< Proverbes 17 >

1 Mieux vaut un morceau de pain avec la joie de la paix, qu'une maison pleine de biens et d'offrandes iniques avec des querelles.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Le serviteur intelligent gouvernera des maîtres insensés, et il fera les parts entre les frères.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Comme dans une fournaise on éprouve l'argent et l'or, ainsi les âmes sont élues par le Seigneur.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Le méchant obéit à la langue des pervers; le juste ne fait pas attention à des lèvres menteuses.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Railler le mendiant, c'est irriter son Créateur; celui qui se réjouit de la ruine de son prochain ne sera point innocent; celui qui a des entrailles faciles à émouvoir obtiendra miséricorde.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Les fils de ses fils sont la couronne du vieillard; les pères sont la gloire des enfants. Le fidèle a le monde entier pour richesses; l'infidèle n'a pas même une obole.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Des livres fidèles ne vont pas à l'insensé, ni des livres trompeurs au juste.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Les corrections sont, pour ceux qui les mettent à profit, une récompense de la grâce; où elles s'adressent, elles remettent dans le bon chemin.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Celui qui garde le secret sur les mauvaises actions, maintient les amitiés; celui à qui il est odieux de les cacher, sépare les amis et ceux d'une même maison.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 Une menace fait naître le repentir dans le cœur du sage; l'insensé ne sent pas même les coups de fouet.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Tout méchant excite des querelles; mais le Seigneur lui enverra un ange inexorable.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 L'homme prudent n'est pas exempt de honte; l'injuste ne songe qu'à mal.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Celui qui rend le mal pour le bien n'éloignera pas le mal de sa maison.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 L'autorité de la justice donne du pouvoir aux paroles; les séditions et les querelles précèdent la misère.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 Celui qui déclare le juste injuste, et l'injuste juste, est impur et abominable aux yeux de Dieu.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 À quoi servent ses richesses à l'insensé, puisque l'homme sans cœur ne pourra pas en acheter la sagesse? Celui qui exhausse sa maison cherche sa ruine; celui qui prend une voie mauvaise pour s'instruire tombera dans le malheur.
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Aie en tout temps un ami; que tes frères te soient secourables dans tes nécessités: c'est pour cela qu'ils sont nés.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 L'imprudent bat des mains et se complaît en lui-même, quand il s'est rendu caution d'une somme pour ses amis.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 Si l'on aime le péché, on se réjouit des querelles.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Celui qui a le cœur dur ne trouvera pas de biens. L'homme dont la langue est facilement changeante tombera dans le malheur.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Le cœur de l'insensé est pour lui un sujet de troubles. Le père ne se réjouit pas en un fils ignorant; le fils sage réjouit sa mère.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 La joie du cœur donne la santé; les os d'un homme triste se dessèchent.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Les voies de celui qui emporte des présents iniques dans les plis de son manteau ne seront point prospères; l'impie s'écarte des voies de la justice.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 Sur la face du sage brille l'intelligence; les yeux de l'insensé sont égarés aux bouts du monde.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Un fils insensé, courroux du père, douleur de la mère.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Il n'est pas bien de nuire à un homme juste; conspirer contre des princes équitables est une iniquité.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Celui qui s'abstient de paroles dures est un sage; l'homme patient est sensé.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 Si l'insensé cherche la sagesse, il sera réputé sage; et s'il ferme la bouche, il passera pour prudent.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Proverbes 17 >