< 1 Samuel 14 >

1 Or il arriva que Jonathan, fils de Saül, dit un jour au garçon qui portait ses armes: Viens et passons vers le corps de garde des Philistins qui est au delà de ce lieu-là; mais il ne le déclara point à son père.
Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
2 Et Saül se tenait à l'extrémité du coteau sous un grenadier, à Migron, et le peuple qui était avec lui était d'environ six cents hommes.
Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
3 Et Ahija, fils d'Ahitub, frère d'I-cabod, fils de Phinées, fils d'Héli, Sacrificateur de l'Eternel à Silo, portait l'Ephod; et le peuple ne savait point que Jonathan s'en fût allé.
miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
4 Or entre les passages par lesquels Jonathan cherchait de passer jusqu'au corps de garde des Philistins, il y avait un rocher du côté de deçà, et un autre rocher du côté de delà; l'un avait nom Botsets, et l'autre Séné.
Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
5 L'un de ces rochers était situé du côté de l'Aquilon vis-à-vis de Micmas; et l'autre, du côté du Midi vis-à-vis de Guébah.
Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
6 Et Jonathan dit au garçon qui portait ses armes: Viens, passons au corps de garde de ces incirconcis; peut-être que l'Eternel opérera pour nous: car on ne saurait empêcher l'Eternel de délivrer avec beaucoup ou avec peu de gens.
Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
7 Et celui qui portait ses armes lui dit: Fais tout ce que tu as au cœur, vas-y; voici je serai avec toi où tu voudras.
Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
8 Et Jonathan lui dit: Voici nous allons passer vers ces gens, et nous nous montrerons à eux.
Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
9 S'ils nous disent ainsi: Attendez jusqu'à ce que nous soyons venus à vous, alors nous nous arrêterons à notre place, et nous ne monterons point vers eux.
Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
10 Mais s'ils disent ainsi: Montez vers nous, alors nous monterons; car l'Eternel les aura livrés entre nos mains. Que cela nous soit pour signe.
Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
11 Ils se montrèrent donc tous deux au corps de garde des Philistins, et les Philistins dirent: Voilà, les Hébreux sortent des trous où ils s'étaient cachés.
Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
12 Et ceux du corps de garde dirent à Jonathan, et à celui qui portait ses armes: Montez vers nous, et nous vous montrerons quelque chose. Et Jonathan dit à celui qui portait ses armes: Monte après moi; car l'Eternel les a livrés entre les mains d'Israël.
Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
13 Et Jonathan monta [en grimpant] de ses mains et de ses pieds, avec celui qui portait ses armes; puis ceux du corps de garde tombèrent devant Jonathan, et celui qui portait ses armes les tuait après lui.
Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
14 Et cette première défaite que fit Jonathan et celui qui portait ses armes, fut d'environ vingt hommes, [qui furent tués dans l'espace] d'environ la moitié d'un arpent de terre.
Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
15 Et il y eut un [grand] effroi au camp, à la campagne, et parmi tout le peuple; le corps de garde aussi, et ceux qui [étaient allés] ravager, furent effrayés, et le pays fut en trouble, tellement que ce fut comme une frayeur [envoyée] de Dieu.
Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
16 Et les sentinelles de Saül qui étaient à Guibha de Benjamin regardèrent; et voici, la multitude était en [un si grand] désordre qu'elle se foulait en s'en allant.
Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
17 Alors Saül dit au peuple qui était avec lui: Faites maintenant la revue, et voyez qui s'en est allé d'entre nous. Ils firent donc la revue, et voici Jonathan n'y était point, ni celui qui portait ses armes.
Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
18 Et Saül dit à Ahija: Approche l'Arche de Dieu; (car l'Arche de Dieu était en ce jour-là avec les enfants d'Israël )
Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
19 Mais il arriva que pendant que Saül parlait au Sacrificateur, le tumulte qui était au camp des Philistins s'augmentait de plus en plus; et Saül dit au Sacrificateur: Retire ta main.
Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
20 Et Saül et tout le peuple qui était avec lui, fut assemblé à grand cri; et ils vinrent jusqu'à la bataille, et voici, les Philistins avaient les épées tirées les uns contre les autres, [et il y avait] un fort grand effroi.
Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
21 Or les Philistins avaient [avec eux] des Hébreux comme [ils avaient eu] auparavant, qui étaient montés [du pays] d'alentour avec eux en leur camp, et qui se joignirent incontinent aux Israëlites qui étaient avec Saül et Jonathan.
Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Et tous les Israëlites qui s'étaient cachés dans la montagne d'Ephraïm, ayant appris que les Philistins s'enfuyaient, les poursuivirent aussi pour les combattre.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
23 Et ce jour-là l'Eternel délivra Israël, et ils allèrent en combattant jusqu'à Beth-aven.
Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
24 Mais ceux d'Israël se trouvèrent fort fatigués en ce jour-là; et Saül avait fait faire au peuple ce serment, disant: Maudit soit l'homme qui mangera d'aucune chose jusqu'au soir, afin que je me venge de mes ennemis; de sorte que tout le peuple ne goûta d'aucune chose.
Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
25 Et tout le peuple du pays vint en une forêt, où il y avait du miel qui [découlait] sur le dessus d'un champ.
Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
26 Le peuple donc entra dans la forêt, et voici du miel qui découlait; et il n'y en eut aucun qui portât sa main à sa bouche; car le peuple avait peur du serment.
Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
27 Or Jonathan n'avait point entendu son père lorsqu'il avait fait jurer le peuple, et il étendit le bout de la verge qu'il avait en sa main, et la trempa dans un rayon de miel; et il porta sa main à sa bouche, et ses yeux furent éclaircis.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
28 Alors quelqu'un du peuple prenant la parole, lui dit: Ton père a fait expressément jurer le peuple en disant: Maudit soit l'homme qui mangera aujourd'hui aucune chose; quoique le peuple fût fort fatigué.
Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
29 Et Jonathan dit: Mon père a troublé le peuple du pays. Voyez, je vous prie, comment mes yeux sont éclaircis, pour avoir un peu goûté de ce miel;
Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
30 combien plus si le peuple avait aujourd'hui mangé abondamment de la dépouille de ses ennemis, qu'il a trouvée; car la défaite des Philistins n'en aurait-elle pas été plus grande?
Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
31 En ce jour-là donc ils frappèrent les Philistins depuis Micmas jusqu'à Ajalon, et le peuple fut fort las.
Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
32 Puis il se jeta sur le butin, et ils prirent des brebis, des bœufs, et des veaux, et les égorgèrent sur la terre; et le peuple les mangeait avec le sang.
Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
33 Et on en fit rapport à Saül, en disant: Voici, le peuple pèche contre l'Eternel, en mangeant, avec le sang; et il dit: Vous avez péché, roulez aujourd'hui une grande pierre sur moi.
Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
34 Et Saül dit: Allez partout parmi le peuple, et dites-leur que chacun amène vers moi son bœuf, et chacun ses brebis; vous les égorgerez ici, vous les mangerez, et vous ne pécherez point contre l'Eternel, en mangeant avec le sang. Et chacun du peuple amena cette nuit-là son bœuf à la main, et ils les égorgèrent là.
Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
35 Et Saül bâtit un autel à l'Eternel; ce fut le premier autel qu'il bâtit à l'Eternel.
Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
36 Puis Saül dit: Descendons et poursuivons de nuit les Philistins, et les pillons jusqu'à ce que le matin soit venu, et n'en laissons pas un de reste. Et ils dirent: Fais tout ce qui te semble bon; mais le Sacrificateur dit: Approchons-nous ici vers Dieu.
Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
37 Alors Saül consulta Dieu, [en disant]: Descendrai-je pour poursuivre les Philistins? les livreras-tu entre les mains d'Israël? et il ne lui donna point de réponse en ce jour-là.
Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
38 Et Saül dit: Toutes les Tribus du peuple approchez-vous; et sachez, et voyez par qui ce péché est aujourd'hui arrivé:
Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
39 Car l'Eternel qui délivre Israël est vivant, qu'encore que cela eût été fait par mon fils Jonathan, il en mourra certainement. Et aucun de tout le peuple ne lui répondit rien.
Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
40 Puis il dit à tout Israël: Mettez-vous d'un côté, et nous serons de l'autre côté moi et Jonathan mon fils. Le peuple répondit à Saül: Fais ce qui te semble bon.
Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
41 Et Saül dit à l'Eternel le Dieu d'Israël: Fais connaître celui qui est innocent. Et Jonathan et Saül furent saisis; et le peuple échappa.
Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
42 Et Saül dit: Jetez [le sort] entre moi et Jonathan mon fils. Et Jonathan fut saisi.
Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
43 Alors Saül dit à Jonathan: Déclare-moi ce que tu as fait. Et Jonathan lui déclara et dit: Il est vrai que j'ai goûté avec le bout de ma verge que j'avais en ma main un peu de miel; me voici, je mourrai.
Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
44 Et Saül dit: Que Dieu me fasse ainsi, et ainsi y ajoute, si tu ne meurs certainement, Jonathan.
Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
45 Mais le peuple dit à Saül: Jonathan qui a fait cette grande délivrance en Israël, mourrait-il? A Dieu ne plaise! l'Eternel est vivant, si un seul des cheveux de sa tête tombe à terre; car il a aujourd'hui opéré avec Dieu. Ainsi le peuple délivra Jonathan, et il ne mourut point.
Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
46 Puis Saül s'en retourna de la poursuite des Philistins, et les Philistins s'en allèrent en leur lieu.
Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
47 Saül donc prit possession du Royaume d'Israël, et fit la guerre de tous côtes contre ses ennemis, contre Moab, et contre les enfants de Hammon, et contre Edom, et contre les Rois de Tsoba, et contre les Philistins; partout où il se tournait, il mettait tout en trouble.
Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
48 Il assembla aussi une armée, et frappa Hamalec, et délivra Israël de la main de ceux qui le pillaient.
Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
49 Or les fils de Saül étaient Jonathan, Jisui, et Malkisuah; et quant aux noms de ses deux filles, le nom de l'aînée était Mérab, et le nom de la plus jeune, Mical.
Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
50 Et le nom de la femme de Saül était Ahinoham, fille d'Ahimahats; et le nom du Chef de son armée était Abner, fils de Ner, oncle de Saül.
Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
51 Et Kis père de Saül, et Ner père d'Abner étaient fils d'Abiël.
Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
52 Et il y eut une forte guerre contre les Philistins durant tout le temps de Saül; et aussitôt que Saül voyait quelque homme fort, et quelque homme vaillant, il le prenait auprès de lui.
Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.

< 1 Samuel 14 >