheur à eux, quand je me serai retiré d'eux.
Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
13 Ephraïm était comme j'ai vu Tyr, plantée en un lieu agréable, mais néanmoins Ephraïm mènera ses fils au meurtrier.
Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
14 Ô Eternel! donne-leur; [mais] que leur donnerais-tu? donne-leur un sein sujet à avorter, et des mamelles taries.
Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
15 Toute leur méchanceté est à Guilgal; c'est pourquoi je les ai là haïs; je les chasserai de ma maison à cause de la malice de leurs actions; je ne continuerai plus à les aimer; tous les principaux d'entre eux sont revêches.
“Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
16 Ephraïm a été frappé; et leur racine est asséchée, ils ne feront plus de fruit; et s'ils engendrent [des enfants], je mettrai à mort les [fruits] désirables de leur ventre.
Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
17 Mon Dieu les rejettera, parce qu'ils ne l'ont point écouté, et ils seront vagabonds parmi les nations.
Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.

< Osée 9 >