< 2 Chroniques 26 >

1 Alors tout le peuple de Juda prit Hozias, qui était âgé de seize ans, et ils l'établirent Roi en la place d'Amatsia son père.
Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
2 Il bâtit Eloth, l'ayant remise en la puissance de Juda, après que le Roi se fut endormi avec ses pères.
Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
3 Hozias [était] âgé de seize ans quand il commença à régner, et régna cinquante-deux ans à Jérusalem. Sa mère avait nom Jécolia, [et] elle était de Jérusalem.
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
4 Il fit ce qui est droit devant l'Eternel, comme avait fait Amatsia son père.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
5 Il s'appliqua à rechercher Dieu pendant les jours de Zacharie, [homme] intelligent dans les visions de Dieu; et pendant les jours qu'il rechercha l'Eternel, Dieu le fit prospérer.
Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
6 Car il sortit et fit la guerre contre les Philistins, et fit brèche à la muraille de Gath, et à la muraille de Jabné, et à la muraille d'Asdod; et il bâtit des villes [dans le pays] d'Asdod, et entre les [autres] Philistins.
Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
7 Et Dieu lui donna du secours contre les Philistins, et contre les Arabes qui habitaient à Gur-bahal, et contre les Méhunites.
Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
8 Et même les Hammonites donnaient des présents à Hozias; de sorte que sa réputation se répandit jusqu'à l'entrée d'Egypte; car il s'était rendu fort puissant.
Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
9 Et Hozias bâtit des tours à Jérusalem, sur la porte du coin, et sur la porte de la vallée, et sur l'encoignure, et les fortifia.
Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
10 Il bâtit aussi des tours au désert, et creusa plusieurs puits, parce qu'il avait beaucoup de bétail dans la plaine et dans la campagne; et des laboureurs et des vignerons dans les montagnes, et en Carmel; car il aimait l'agriculture.
Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
11 Et Hozias avait une armée composée de gens dressés à la guerre, qui marchaient en bataille par bandes, selon le compte de leur dénombrement, fait par Jéhiël scribe, et Mahaséja prévôt, sous la conduite de Hanania, l'un des principaux capitaines du Roi.
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
12 Tout le nombre des Chefs des pères, d'entre ceux qui étaient forts et vaillants, était de deux mille et six cents.
Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
13 Et il y avait sous leur conduite une armée de trois cent sept mille et cinq cents combattants, tous gens aguerris, forts et vaillants, pour aider le Roi contre l'ennemi.
Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
14 Et Hozias leur prépara, [savoir] à toute cette armée-là, des boucliers, des javelines, des casques, des cuirasses, des arcs, et des pierres de fronde.
Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
15 Et il fit à Jérusalem des machines de l'invention d'un ingénieur, afin qu'elles fussent sur les tours, et sur les coins, pour jeter des flèches, et de grosses pierres. Ainsi sa réputation alla fort loin; car il fut extrêmement aidé jusqu'à ce qu'il fût devenu fort puissant.
Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
16 Mais sitôt qu'il fut devenu fort puissant, son cœur s'éleva pour sa perte, et il commit un [grand] péché contre l'Eternel son Dieu; car il entra dans le Temple de l'Eternel pour faire le parfum sur l'autel des parfums.
Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
17 Mais Hazaria le Sacrificateur [y] entra après lui, accompagné des Sacrificateurs de l'Eternel, au nombre de quatre-vingts vaillants hommes;
Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
18 Qui s'opposèrent au Roi Hozias, et lui dirent: Hozias! il ne t'appartient pas de faire le parfum à l'Eternel; car cela appartient aux Sacrificateurs, fils d'Aaron, qui sont consacrés pour faire le parfum. Sors du Sanctuaire, car tu as péché; et ceci ne te sera point honorable de la part de l'Eternel Dieu.
Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
19 Alors Hozias, qui avait en sa main le parfum pour faire des encensements, se mit en colère; et comme il s'irritait contre les Sacrificateurs, la lèpre s'éleva sur [son] front, en la présence des Sacrificateurs, dans la maison de l'Eternel, près de l'autel des parfums.
Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
20 Alors Hazaria le principal Sacrificateur le regarda avec tous les sacrificateurs, et voilà, il était lépreux en son front, et ils le firent incessamment sortir; et il se hâta de sortir, parce que l'Eternel l'avait frappé.
Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
21 Et ainsi le Roi Hozias fut lépreux, jusqu'au jour qu'il mourut; et il demeura lépreux dans une maison écartée; même il fut retranché de la maison de l'Eternel, et Jotham son fils avait la charge de la maison du Roi, jugeant le peuple du pays.
Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
22 Or Esaïe fils d'Amots, Prophète, a écrit le reste des faits d'Hozias, tant les premiers que les derniers.
Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23 Et Hozias s'endormit avec ses pères, et fut enseveli avec eux dans le champ des sépulcres des Rois; car, ils dirent, il est lépreux; et Jotham son fils régna en sa place.
Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 26 >