< Ézéchiel 7 >

1 Puis la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Yahwe likanijia, likisema,
2 Et toi, fils d'homme, [écoute]: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel à la terre d'Israël: la fin, la fin [vient] sur les quatre coins de la terre.
Wewe, mwanadamu-Bwana Yahwe asema hivi kwa nchi ya Israeli.”'Mwisho! Mwisho umekuja kwenye mipaka minne ya nchi.
3 Maintenant la fin vient sur toi, et j'enverrai sur toi ma colère, et je te jugerai selon ta voie, et je mettrai sur toi toutes tes abominations.
Sasa mwisho uko juu yako, kwa kuwa natuma ghadhabu yangu juu yako, nitakuhukumu kulingana na njia zako; nitaleta machukizo yako yote juu yako.
4 Et mon œil ne t'épargnera point, et je n'aurai point de compassion; mais je mettrai ta voie sur toi, et tes abominations seront au milieu de toi; et vous saurez que je suis l'Eternel.
Kwa kuwa macho yangu hayatakuhurumia, na sitakuharibu. Badala yake, nitaleta njia zako zote juu yako, na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako, hivyo utajua kwamba mimi ni Yahwe.
5 Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici un mal, un seul mal qui vient.
Bwana Yahwe asema hivi: Msiba! Msiba wa pekee! Tazama, unakuja.
6 La fin vient, la fin vient, elle se réveille contre toi; voici, [le mal] vient.
Mwisho unakuja hakika. Mwisho umeamsha dhidi yenu. Tazama! unakuja!
7 Le matin vient sur toi qui demeures au pays; le temps vient, le jour est près de toi; il ne sera que frayeur, et non point une invitation des montagnes à s'entre-réjouir.
Kifo chako kinakuja kwako ukaaye kwenye nchi. Mda umefika; siku ya uharibifu iko karibu, na milima haitakuwa na shangwe tena.
8 Maintenant je répandrai bientôt ma fureur sur toi, et je consommerai ma colère sur toi, et je te jugerai selon ta voie, je mettrai sur toi toutes tes abominations.
Sasa baada ya mda mfupi nitamwaga dhahabu yangu juu yako na kujaza hasira yangu juu yako wakati nitakapokuhukumu kulingana na njia zako na kuleta machukizo yako yote juu yako.
9 Mon œil ne t'épargnera point, et je n'aurai point de compassion, je te punirai selon ta voie, et tes abominations seront au milieu de toi; et vous saurez que je suis l'Eternel qui frappe.
Kwa kuwa jicho langu halitaona kwa huruma, sitakuharibu, kama ulivyofanya, nitafanya kwako; na machukizo yako yatakuwa katikati yako hivyo utajua kwamba ni mimi Yahwe, anayekuadhibu.
10 Voici le jour, voici il vient, le matin paraît, la verge a fleuri, la fierté a jeté des boutons.
Tazama, siku! Tazama, inakuja! Kifo kimetoka! fimbo ya kuadhibia imechanua, kiburi kimechipua!
11 La violence est crûe en verge de méchanceté; il ne restera rien d'eux, ni de leur multitude, ni de leur tumulte, et on ne les lamentera point.
Udhalimu umekua kwenye fimbo ya udhaifu-hakuna kati yao, na hakuna katika ya kundi lao, hakuna katika utajiri wao, na hakuna wa muhimu wao atakaye baki!
12 Le temps vient, le jour est tout proche: que celui donc qui achète ne se réjouisse point, et que celui qui vend n'en mène point de deuil; car il y a une ardeur de colère sur toute la multitude de son [pays].
Muda unakuja; siku imekaribia. Usimuache anayenunua shangwe, wala asihuzunike auzaye, kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kikundi kizima!
13 Car celui qui vend ne retournera point à ce qu'il aura vendu, quand ils seraient encore en vie; parce que la vision touchant toute la multitude de son [pays] ne sera point révoquée, et chacun [portera] la peine de son iniquité, tant qu'il vivra; ils ne reprendront jamais courage.
Kwa kuwa muuzaji hatarudia kile kilichouzwa, kadiri wanapoendelea kuishi, kwa kuwa maono yako juu yako kikundi kizima. Hawatarudi, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi kwenye dhambi atakayejitia nguvu!
14 Ils ont sonné la trompette, et ils ont tout préparé, mais il n'y a personne qui aille au combat, parce que l'ardeur de ma colère est sur toute la multitude de son [pays].
Wamepiga tarumbeta na kufanya kila kitu tayari, lakini hakuna mtu anayeenda kupigana; kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kundi zima.
