< Exode 10 >

1 Et l'Eternel dit à Moïse: va vers Pharaon, car j'ai endurci son cœur, et le cœur de ses serviteurs, afin que je mette au-dedans de lui les signes que je m'en vais faire.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
2 Et afin que tu racontes, ton fils et le fils de ton fils l'entendant, ce que j'aurai fait en Egypte, et mes signes que j'aurai faits entre eux; et vous saurez que je [suis] l'Eternel.
ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
3 Moïse donc et Aaron vinrent vers Pharaon, et lui dirent: ainsi a dit l'Eternel le Dieu des Hébreux: jusques à quand refuseras-tu de t'humilier devant ma face? Laisse aller mon peuple afin qu'ils me servent.
Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
4 Car si tu refuses de laisser aller mon peuple, voici, je m'en vais faire venir demain des sauterelles en tes contrées
Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
5 Qui couvriront toute la face de la terre, tellement qu'on ne pourra voir la terre: et qui brouteront le reste de ce qui est échappé, que la grêle vous a laissé; et brouteront tous les arbres qui poussent dans les champs.
Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
6 Et elles rempliront tes maisons, et les maisons de tous tes serviteurs; et les maisons de tous les Egyptiens; ce que tes pères n'ont point vu, ni les pères de tes pères, depuis le jour qu'ils ont été sur la terre, jusqu'à aujourd'hui. Puis ayant tourné le dos à Pharaon, il sortit d'auprès de lui.
Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
7 Et les serviteurs de Pharaon lui dirent: jusques à quand celui-ci nous tiendra-t-il enlacés? Laisse aller ces gens, et qu'ils servent l'Eternel leur Dieu. [Attendras-]tu de savoir avant cela que l'Egypte est perdue?
Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
8 Alors on fit revenir Moïse et Aaron vers Pharaon; et il leur dit: allez, servez l'Eternel votre Dieu. Qui sont tous ceux qui iront?
Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
9 Et Moïse répondit: nous irons avec nos jeunes gens et nos vieillards, avec nos fils et nos filles, avec notre menu et gros bétail; car nous avons [à célébrer] une fête solennelle à l'Eternel.
Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
10 Alors il leur dit: que l'Eternel soit avec vous, comme je laisserai aller vos petits enfants; prenez garde, car le mal est devant vous.
Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
11 Il n'en sera [donc] pas ainsi [que vous l'avez demandé], mais vous hommes, allez maintenant, et servez l'Eternel; car c'est ce que vous demandez. Et on les chassa de devant Pharaon.
La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
12 Alors l'Eternel dit à Moïse: étends ta main sur le pays d'Egypte [pour faire] venir les sauterelles, afin qu'elles montent sur le pays d'Egypte, et qu'elles broutent toute l'herbe de la terre, et tout ce que la grêle a laissé de reste.
Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
13 Moïse donc étendit sa verge sur le pays d'Egypte, et l'Eternel amena sur la terre un vent Oriental tout ce jour-là et toute la nuit; [et] au matin le vent Oriental eut enlevé les sauterelles.
Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
14 Et il fit monter les sauterelles sur tout le pays d'Egypte, et les mit dans toutes les contrées d'Egypte, elles étaient fort grosses, et il n'y en avait point eu de semblables avant elles, et il n'y en aura point de semblables après elles.
Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
15 Et elles couvrirent la face de tout le pays, tellement que la terre en fut couverte; et elles broutèrent toute l'herbe de la terre, et tout le fruit des arbres que la grêle avait laissé, et il ne demeura aucune verdure aux arbres, ni aux herbes des champs, dans tout le pays d'Egypte.
Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
16 Alors Pharaon fit appeler en toute diligence Moïse et Aaron, et [leur] dit: j'ai péché contre l'Eternel votre Dieu, et contre vous.
Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
17 Mais maintenant, je te prie, pardonne-moi mon péché, seulement pour cette fois; et fléchissez l'Eternel votre Dieu par prières, afin qu'il retire de moi cette mort-ci seulement.
Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
18 Il sortit donc d'auprès de Pharaon, et il fléchit l'Eternel par prières.
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
19 Et l'Eternel fit lever à l'opposite un vent très-fort de l'Occident, qui enleva les sauterelles, et les enfonça dans la mer rouge. Il ne resta pas une seule sauterelle dans toutes les contrées d'Egypte.
Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
20 Mais l'Eternel endurcit le cœur de Pharaon, et il ne laissa point aller les enfants d'Israël.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
21 Puis l'Eternel dit à Moïse: Etends ta main vers les cieux, et qu'il y ait sur le pays d'Egypte des ténèbres [si épaisses], qu'on les puisse toucher à la main.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
22 Moïse donc étendit sa main vers les cieux; et il y eut des ténèbres fort obscures en tout le pays d'Egypte durant trois jours.
Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
23 L'on ne se voyait pas l'un l'autre, et nul ne se leva du lieu où il était pendant trois jours; mais il y eut de la lumière pour les enfants d'Israël dans le lieu de leurs demeures.
Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
24 Alors Pharaon appela Moïse, et lui dit: allez, servez l'Eternel; seulement que votre menu et gros bétail demeurent; même vos petits enfants iront avec vous.
Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
25 Mais Moïse répondit: tu nous laisseras aussi amener les sacrifices et les holocaustes que nous ferons à l'Eternel notre Dieu.
Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
26 Et même nos troupeaux viendront avec nous, sans qu'il en demeure un ongle; car nous en prendrons pour servir à l'Eternel notre Dieu; et nous ne savons pas ce que nous offrirons à l'Eternel, jusques à ce que nous soyons parvenus en ce lieu-là.
Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
27 Mais l'Eternel endurcit le cœur de Pharaon, et il ne voulut point les laisser aller.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
28 Et Pharaon lui dit: va-t'en arrière de moi; donne-toi de garde de voir plus ma face; car au jour où tu verras ma face, tu mourras.
Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
29 Et Moïse répondit: tu as bien dit; je ne verrai plus ta face.
Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”

< Exode 10 >