< Lévitique 12 >

1 Et le Seigneur parla à Moïse, disant:
Yahweh akamwambia Musa,
2 Parle aux fils d'Israël, et dis-leur: La femme qui aura été fécondée et qui aura enfanté un garçon sera impure pendant sept jours, jours de séparation à cause du flux ordinaire.
“zungumza na watu wa Israeli, uwaambie, 'endapo mwanamke anakuwa mjamzito na kujifungua mtoto wa kiume, naye atakuwa najisi kwa muda wasiku saba, ni kama tu vile anavyokuwa najisi katika siku za kipindi chake kwa mwezi.
3 Et le huitième jour, elle circoncira son fils.
Katika siku ya nane nyama ya govi la mtoto mvulana itatahiriwa.
4 Ensuite, pendant trente-trois jours, elle restera en son sang impur; elle ne touchera à rien de saint; elle n'entrera pas dans le sanctuaire jusqu'à ce que les jours de la purification soient accomplis.
Kisha utakaso wa mama wa kutokwa damu yake utaendelea kwa muda wa siku tatu. Haimpasi kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kukaribia eneo la hema mpaka zitakapomalizika siku za kutakaswa kwake.
5 Si elle a enfanté une fille, elle sera impure deux fois sept jours à cause du flux ordinaire, et pendant soixante-six jours, elle restera dans son sang impur.
Lakini kama atajifungua mtoto wa kike, naye atakuwa najisi kwa mud wa majuma mawili, kama alivyo wakati wa kipindi chake. Kisha utakaso wa mama utaendelea kwa siku sitini sita.
6 Et lorsque les jours de sa purification seront accomplis, qu'elle ait enfanté un garçon ou une fille, elle offrira au prêtre, en holocauste, devant la porte du tabernacle du témoignage, un agneau sans tache, et pour le péché une petite colombe avec une tourterelle.
Siku za kutakaswa kwake zitakapoisha, kwa ajili ya mwana au binti, atalazimika kuleta kwa kuhani mwana-kondoo wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au huwa kuwa sadaka ya dhambi, mbele ya ingilio la hema la kukutania,
7 Et le prêtre sacrifiera les hosties au Seigneur; il priera pour elle, et il la purifiera de la fontaine de son sang; telle est la loi pour celle qui aura enfanté un fils ou une fille.
Kisha atawatoa mbele za Yahweh na kufanya sadaka ya upatanisho kwa ajili yake, naye atatakaswa kutokana kutiririka kwa damu yake. Hii ndiyo sheria kuhusu mwanamke aifunguaye ama mtoto wa kiume au wa kike.
8 Si ses facultés sont insuffisantes pour qu'elle donne un agneau, elle prendra deux tourterelles ou deux petits de colombes, qui seront: l'un l'holocauste, l'autre la victime du péché; et le prêtre priera pour elle, et elle sera purifiée.
Na kama hana uwezo wa kutoa mwana-kondoo, naye ataleta makinda mawili ya njiwa ua hua, mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kuwa sadaka ya dhambi, naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake; naye atakuwa safi.”

< Lévitique 12 >