< Proverbes 21 >

1 Tel est le cours de l'eau, tel est le cœur du roi dans la main de Dieu; de quelque côté qu'il veuille l'incliner, c'est là qu'Il le dirige.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Tout homme semble juste à ses yeux; mais Dieu dirige les cœurs.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Faire des choses justes et dire la vérité est plus agréable au Seigneur que le sang des victimes.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Le cœur de l'audacieux est superbe dans son insolence; la lampe des impies est le péché.
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Amasser des trésors avec une langue trompeuse, c'est poursuivre des vanités sur les filets de la mort.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 La destruction habitera avec les impies, parce qu'ils ne veulent pas pratiquer la justice.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 Devant les hommes tortueux Dieu place des voies tortueuses; car Ses œuvres sont droites et pures.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 Mieux vaut demeurer dans un carrefour en plein air, que dans une grande maison bien crépie avec l'iniquité.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 Nul homme ne sera miséricordieux pour l'âme des impies.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 La punition de l'intempérant rend l'innocent plus réfléchi; l'homme sage et intelligent en reçoit une leçon.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 Le juste pénètre le cœur des impies, et les méprise à cause de leur malice.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 Celui qui ferme l'oreille au cri du faible criera lui-même, et nul ne l'écoutera.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 Un don secret détourne les colères; celui qui épargne les présents excite de violents courroux.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 La joie du juste est de faire justice; le saint n'est pas pur aux yeux des méchants.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 L'homme qui s'égare loin des voies de la justice se reposera dans l'assemblée des géants.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 L'indigent aime la joie; il désire le vin et l'huile en abondance.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 Les déréglés sont en abomination aux justes.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 Mieux vaut habiter le désert qu'avec une femme bavarde, colère et querelleuse.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 Un trésor désirable reposera sur la bouche du sage; mais les insensés le dévorent.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 Les voies de la justice et de la miséricorde conduisent à la vie et à la gloire.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 Le sage a pris d'assaut les villes fortes; il a démoli les forteresses sur lesquelles comptaient les impies.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 Celui qui est maître de sa bouche et de sa langue garde son âme de la tribulation.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 L'homme audacieux, arrogant et présomptueux peut être appelé un fléau; le vindicatif n'est pas dans la loi.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 Les désirs tuent le paresseux; car ses mains ne se lèvent pas pour faire quoi que ce soit.
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 L'impie, durant tout le jour, a des désirs mauvais; le juste n'est avare ni de compassion ni de miséricorde.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 Les sacrifices des impies sont en abomination au Seigneur; car ils les offrent le cœur plein d'iniquité.
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 Le faux témoin périra; un homme docile parlera avec réserve.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 L'impie compose effrontément son visage; mais l'homme droit saura bien discerner ses voies.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 Il n'est point de sagesse, point de courage, point de raison chez l'impie.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 Le cheval est tout prêt pour le jour du combat; mais le secours vient de Dieu.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Proverbes 21 >