< 2 Rois 10 >

1 Or Achab avait soixante et dix fils à Samarie. Et Jéhu écrivit des Lettres et les envoya à Samarie aux principaux de Jizréhel, aux Anciens, et aux nourriciers d'Achab, leur mandant en ces termes:
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 Aussitôt que ces Lettres vous seront parvenues, à vous, qui avez avec vous les fils de votre maître, les chariots, les chevaux, la ville forte, et les armes;
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 Regardez qui est le plus considérable et le plus agréable d'entre les fils de votre maître, et mettez-le sur le trône de son père, et combattez pour la maison de votre maître.
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 Et ils eurent une très-grande peur, et dirent: Voilà, deux Rois n'ont point pu tenir contre lui, comment donc pourrions-nous nous soutenir?
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 Ceux-là donc qui avaient la charge de la maison, et ceux qui étaient commis sur la ville, et les Anciens, et les nourriciers mandèrent à Jéhu, en disant: Nous sommes tes serviteurs, nous ferons tout ce que tu nous diras; nous ne ferons personne Roi, fais ce qui te semblera bon.
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 Et il leur écrivit des Lettres pour la seconde fois, en ces termes: Si vous êtes à moi, et si vous obéissez à ma voix, prenez les têtes des fils de votre maître, et venez vers moi demain à cette heure-ci à Jizréhel. Or les fils du Roi, qui étaient soixante et dix-hommes, étaient avec les plus grands de la ville qui les nourrissaient.
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 Aussitôt donc que ces Lettres leur furent parvenues, ils prirent les fils du Roi, et mirent à mort soixante et dix hommes, et ayant mis leurs têtes dans des paniers, ils les lui envoyèrent à Jizréhel.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 Et un messager vint qui le lui rapporta, et dit: Ils ont apporté les têtes des fils du Roi. Et il répondit: Mettez-les en deux monceaux à l'entrée de la porte, jusqu'au matin.
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 Et il sortit au matin, et s'étant arrêté, il dit à tout le peuple: Vous êtes justes; voici j'ai fait une ligue contre mon Seigneur, et je l'ai tué; et qui est-ce qui a frappé tous ceux-ci?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Sachez maintenant qu'il ne tombera rien en terre de la parole de l'Eternel, laquelle l'Eternel a prononcée contre la maison d'Achab; et que l'Eternel a fait ce dont il avait parlé par le moyen de son serviteur Elie.
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 Jéhu tua aussi tous ceux qui étaient demeurés de reste de la maison d'Achab à Jizréhel, et tous ceux qu'il avait avancés et ses familiers amis, et ses principaux officiers, en sorte qu'il ne lui en laissa pas un de reste.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 Puis il se leva, et partit, et alla à Samarie; et comme il fut près d'une cabane de bergers sur le chemin,
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 Il trouva les frères d'Achazia Roi de Juda, et il leur dit: Qui êtes-vous? Et ils répondirent: Nous sommes les frères d'Achazia, et nous sommes descendus pour saluer les fils du Roi, et les fils de la reine.
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 Et il dit: Empoignez-les vifs. Et ils les empoignèrent tous vifs, et les mirent à mort, [savoir] quarante-deux hommes, auprès du puits de la cabane des bergers, et on n'en laissa pas un de reste.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 Et [Jéhu] étant parti de là, trouva Jonadab fils de Réchab, qui venait au-devant de lui, lequel il salua, et lui dit: Ton cœur est-il aussi droit [envers moi] que mon cœur l'est à ton égard? Et Jonadab répondit: Il l'est; oui il l'est, donne-moi ta main; et il lui donna sa main, et le fit monter avec lui dans le chariot.
