< Sophonie 1 >

1 Parole du Seigneur, qui vint à Sophonie, fils de Chusi, fils de Godolias, fils d'Amorias, fils d'Ézécias, durant les jours de Josias, fils d'Amon, roi de Juda.
Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
2 Que toute chose tombe de défaillance sur la face de la terre, dit le Seigneur.
Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
3 Que l'homme et les bêtes disparaissent; que disparaissent les oiseaux du ciel et les poissons de la mer; et les impies seront sans force, et Je chasserai les pécheurs de la face de la terre, dit le Seigneur.
“Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
4 Et J'étendrai Ma main sur Juda et sur les habitants de Jérusalem; et J'effacerai de ce lieu les noms de Baal et de ses prêtres,
“Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
5 et ceux qui adorent sur leurs terrasses l'armée du ciel, et se prosternent en jurant par le Seigneur, et ceux qui jurent par leur roi,
wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
6 et ceux qui s'éloignent du Seigneur, et ceux qui ne cherchent pas le Seigneur, et ceux qui ne s'attachent pas au Seigneur.
wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
7 Craignez la face du Seigneur Dieu; car le jour du Seigneur est proche, et le Seigneur a préparé Sa victoire, et Il a sanctifié Ses convives.
Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
8 Et il arrivera que, le jour du sacrifice du Seigneur, Je tirerai vengeance des princes et de la maison du roi, et de tous ceux qui ont porté des vêtements étrangers.
Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
9 Et ce jour-là Je tirerai dans les parvis une vengeance éclatante de ceux qui remplissent d'impiété et de fraude le temple du Seigneur leur Dieu.
Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
10 Et ce jour-là, dit le Seigneur, il y aura des cris à la porte des Assaillants, des hurlements à la seconde porte, et de grands brisements de cœur sur les collines.
Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
11 Pleurez, vous qui habitez cette ville abattue; car tout le peuple est devenu comme Chanaan, et tous ceux qui se glorifiaient de leur argent ont été exterminés.
Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
12 Et en ce jour-là, Je chercherai Jérusalem la lampe à la main, et Je tirerai vengeance des hommes qui méprisent Mes commandements, et qui disent en leur cœur: Le Seigneur ne fera pas de bien, Il ne fera pas de mal.
Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
13 Leur richesse sera mise au pillage, et leurs maisons en ruines. Ils se bâtiront des demeures, et ils ne les habiteront pas; ils planteront des vignes, et ils n'en boiront pas le vin.
Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
14 Car le grand jour du Seigneur est proche; il est proche, il accourt. Le bruit du jour du Seigneur est lamentable et terrible.
“Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
15 Le jour de Sa colère est un grand jour; ce jour-là est un jour d'affliction et de calamité; c'est un jour d'angoisse et d'extermination, un jour d'ombre et de ténèbres, un jour de nuages et de vapeurs.
Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
16 En ce jour-là, sur les villes fortes et sur les cimes élevées, les cris et les trompettes retentissent.
siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
17 Et J'écraserai tous les hommes, et ils marcheront comme des aveugles; car ils ont péché contre le Seigneur; et Il répandra leur sang comme la poussière, et leurs chairs comme le fumier.
Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
18 Et au jour de la colère du Seigneur, ni leur argent ni leur or ne pourront les sauver; et, dans le feu de Son zèle, toute la terre périra, car Il aura hâte d'exterminer jusqu'au dernier de tous ceux qui l'habitent.
Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”

< Sophonie 1 >