< Isaïe 17 >

1 Voilà que Damas va être retranchée du nombre des villes; elle sera en ruines,
Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
2 Abandonnée pour toujours; les menus troupeaux s'y reposeront, et nul ne sera là pour les en chasser.
Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 Et il n'y aura plus de forteresse où Ephraïm puisse se réfugier; et il n'y aura plus de royauté pour Damas, ni pour le reste des Syriens. Car tu ne vaux pas mieux que les fils d'Israël; ta gloire ne vaut pas mieux que leur gloire: voilà ce que dit le Seigneur des armées.
Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 En ce jour, la gloire de Jacob sera obscurcie, et les richesses qui font sa gloire seront ébranlées.
“Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
5 Et ce sera comme lorsque un homme glane ou ramasse les grains des épis dans une vallée féconde.
Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
6 Et des glanures y ont été laissées, comme les trois ou quatre olives de rebut qu'on laisse à la cime de l'arbre, comme les quatre ou cinq qui restent au bout des branches: voilà ce que dit le Seigneur, Dieu d'Israël.
Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
7 Ce jour-là, l'homme mettra sa confiance en son Créateur; il tournera ses yeux vers le Saint d'Israël.
Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 Et ils ne croiront plus à leurs autels, ni aux ouvrages de leurs mains que leurs doigts ont façonnés; ils ne regarderont plus leurs bois sacrés ni leurs abominations.
Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
9 En ce jour tes villes seront abandonnées, comme le furent celles des Amorrhéens et des Hévéens, en présence des fils d'Israël; et elles seront désertes,
Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
10 Parce que tu as délaissé Dieu ton Sauveur, et que tu ne t'es plus souvenu du Seigneur qui t'avait secouru; et, à cause de cela, tu planteras des arbres trompeurs et des graines infidèles.
Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
11 Le jour où tu planteras, tu seras déçu. Si tu sèmes le matin, ta semence fleurira pour être moissonnée le jour où tu laisseras ton héritage, et où, comme le père de l'homme, tu distribueras ton patrimoine à tes fils.
hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
12 Malheur à la multitude des nations! Comme une mer agitée, ainsi vous serez bouleversées; et leurs armes retentiront sur leur dos, comme des vagues.
Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
13 Cette multitude ressemblera à des flots tumultueux, à des ondes emportées par le vent. Le Seigneur exterminera le peuple assyrien, et il le rejettera au loin, comme au moindre souffle vole la paille légère des vanneurs, ou le tourbillon de poussière que soulève un ouragan.
Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
14 Sa douleur durera jusqu'au soir, et avant l'aurore il ne sera plus. Tel sera le partage de ceux qui ont fait de vous leur proie; tel sera l'héritage de ceux qui ont pris possession de vous.
Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.

< Isaïe 17 >