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 Puis il dit: Viens avec moi, et tu verras le zèle que j'ai pour l'Eternel. Ainsi on le mena dans son chariot.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 Et quand [Jéhu] fut venu à Samarie, il tua tous ceux qui étaient demeurés de reste [de la maison] d'Achab à Samarie, jusqu'à ce qu'il eût tout exterminé, selon la parole que l'Eternel avait dite à Elie.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 Puis Jéhu assembla tout le peuple, et leur dit: Achab n'a servi qu'un peu Bahal; mais Jéhu le servira beaucoup.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 Maintenant donc appelez-moi tous les Prophètes de Bahal, tous ses serviteurs, et tous ses Sacrificateurs; qu'il n'y en manque pas un, car j'ai à faire un grand sacrifice à Bahal. Quiconque ne s'y trouvera pas il ne vivra point. Or Jéhu faisait cela par finesse, pour faire périr les serviteurs de Bahal.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 Et Jéhu dit: Sanctifiez une fête solennelle à Bahal; et ils la publièrent.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 Et Jéhu envoya par tout Israël, et tous les serviteurs de Bahal vinrent; il n'y en eut pas un qui n'y vînt; et ils entrèrent dans la maison de Bahal, et la maison de Bahal fut remplie depuis un bout jusqu'à l'autre.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 Alors il dit à celui qui avait la charge du revestiaire: Tires-en des vêtements pour tous les serviteurs de Bahal; et il leur en tira des vêtements.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 Et Jéhu et Jonadab fils de Réchab entrèrent dans la maison de Bahal, et [Jéhu] dit aux serviteurs de Bahal: Cherchez diligemment, et regardez que par hasard il n'y ait ici entre vous quelqu'un des serviteurs de l'Eternel; et prenez garde qu'il n'y ait que les seuls serviteurs de Bahal.
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 Ils entrèrent donc pour faire des sacrifices et des holocaustes. Or Jéhu avait fait mettre par dehors quatre-vingts hommes, et leur avait dit: S'il y a quelqu'un de ces hommes que je m'en vais mettre entre vos mains, qui en échappe, la vie de chacun de vous répondra pour la vie de cet homme.
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 Et il arriva que dès qu'on eut achevé de faire l'holocauste, Jéhu dit aux archers et aux capitaines: Entrez, tuez-les, [et] que nul n'échappe. Les archers donc et les capitaines les passèrent au fil de l'épée, et les jetèrent là, puis ils s'en allèrent jusqu'à la ville de la maison de Bahal.
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 Et ils tirèrent dehors les statues de la maison de Bahal, et les brûlèrent.
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 Et ils démolirent la statue de Bahal. Ils démolirent aussi la maison de Bahal, et la firent [servir] de retraits, jusqu'à ce jour.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 Ainsi Jéhu extermina Bahal d'Israël.
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 Toutefois Jéhu ne se détourna point des péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël, [savoir] des veaux d'or qui étaient à Bethel, et à Dan.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 Et l'Eternel dit à Jéhu: Parce que tu as fort bien exécuté ce qui était droit devant moi, et que tu as fait à la maison d'Achab tout ce que j'avais en mon cœur, tes fils seront assis sur le trône d'Israël jusqu'à la quatrième génération.
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 Mais Jéhu ne prit point garde à marcher de tout son cœur dans la loi de l'Eternel le Dieu d'Israël, [et] il ne se détourna point des péchés de Jéroboam par lesquels il avait fait pécher Israël.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 En ce temps-là l'Eternel commença à retrancher [quelque partie du Royaume] d'Israël, car Hazaël battit les Israëlites dans toutes les frontières.
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 Depuis le Jourdain jusqu'au soleil levant [savoir] dans tout le pays de Galaad, des Gadites, des Rubénites, et de ceux de Manassé, depuis Haroher, qui est sur le torrent d'Arnon, jusqu'en Galaad et en Basan.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 Le reste des faits de Jéhu, tout ce, [dis-je], qu'il a fait, et tous ses exploits, ne sont-ils pas écrits au Livre des Chroniques des Rois d'Israël.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 Et Jéhu s'endormit avec ses pères, et fut enseveli à Samarie; et Joachaz son fils régna en sa place.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 Or les jours que Jéhu régna sur Israël à Samarie furent vingt-huit ans.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< 2 Rois 10 >