< 1 Rois 5 >

1 Hiram aussi Roi de Tyr envoya ses serviteurs vers Salomon, ayant appris qu'on l'avait oint pour Roi en la place de son père; car Hiram avait toujours aimé David.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 Et Salomon envoya vers Hiram pour lui dire:
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 Tu sais que David mon père n'a pu bâtir une maison au Nom de l'Eternel son Dieu, à cause des guerres qui l'ont environné, jusqu'à ce que l'Eternel a eu mis ses [ennemis] sous ses pieds.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 Et maintenant l'Eternel mon Dieu m'a donné du repos tout alentour, et je n'ai point d'ennemis, ni d'affaire fâcheuse.
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 Voici donc je prétends bâtir une maison au Nom de l'Eternel mon Dieu, selon que l'Eternel en a parlé à David mon père en disant: Ton fils que je mettrai en ta place sur ton trône sera celui qui bâtira une maison à mon Nom.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 C'est pourquoi commande maintenant qu'on coupe des cèdres du Liban, et que mes serviteurs soient avec tes serviteurs; et je te donnerai pour tes serviteurs telle récompense que tu me diras; car tu sais qu'il n'y a point de gens parmi nous qui s'entendent comme les Sidoniens, à couper le bois.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 Or il arriva que quand Hiram eut entendu les paroles de Salomon, il s'en réjouit fort, et dit: Béni soit aujourd'hui l'Eternel, qui a donné à David un fils sage [pour être Roi] sur ce grand peuple.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 Hiram envoya donc vers Salomon pour [lui] dire: J'ai entendu ce que tu m'as envoyé dire, et je ferai tout ce que tu veux au sujet du bois de cèdre et du bois de sapin.
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 Mes serviteurs les amèneront depuis le Liban jusqu'à la mer, puis je les ferai mettre sur la mer par radeaux, jusqu'au lieu que tu m'auras marqué, et je les ferai là délier, et tu les prendras, et de ton côté tu me satisferas en fournissant de vivres ma maison.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 Hiram donc donnait du bois de cèdre et du bois de sapin à Salomon, autant qu'il en voulait.
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 Et Salomon donnait à Hiram vingt mille Cores de froment pour la nourriture de sa maison, et vingt Cores d'huile très-pure; Salomon en donnait autant à Hiram chaque année.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 Et l'Eternel donna de la sagesse à Salomon, comme l'Eternel lui [en] avait parlé; et il y eut paix entre Hiram et Salomon, et ils traitèrent alliance ensemble.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 Le Roi Salomon fit aussi une levée [de gens] sur tout Israël, et la levée fut de trente mille hommes.
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 Et il en envoyait dix mille au Liban chaque mois, tour à tour, ils étaient un mois au Liban, et deux mois en leur maison; et Adoniram [était commis] sur cette levée.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 Salomon avait aussi soixante-dix mille hommes qui portaient les faix, et quatre-vingt mille qui coupaient le bois sur la montagne;
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 Sans les Chefs des Commis de Salomon, qui avaient la charge de l'ouvrage, au nombre de trois mille trois cents, lesquels commandaient au peuple qui était employé à ce travail.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 Et par le commandement du Roi, on amena de grandes pierres, et des pierres de prix, pour faire le fondement de la maison, qui étaient toutes taillées.
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 De sorte que les maçons de Salomon, et les maçons d'Hiram, et les tailleurs de pierres taillèrent et préparèrent le bois et les pierres pour bâtir la maison.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

< 1 Rois 5 >