15 L'épée est au dehors, et la mortalité et la famine sont au dedans; celui qui sera aux champs, mourra par l'épée; et celui qui sera dans la ville, la famine et la mortalité le dévoreront.
Upanga uko nje, na tauni na njaa viko nje kwenye jengo. Wale walioko shambani watakufa kwa upanga, wakati njaa na tauni zitakapowala wale waliopo kwenye mji.
16 Et les réchappés d'entre eux s'enfuiront, et seront par les montagnes comme les pigeons des vallées, tous gémissants, chacun dans son iniquité.
Lakini watakao salia watatoroka kutoka miongoni mwao, na watakwenda kwenye milima. Kama hua wa mabondeni, wote watalia-kila mtu kwa ajili ya uovu wake.
17 Toutes les mains deviendront lâches, et tous les genoux se fondront en eau.
Kila mkono utasita na kila goti litakuwa dhaifu kama maji, na watavaa nguo za magunia, na hofu kuu itawafunika,
18 Ils se ceindront de sacs, et le tremblement les couvrira, la confusion sera sur tous leurs visages, et leurs têtes deviendront chauves.
na aibu itakuwa juu ya kila uso, na upara juu ya vichwa vyao vyote.
19 Ils jetteront leur argent par les rues, et leur or s'en ira au loin; leur argent ni leur or ne les pourront pas délivrer au jour de la grande colère de l'Eternel; ils ne rassasieront point leurs âmes, et ne rempliront point leurs entrailles, parce que leur iniquité aura été leur ruine.
Watatupa fedha yao kwenye mitaa na dhahabu yao itakuwa kama jalala. Fedha yao na dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe. Maisha yao hayataokolewa, na njaa yao haitashiba, kwa sababu uovu wao umekuwa kizuizi.
20 II avait mis [entre eux] la noblesse de son magnifique ornement; mais ils y ont placé des images de leurs abominations, et de leurs infamies, c'est pourquoi je la leur ai exposée à être chassée au loin.
Kwenye fahari yao walichukua kito yake nzuri za mapambo, pamoja nao wakatengeza sanamu zao za vinyago, na vitu vyao vichukizavyo. Kwa hiyo, nayabadilisha haya kuwa kitu najisi kwao.
21 Et je l'ai livrée en pillage dans la main des étrangers, et en proie aux méchants de la terre, qui la profaneront.
Kisha nitawapatia hivyo vitu kwenye mikono ya wageni kama mateka na kwa waovu wa dunia kama mateka, na watapanajisi.
22 Je détournerai aussi ma face d'eux, et on violera mon lieu secret, et les saccageurs y entreront, et le profaneront.
Kisha nitaugeuza uso wangu mbali kutoka kwao watakapo najisi mahali pangu pa siri; maharamia wataingia humo na kupanajisi.
23 Fais une chaîne; car le pays est plein de crimes de meurtre, et la ville est pleine de violence.
Tengeneza mnyororo, kwa sababu nchi imejaa hukumu ya damu, na mji umejaa udhalimu.
24 C'est pourquoi je ferai venir les plus méchants des nations, qui possèderont leurs maisons, et je ferai cesser l'orgueil des puissants, et leurs saints lieux seront profanés.
Hivyo nitaleta waovu wengi wa mataifa, na watamilki nyumba zao, na nitaleta mwisho kwenye fahari ya uweza, kwenda mahali pao patakatifu patanajisiwa!
25 La destruction vient, et ils chercheront la paix, mais il n'y en aura point.
Hofu itakuja! Wataitafuta amani, lakini haitakuwepo.
26 Malheur viendra sur malheur, et il y aura rumeur sur rumeur; ils demanderont la vision aux Prophètes; la Loi périra chez le Sacrificateur, et le conseil chez les anciens.
Majanga juu ya majanga yatakuja juu yangu, na kutakuwa na tetesi juu ya tetesi. Kisha watatafuta ono moja kutoka kwa nabii, lakini sheria itawaangamiza kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wazee.
27 Le Roi mènera deuil, les principaux se vêtiront de désolation, et les mains du peuple du pays tomberont de frayeur; je les traiterai selon leur voie, et je les jugerai selon qu'ils l'auront mérité; et ils sauront que je suis l'Eternel.
Mfalme ataomboleza na mwana wa mfalme atakata tamaa, wakati mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Kulingana na njia zao wenyewe nitafanya hivi kwao! Nitawahukumu sawa sawa na wanavyostahili hadi watakapojua yakwamba mimi ni Yahwe.'”

< Ézéchiel 7 >