< Esther 1 >

1 Or il arriva au temps d'Assuérus, qui régnait depuis les Indes jusqu'en Ethiopie, sur cent vingt-sept provinces;
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
2 [Il arriva, dis-je], en ce temps-là, que le Roi Assuérus étant assis sur le trône de son règne à Susan, la ville capitale;
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
3 La troisième année de son règne, il fit un festin à tous les principaux Seigneurs de ses pays, et à ses serviteurs, de sorte que la puissance de la Perse et de la Médie, [savoir] les plus grands Seigneurs, et les Gouverneurs des provinces étaient devant lui;
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
4 Pour montrer les richesses de la gloire de son Royaume, et la splendeur de l'excellence de sa grandeur, durant plusieurs jours; [savoir] cent quatre-vingts jours.
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
5 Et au bout de ces jours-là, le Roi fît un festin pendant sept jours, dans le parvis du jardin du palais Royal, à tout le peuple qui se trouva dans Susan, la ville capitale, depuis le plus grand jusqu'au plus petit.
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
6 [Les tapisseries] de blanc, de vert et de pourpre tenaient avec des cordons de fin lin et d'écarlate à des anneaux d'argent, et à des piliers de marbre; les lits étaient d'or et d'argent sur un pavé de porphyre, de marbre, d'albâtre, et de marbre tacheté.
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
7 Et on donnait à boire en vaisselle d'or, qui était en diverses façons; et il y avait du vin Royal en abondance, selon l'opulence du Roi.
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
8 Et la manière de boire fut telle qu'on l'avait ordonné. On ne contraignait personne; car le Roi avait ainsi expressément commandé à tous ses maîtres d'hôtel, de faire selon la volonté de chacun.
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
9 Et Vasti la Reine fit aussi un festin aux femmes dans la maison Royale, qui [était] au Roi Assuérus.
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
10 Or au septième jour, comme le Roi avait le cœur gai de vin, il commanda à Méhuman, Bizta, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zéthar, et Carcas, les sept Eunuques qui servaient devant le Roi Assuérus,
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
11 Qu'ils amenassent devant lui la Reine Vasti, portant la couronne Royale, afin de faire voir sa beauté aux peuples et aux Seigneurs; car elle était belle à voir.
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 Mais la Reine Vasti refusa de venir au commandement que le Roi lui fit faire par les Eunuques; et le Roi se mit en fort grande colère, et sa colère s'embrasa au dedans de lui.
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
13 Alors le Roi dit aux Sages qui avaient la connaissance des temps, (car le Roi communiquait ainsi avec tous ceux qui connaissaient les lois et le droit;
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
14 Et alors Carséna, Séthar, Admatha, Tarsis, Mérès, Marséna, [et] Mémucan, sept Seigneurs de Perse et de Médie, étaient proches de lui, qui voyaient la face du Roi, et ils avaient les premiers sièges dans le Royaume.)
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15 Qu'y a-t-il à faire selon les lois à la Reine Vasti, pour n'avoir pas exécuté le commandement que le Roi Assuérus lui a envoyé faire par les Eunuques?
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
16 Alors Mémucan parla en présence du Roi et des Seigneurs, [disant]: La Reine Vasti n'a pas seulement mal agi contre le Roi, mais aussi contre tous les Seigneurs, et contre tous les peuples qui sont dans toutes les provinces du Roi Assuérus.
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
17 Car l'action de la Reine viendra [à la connaissance] de toutes les femmes, pour leur faire mépriser leurs maris, quand on dira: Le Roi Assuérus avait commandé qu'on lui amenât la Reine, et elle n'y est pas venue.
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
18 Et aujourd'hui les Dames de Perse et de Médie qui auront appris la réponse de la Reine, répondront [ainsi] à tous les Seigneurs [des pays] du Roi; et comme ce sera une marque de mépris, ce sera aussi un sujet d'emportement.
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
19 Si le Roi donc le trouve ainsi bon, qu'un Edit Royal soit publié de sa part, et qu'il soit écrit entre les ordonnances de Perse et de la Médie, et qu'il soit irrévocable; [savoir] que Vasti ne vienne plus devant le Roi Assuérus; et que le Roi donne son Royaume à sa compagne, [qui sera] meilleure qu'elle.
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
20 Et l'Edit, que le Roi aura fait ayant été su par tout son Royaume, quelque grand qu'il soit, toutes les femmes honoreront leurs maris, depuis le plus grand jusqu'au plus petit.
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
21 Et cette parole plut au Roi et aux Seigneurs; et le Roi fit selon la parole de Mémucan.
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
22 Il envoya des lettres par toutes les provinces du Roi, à chaque province selon sa manière d'écrire, et à chaque peuple selon sa langue, afin que chacun fût maître en sa maison, et parlant selon la langue de son peuple.
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< Esther 1 >