< Isaïe 40 >

1 Consolez, consolez mon peuple, dit le Seigneur;
Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Prêtres, parlez au cœur de Jérusalem; consolez-la, car son humiliation est accomplie; son péché lui est remis, parce qu'elle a reçu de la main du Seigneur un châtiment double de ses péchés.
Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
3 On entend la voix de celui qui crie dans le désert: Préparez la voie du Seigneur, redressez les sentiers de notre Dieu.
Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
4 Toute vallée sera remplie, toute montagne sera abaissée; les chemins tortueux seront redressés, ceux qui étaient raboteux seront aplanis.
Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
5 Et la gloire du Seigneur se manifestera, et toute chair verra le salut de Dieu; car le Seigneur a parlé.
Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
6 Une voix m'a dit: Crie; et j'ai répondu: Que crierai-je? Toute chair est de l'herbe; toute gloire humaine est comme la fleur des champs.
Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
7 L'herbe s'est desséchée, et la fleur est tombée.
Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
8 Mais la parole de notre Dieu subsistera dans tous les siècles.
Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9 Ô toi qui annonce à Sion la bonne nouvelle, monte sur le sommet de la montagne; élève la voix de toutes tes forces, toi qui annonce à Jérusalem la bonne nouvelle; dis-leur: Glorifiez-vous, ne craignez point; dis aux villes de Juda: Voilà votre Dieu.
Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
10 Voilà le Seigneur, le Seigneur vient avec la force, son bras a la puissance; voilà dans ses mains le salaire, et l'œuvre est devant ses yeux.
Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
11 Il fera paître son troupeau comme un pasteur; il rassemblera les agneaux, et il encouragera les brebis pleines.
Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
12 Qui a mesuré les eaux à la main, le ciel à la palme, et toute la terre à la poignée? Qui a placé les montagnes dans une balance? Qui a pesé les forêts?
Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
13 Qui sait la pensée du Seigneur? Qui a tenu conseil avec lui pour l'instruire?
Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
14 Avec qui a-t-il tenu conseil, et qui l'a instruit? Qui lui a enseigné le jugement? Qui lui a montré la voie de la sagesse?
Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
15 Est-ce que toutes les nations ne sont pas à ses yeux comme la goutte d'eau qui s'échappe du vase? comme l'oscillation d'une balance? Ne seront- elles pas à ses yeux comme un peu de salive?
Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
16 Le Liban ne suffirait pas pour un bûcher; tous les quadrupèdes ne suffiraient pas pour un holocauste.
Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
17 Toutes les nations sont comme un néant; elles sont comptées comme un néant à ses yeux.
Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
18 A qui avez-vous comparé le Seigneur? A quel simulacre l'avez-vous assimilé?
Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
19 Est-ce qu'un artisan a jamais fait son image? Est-ce qu'un fondeur, en jetant de l'or dans un moule, l'a fait en or et a reproduit sa ressemblance?
Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
20 L'ouvrier a choisi un bois incorruptible; puis il cherche avec soin de quelle manière il posera sa statue, pour qu'elle ne soit point ébranlée.
Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
21 Ne savez-vous pas cela? Ne l'avez-vous pas ouï dire? Ne vous l'a-t-on pas appris dès le commencement? Ne connaissez-vous pas les fondements de la terre?
Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
22 C'est lui qui tient dans sa main le cercle de la terre, et, comme une nuée de sauterelles, tous ceux qui l'habitent. C'est lui qui a posé les cieux comme une voûte, et qui les a tendus comme la tente où l'on s'abrite.
Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
23 C'est lui par qui règnent les princes, qui sont comme un néant devant lui. C'est lui qui a créé la terre et la regarde comme un néant.
Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
24 Car ces princes ne planteront pas, ils ne sèmeront pas, et leur racine ne prendra pas en terre. Il a soufflé sur eux, et ils se sont desséchés; la tempête les emportera comme des broussailles.
Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
25 Maintenant donc, à qui m'avez-vous comparé, pour que je m'en glorifie? dit le Saint.
“Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
26 Levez les yeux et voyez; qui vous a montré toutes ces choses? C'est celui qui a produit les innombrables ornements des cieux qui dans sa gloire les appelle tous par leur nom, et qui, dans la plénitude de sa puissance, ne vous a rien caché.
Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
27 Et toi, qu'as-tu dit, Jacob? Pourquoi as-tu ainsi parlé, Israël? Ma voix est ignorée de Dieu, et mon Dieu m'a retiré sa justice, et il s'est éloigné.
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
28 Et maintenant n'as-tu pas appris, n'as-tu pas entendu? Dieu, c'est l'Éternel; c'est Dieu qui a assigné des limites à la terre; il ne sentira jamais la faim ni la fatigue; et il n'y a pas à pénétrer sa sagesse.
Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
29 C'est lui qui donne la force aux affamés, et non la tristesse à ceux qui sont dans la douleur.
Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
30 Car les adolescents auront faim, les jeunes gens seront fatigués, les hommes d'élite seront affaiblis.
Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
31 Mais ceux qui attendent le Seigneur trouveront des forces nouvelles; il leur poussera des ailes comme aux aiglons; ils courront, et ne seront point fatigués; ils marcheront, et n'auront pas faim.
bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

< Isaïe 40 >