< Ézéchiel 21 >

1 Et la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d'homme, tourne ta face vers Jérusalem, et fais découler [ta parole] vers les saints lieux, et prophétise contre la terre d'Israël.
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 Et dis à la terre d'Israël: ainsi a dit l'Eternel: voici, j'en [veux] à toi, et je tirerai mon épée de son fourreau, et je retrancherai du milieu de toi le juste et le méchant.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Parce que je retrancherai du milieu de toi le juste et le méchant, à cause de cela mon épée sortira de son fourreau contre toute chair, depuis le Midi jusqu'au Septentrion.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 Et toute chair saura que moi l'Eternel j'aurai tiré mon épée de son fourreau, [et] elle n'y retournera plus.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 Aussi toi, fils d'homme gémis en te rompant les reins de douleur, et soupire avec amertume en leur présence.
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 Et quand ils te diront: pourquoi gémis-tu? alors tu répondras: c'est à cause du bruit, car il vient, et tout cœur se fondra, et toutes les mains deviendront lâches, et tout esprit sera étourdi, et tous les genoux se fondront en eau; voici, il vient, et il sera accompli, dit le Seigneur l'Eternel.
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Puis la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 Fils d'homme, prophétise, et dis: ainsi a dit l'Eternel: dis, l'épée, l'épée a été aiguisée, et elle est aussi fourbie.
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 Elle a été aiguisée pour faire un grand carnage, elle a été fourbie afin qu'elle brille: nous réjouirons-nous? C'[est] la verge de mon fils; elle dédaigne tout bois.
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 Et [l'Eternel] l'a donnée à fourbir, afin qu'on la tienne à la main; l'épée a été aiguisée, et elle a été fourbie pour la mettre en la main du destructeur.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Crie et hurle, fils d'homme, car elle est contre mon peuple, elle est contre tous les principaux d'Israël; les frayeurs de l'épée seront sur mon peuple; c'est pourquoi frappe sur ta cuisse.
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 Quand ce serait une épreuve, et que serait-ce? Si même [cette épée] qui dédaigne [tout bois, était] une verge, il n'en serait rien, dit le Seigneur l'Eternel.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Toi donc, fils d'homme, prophétise, et frappe d'une main contre l'autre, et que l'épée soit redoublée pour la troisième fois, l'épée des tués est l'épée contre les grands qui seront tués, passant jusqu'à eux dans leurs cabinets.
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 J'ai mis à toutes leurs portes l'épée luisante, afin que le cœur se fonde, et que les ruines soient multipliées. Ah! elle est faite pour briller et réservée pour tuer.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Joins-toi épée, frappe à la droite; avance-toi, frappe à la gauche, à quelque côté que tu te rencontres.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 Je frapperai aussi d'une main contre l'autre, et je satisferai ma colère: moi l'Eternel j'ai parlé.
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 Et la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 Et toi, fils d'homme, propose-toi deux chemins par où l'épée du Roi de Babylone pourrait venir, [et] que les deux chemins sortent d'un même pays, et les choisis, choisis-les à l'endroit où commence le chemin de la ville de [Babylone].
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Tu te proposeras le chemin par lequel l'épée doit venir contre Rabba des enfants de Hammon, et [le chemin] qui va en Judée, et à Jérusalem, ville forte.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 Car le Roi de Babylone s'est arrêté dans un chemin fourchu, au commencement de deux chemins, pour consulter les devins; il a poli les flèches; il a interrogé les Théraphims; il a regardé au foie.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 Dans sa main droite est la divination contre Jérusalem, pour y disposer les béliers, pour publier la tuerie, pour crier l'alarme à haute voix, pour ranger les béliers contre les portes, pour dresser des terrasses, [et] bâtir des forts.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 Mais ce leur sera comme qui devinerait faussement en leur présence; il y a de grands serments entre eux, mais il va rappeler le souvenir de leur iniquité, afin qu'on y soit surpris.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: parce que vous avez fait revenir le souvenir de votre iniquité, lorsque vos crimes se sont découverts, tellement que vos péchés se voient dans toutes vos actions; parce, [dis-je], que vous avez fait qu'on se souvienne de vous, vous serez surpris avec la main.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 Et toi profane, méchant, Prince d'Israël, le jour duquel est venu au temps de l'iniquité, ce qui fera sa fin.
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel, qu'on ôte cette tiare, et qu'on enlève cette couronne: ce ne sera plus celle-ci; j'élèverai ce qui est bas, et j'abaisserai ce qui est haut.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 Je la mettrai à la renverse, à la renverse, à la renverse, et elle ne sera plus, jusqu'à ce que vienne celui auquel appartient le gouvernement, et je le lui donnerai.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 Et toi, fils d'homme, prophétise, et dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel touchant les enfants de Hammon, et touchant leur opprobre; dis donc, épée, épée dégainée, fourbie pour faire la tuerie, pour consumer avec son éclat.
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 Pendant qu'on voit pour toi des visions de vanité, et qu'on devine pour toi le mensonge, afin qu'on te mette sur le cou des méchants qui sont mis à mort; le jour desquels est venu au temps de l'iniquité, ce qui sera sa fin.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 La remettrait-on dans son fourreau? je te jugerai sur le lieu auquel tu as été créé, au pays de ton extraction.
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 Je répandrai mon indignation sur toi, j'allumerai sur toi le feu de ma fureur, et je te livrerai entre les mains d'hommes brutaux, et forgeurs de destruction.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Tu seras destiné au feu pour être dévoré; ton sang sera au milieu de la terre: on ne se souviendra plus de toi, car c'est moi l'Eternel, qui ai parlé.
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”

< Ézéchiel 21 >