< Ézéchiel 43 >

1 Puis il me ramena vers la porte mentionnée ci-dessus, [savoir] vers la porte qui regardait le chemin de l'Orient.
Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
2 Et voici la gloire du Dieu d'Israël qui venait de devers le chemin de l'Orient, et le bruit qu'il menait, était comme le bruit de beaucoup d'eaux, et la terre resplendissait de sa gloire.
nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
3 Et la vision que j'eus alors était semblable à celle que j'avais vue lorsque j'étais venu pour détruire la ville, tellement que ces visions étaient comme la vision que j'avais vue sur le fleuve de Kébar; et je me prosternai le visage contre terre.
Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
4 Puis la gloire de l'Eternel entra dans la maison par le chemin de la porte qui regardait le chemin de l'Orient.
Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
5 Et l'Esprit m'enleva, et me fit entrer dans le parvis intérieur, et voici la gloire de l'Eternel avait rempli la maison.
Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
6 Et je l'ouïs s'adressant à moi du dedans de la maison, et l'homme [qui me conduisait] était debout près de moi.
Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
7 [L'Eternel] donc me dit: fils d'homme, c'est ici le lieu de mon trône, et le lieu des plantes de mes pieds, dans lequel je ferai ma demeure pour jamais parmi les enfants d'Israël; et la maison d'Israël ne souillera plus mon saint Nom, ni eux, ni leurs Rois, par leurs fornications; [mais plutôt ils] souilleront leurs hauts lieux par les cadavres de leurs Rois.
Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
8 Car ils ont mis leur seuil près de mon seuil, et leur poteau tout joignant mon poteau, tellement qu'il n'y a eu que la paroi entre moi et eux; et ainsi ils ont souillé mon saint Nom par leurs abominations, lesquelles ils ont faites, c'est pourquoi je les ai consumés en ma colère.
Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
9 Maintenant ils rejetteront loin de moi leurs adultères et les cadavres de leurs Rois, et je ferai ma demeure pour jamais parmi eux.
Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
10 Toi donc, fils d'homme, fais entendre à la maison d'Israël ce qui est de ce Temple; et qu'ils soient confus à cause de leurs iniquités; et qu'ils en mesurent le plan.
“Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
11 Quand donc ils auront été confus de tout ce qu'ils ont fait, fais-leur entendre la forme de ce Temple, et sa disposition, avec ses sorties et ses entrées, et toutes ses figures et toutes ses ordonnances, et toutes ses formes, et toutes ses lois, et les écris, eux le voyant, afin qu'ils observent toute la disposition qu'il y faut garder, et toutes les ordonnances qui en auront été établies, et qu'ils les pratiquent.
Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
12 C'est donc ici la Loi de ce Temple; tout l'enclos de ce Temple, sur le haut de la montagne, [sera] un lieu très-saint tout à l'entour. Voilà telle est la Loi de ce Temple.
“Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
13 Mais ce sont ici les mesures de l'autel prises à la coudée, qui vaut une coudée [commune] et une paume. Le sein [de l'autel aura] une coudée de hauteur et une coudée de largeur, et son enclos sur son bord tout à l'entour sera [haut] d'une demi-coudée; ce [sein sera] le dos de l'autel.
“Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
14 Or depuis le sein enfoncé en terre jusques à la saillie d'en bas il y aura deux coudées, et cette saillie aura une coudée de largeur; puis il y aura quatre coudées depuis la petite saillie jusques à la grande saillie, laquelle aura une coudée de largeur.
Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
15 Après cela il y aura l'hariel, [haut] de quatre coudées; puis il y aura quatre cornes [qui sortiront] de l'hariel, et qui [s'élèveront] en haut.
Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
16 Et l'hariel aura douze coudées de longueur, correspondantes à douze coudées de largeur; et il sera carré par ses quatre côtés.
Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
17 Mais chaque saillie aura quatorze coudées de longueur, correspondantes à quatorze coudées de largeur à ses quatre côtés, et elle aura tout à l'entour un enclos [haut] de demi-coudée, parce que chaque saillie aura un sein d'une coudée tout à l'entour, et les endroits par où on y montera regarderont l'Orient.
Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
18 Et il me dit: fils d'homme, ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: ce sont ici les statuts de l'autel pour le jour qu'il aura été fait, afin qu'on y offre l'holocauste, et qu'on y répande le sang.
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
19 C'est que tu donneras aux Sacrificateurs Lévites, qui sont de la race de Tsadok, et qui approchent de moi, dit le Seigneur l'Eternel, afin qu'ils y fassent mon service, un jeune veau en sacrifice pour le péché.
Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
20 Et tu prendras de son sang, et en mettras sur les quatre cornes de l'autel, et sur les quatre coins des saillies, et sur les enclos à l'entour, [et ainsi] tu purifieras l'autel, et feras propitiation pour lui.
Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Puis tu prendras le veau qui [est] le sacrifice pour le péché, et on le brûlera au lieu ordonné de la maison, au dehors du Sanctuaire.
Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
22 Et le second jour tu offriras un bouc d'entre les chèvres, sans tare, en sacrifice pour le péché; et on en purifiera l'autel comme on l'aura purifié avec le veau.
“Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
23 Après que tu auras achevé de purifier l'autel, tu offriras un jeune veau sans tare, et un bélier sans tare, d'entre les brebis;
Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
24 Tu les offriras en la présence de l'Eternel, et les Sacrificateurs jetteront du sel par dessus, et les offriront en holocauste à l'Eternel.
Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
25 Durant sept jours tu sacrifieras chaque jour un bouc, tel qu'on sacrifie pour le péché, et [les Sacrificateurs] sacrifieront un jeune veau et un bélier sans tare, d'entre les brebis.
“Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
26 Durant sept jours [les Sacrificateurs] feront propitiation pour l'autel, et le nettoieront, et chacun d'eux sera consacré.
Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
27 Après qu'on aura achevé ces jours-là, s'il arrive dès le huitième jour, et dans la suite, que les Sacrificateurs sacrifient sur cet autel vos holocaustes et vos sacrifices de prospérité, je serai apaisé envers vous, dit le Seigneur l'Eternel.
Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 43 >