< 2 Chroniques 23 >

1 Mais en la septième année Jéhojadah se fortifia, et prit avec soi des centeniers; [savoir] Hazaria fils de Jéroham, Ismahël fils de Jéhohanan, Hazaria fils de Hobed, Mahaséja fils de Hadaja, Elisaphat fils de Zicri, et traita alliance avec eux.
Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.
2 Et ils firent le tour de Juda, et assemblèrent de toutes les villes de Juda les Lévites, et les Chefs des pères d'Israël, et vinrent à Jérusalem.
Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu,
3 Et toute cette assemblée traita alliance avec le Roi dans la maison de Dieu, et [Jéhojadah] leur dit: Voici, le fils du Roi régnera selon que l'Eternel en a parlé touchant les fils de David.
kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu. Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi.
4 C'est ici [donc] ce que vous ferez: La troisième partie de ceux d'entre vous qui entrerez en semaine, tant des Sacrificateurs, que des Lévites, sera à la porte de Sippim.
Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni,
5 Et la troisième partie se tiendra vers la maison du Roi; et la troisième partie à la porte du fondement; et que tout le peuple soit dans les parvis de la maison de l'Eternel.
theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana.
6 Que nul n'entre dans la maison de l'Eternel, que les Sacrificateurs et les Lévites servants; ceux-ci y entreront, parce qu'ils sont sanctifiés; et le reste du peuple fera la garde de l'Eternel.
Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana.
7 Et ces Lévites-là environneront le Roi tout autour, ayant chacun ses armes en sa main; mais que celui qui entrera dans la maison, soit mis à mort; et tenez-vous auprès du Roi quand il sortira et quand il entrera.
Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
8 Les Lévites donc et tous ceux de Juda firent tout ce que Jéhojadah le Sacrificateur avait commandé, et prirent chacun ses gens, tant ceux qui entraient en semaine que ceux qui sortaient de semaine; car Jéhojadah le Sacrificateur n'avait point donné congé aux départements.
Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke.
9 Et Jéhojadah le sacrificateur donna aux centeniers des hallebardes, des boucliers, et des rondelles, qui avaient été au Roi David, et qui étaient dans la maison de Dieu.
Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu.
10 Et il rangea tout le peuple, tout autour du Roi; chacun tenant ses armes en sa main, depuis le côté droit du Temple jusqu'au côté gauche du Temple, tant pour l'autel, que pour le Temple.
Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
11 Alors on amena le fils du Roi, et on mit sur lui la couronne et le témoignage, et ils l'établirent Roi; et Jéhojadah et ses fils l'oignirent, et dirent: Vive le Roi!
Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
12 Et Hathalie entendant le bruit du peuple qui courait, et qui chantait les louanges [de Dieu] autour du Roi, vint vers le peuple en la maison de l'Eternel.
Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana.
13 Et elle regarda, et voilà, le Roi était près de sa colonne à l'entrée, et les capitaines, et les trompettes étaient près du Roi, et tout le peuple du pays était en joie, et on sonnait des trompettes; les chantres aussi [chantaient] avec des instruments de musique, et montraient comment il fallait chanter les louanges [de Dieu]; et sur cela Hathalie déchira ses vêtements, et dit: Conjuration! conjuration!
Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”
14 Alors le Sacrificateur Jéhojadah fit sortir les centeniers, qui avaient la charge de l'armée, et leur dit: Menez-la hors des rangs; et que celui qui la suivra, soit mis à mort par l'épée; car le Sacrificateur avait dit: Ne la mettez point à mort dans la maison de l'Eternel.
Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.”
15 Ils lui firent donc place; et elle s'en retourna en la maison du Roi par l'entrée de la porte des chevaux, et ils la firent mourir là.
Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.
16 Et Jéhojadah, tout le peuple, et le Roi traitèrent cette alliance, qu'ils seraient le peuple de l'Eternel.
Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana.
17 Alors tout le peuple entra dans la maison de Bahal, et ils la démolirent; ils brisèrent ses autels et ses images, et tuèrent Mattan Sacrificateur de Bahal, devant les autels.
Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.
18 Jéhojadah rétablit aussi les charges de la maison de l'Eternel, entre les mains des Sacrificateurs Lévites, que David avait distribués pour la maison de l'Eternel, afin qu'ils offrissent les holocaustes à l'Eternel, ainsi qu'il est écrit dans la Loi de Moïse, avec joie et avec des cantiques, selon la disposition qui en avait été faite par David.
Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza.
19 Il établit aussi des portiers aux portes de la maison de l'Eternel; afin qu'aucune personne souillée, pour quelque chose que ce fût, n'y entrât.
Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.
20 Il prit [ensuite] les centeniers, les hommes les plus considérables, ceux qui étaient établis en autorité sur le peuple, et tout le peuple du pays; et il fit descendre le Roi de la maison de l'Eternel, et ils entrèrent par le milieu de la haute porte dans la maison du Roi; puis ils firent asseoir le Roi sur le trône Royal.
Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi,
21 Et tout le peuple du pays fut en joie, et la ville demeura tranquille, bien qu'on eût mis à mort Hathalie par l'épée.
nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.

< 2 Chroniques 23 >