< Psaumes 22 >

1 Jusqu'à la Fin, pour la prière du matin, psaume de David. Ô Dieu, ô mon Dieu, regarde-moi; pourquoi m'as-tu délaissé? la voix de mes péchés a fait fuir mon salut.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
2 Ô mon Dieu, je crierai vers toi le jour, et tu ne m'exauceras point; je crierai la nuit, et ce n'est point folie à moi.
Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
3 Mais toi, gloire d'Israël, tu résides au lieu saint.
Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
4 Nos pères ont espéré en toi; ils ont espéré, et tu les as délivrés.
Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
5 Ils ont crié vers toi, et ils ont été sauvés; ils ont espéré en toi, et n'ont point été confondus.
Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
6 Mais moi je suis un ver de terre et non un homme; opprobre des hommes et mépris du peuple.
Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
7 Tous ceux qui m'ont vu se sont moqués de moi; ils ont murmuré entre leurs lèvres, ils ont secoué la tête.
Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
8 (Ils ont dit): Il a mis son espoir en Dieu, que le Seigneur le sauve; qu'il le délivre, puisqu'il se complaît en lui.
Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
9 C'est toi, il est vrai, qui m'as tiré des entrailles de ma mère; et, à sa mamelle, j'espérais en toi.
Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
10 Aussitôt sorti de son sein, j'ai été livré à toi; tu es mon Dieu dès le sein de ma mère.
Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
11 Ne t'éloigne point de moi; car l'affliction est proche, et nul ne me porte secours.
Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
12 Une multitude de jeunes taureaux m'investissent, des bœufs robustes m'ont entouré,
Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
13 Et ont ouvert contre moi leur bouche, comme un lion ravisseur et rugissant.
Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
14 Je me suis répandu comme de l'eau; tous mes os ont été dispersés; mon cœur dans ma poitrine est devenu comme de la cire liquide.
Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
15 Ma force s'est desséchée comme la brique; ma langue s'est collée à mon palais, et tu m'as poussé dans la poussière de la mort.
Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
16 Une multitude de chiens m'ont entouré; la synagogue des pervers m'assiège; ils m'ont percé les pieds et les mains,
Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 Ils ont compté mes os; ils m'ont observé et surveillé.
Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
18 Ils se sont partagé mes vêtements, et ils ont tiré ma robe au sort.
Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
19 Et toi, ô Seigneur, n'éloigne pas de moi ton secours, songe à ma défense.
Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
20 Délivre mon âme du glaive; délivre de la griffe des chiens mon unique.
Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
21 Tire-moi de la gueule du lion, et sauve ma faiblesse de la corne des licornes.
Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
22 Je célébrerai ton nom parmi mes frères; Je te chanterai au milieu de l'église.
Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
23 Ô vous qui craignez le Seigneur, louez-le; et toi, peuple de Jacob, glorifie-le. Que toute la race d'Israël le craigne,
Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
24 Parce qu'il n'a ni méprisé ni rebuté la prière des pauvres; parce qu'il n'a point détourné de moi son visage; parce qu'il m'a exaucé quand j'ai crié vers lui.
Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
25 Tu seras ma louange dans la grande église; j'accomplirai mes vœux devant tous ceux qui te craignent.
Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
26 Les pauvres mangeront, et ils seront rassasiés; et ceux qui cherchent le Seigneur le loueront; leurs cœurs vivront dans tous les siècles des siècles.
Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
27 Et jusqu'aux confins de la terre on se souviendra du Seigneur; on se convertira à lui; toutes les tribus des Gentils se prosterneront devant lui pour l'adorer.
Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
28 Car la royauté appartient au Seigneur; il régnera sur les nations.
kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
29 Tous les riches de la terre ont mangé et adoré; tous ceux qui descendent en la terre tomberont devant lui. Que mon âme aussi vive pour lui,
Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30 Toute ma postérité le servira. La génération future sera annoncée au Seigneur;
Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
31 On fera connaître sa justice au peuple qui doit naître, et que le Seigneur s'est préparé.
Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.

< Psaumes 22 >