< Ézéchiel 46 >

1 Voici ce que dit le Seigneur Dieu: La porte du parvis intérieur qui regarde l'orient sera fermée les six jours de travail; elle sera ouverte les jours du sabbat et à chaque nouvelle lune.
Bwana Yahwe asema hivi: Lango la uzio wa ndani, linaloelekea mashariki, litafungwa kwa mda wa siku sita za kazi, lakini katika siku za Sabato litakuwa wazi, na katika siku ya mwezi mpya litafunguliwa.
2 Et le prince entrera par le chemin du vestibule de la porte intérieure, et il s'arrêtera au seuil de la porte, et les prêtres prépareront ses holocaustes et ses hosties pacifiques. Et il adorera au seuil même de la porte, puis il sortira, et la porte ne sera pas fermée jusqu'au soir;
Mwana wa mfalme ataingia kwa kutumia lango la njia ya nyuma ya varanda upande wa nje, na atasimama mbele ya muhimili wa mwimo wa lango la ndani wakati makuhani wakiwa wakitengeza sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani. Kisha ataabudu kwenye kizingiti cha lango la ndani na kutoka nje, lakini lango halitakuwa linafungwa hadi jioni.
3 Et le peuple de la terre adorera près de cette porte, et il se prosternera devant le Seigneur, les jours de sabbat et de nouvelle lune.
Watu wa nchi pia wataabudu mbele ya Yahwe kwenye hili lango la kuingilia katika siku ya Sabato na siku mpya za mwezi.
4 Et le prince offrira les jours de sabbat, en holocauste au Seigneur, six agneaux sans tache et un bélier sans tache,
Sadaka ya kuteketezwa ambayo mwana wa mfalme aitoayo kwa Yahwe katika siku ya Sabato itakuwa wanakondoo sita wasiokuwa na dosari na kondoo dume asiyekuwa na dosari.
5 Et l'oblation d'un gâteau pour le bélier, et un don volontaire de sa main par agneau; et il y aura dans le gâteau un hin d'huile.
Sadaka ya unga pamoja na kondoo dume itakuwa efa moja, na sadaka ya unga pamoja na wanakondoo kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta pamoja na kila efa ya unga.
6 Et il offrira, le jour de la nouvelle lune, un veau sans tache, et six agneaux et un bélier sans tache.
Katika siku ya mwezi mpya atatoa ng'ombe mchanga asiyekuwa na dosari kutoka kuchungwa, wanakondoo sita, na kondoo asyekuwa na dosari.
7 Et il y aura un gâteau pour le bélier; et le gâteau pour le veau, comme pour les agneaux, sera une oblation; il donnera par agneau selon le pouvoir de sa main, et il y aura un hin d'huile dans le gâteau.
Atatengeneza sadaka ya unga ya efa moja kwa ajili ya ng'ombe na efa moja kwa ajili ya kondoo, na kwa kiasi awezacho kukitoa kwa ajili ya wanakondoo, na hini ya mafuta kwa kila efa ya unga.
8 Et lorsque le prince entrera dans le temple, il passera par le chemin du vestibule du parvis, et il sortira par le chemin de la porte.
Wakati mwana wa mfalme atakapokuwa anaingia kwa njia ya lango lenye varanda, ataondoka kwa njia hiyo hiyo.
9 Et lorsque le peuple de la terre viendra devant le Seigneur, celui qui arrivera les jours de fête pour adorer par le chemin de la porte qui regarde l'aquilon, sortira par la porte du midi; et celui qui arrivera par le chemin de la porte du midi sortira par la porte de l'aquilon; nul ne s'en ira par le chemin qu'il aura pris pour entrer, mais il marchera droit devant lui pour sortir.
Lakini wakati watu wa nchi watakakuja kwa Yahwe katika sikukuu zilizoteuliwa, kila mmoja kuingia kupitia kwenye lango la kaskazini kuabudu ataondoka kupitia lango la kusini; na kila atakayeingillia kupitia lango la kusini atatoka kupitia lango la kaskazini. Hakuna atakayerudia kwa lile lango aliloingilia, kwa kuwa atatoka nje moja kwa moja.
10 Et le prince au milieu d'eux entrera avec eux quand ils entreront, et il sortira quand ils sortiront.
Mwana wa mfalme atakuwa kati yao; watakapoingia, ataingia ndani, na watakapoondoka, atatoka nao.
11 Et aux fêtes et aux solennités générales il y aura oblation d'un gâteau par veau et d'un gâteau par bélier; et le prince donnera par agneau selon le pouvoir de sa main, et il y aura un hin d'huile par gâteau.
Kwenye sikukuu hizo, sadaka ya unga itakuwa efa moja ya unga kwa ng'ombe mmoja na efa moja kwa kondoo dume, na chochote atakacho kitoa pamoja na wanakondoo, na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
12 Si le prince prépare en action de grâces un holocauste pacifique au Seigneur, il ouvrira pour lui seul la porte qui regarde l'orient, et il préparera l'holocauste et les hosties pacifiques, comme il fait le jour du sabbat; puis il sortira, et en sortant il fermera les portes.
Wakati mwana wa mfalme atakapotoa sadaka atakayojisikia kutoa, labda sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani kwa Yahwe, lango la kuelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka ya amani kama afanyavyo siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, na baada ya kutoka lango litafungwa.
13 Et chaque jour, dès le matin, il offrira en holocauste au Seigneur un agneau d'un an sans tache.
Kwa kuongeza, utatoa mwanakondoo asiyekuwa na dosari mwenye umri wa mwaka mmoja kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe kila siku; utafanya hivi kila asubuhi.
14 Et il fera dès le matin, pour cet agneau d'oblation d'un sixième d'éphi de fleur de farine et du tiers d'un hin d'huile pour y être mêlée; cette oblation au Seigneur sera de règle perpétuelle.
Utatoa sadaka ya unga pamoja nayo kila asubuhi, efa sita na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta kuchanganya na sadaka ya unga kwa ajili ya Yahwe, kulingana na sheria ilivyo.
15 Vous sacrifierez l'agneau, et vous offrirez dès le matin l'huile et la farine; cet holocauste sera perpétuel.
Watandaa mwanakondoo, sadaka ya kuteketezwa, na mafuta kila asubuhi, sadaka ya kuteketezwa ya kudumu.
16 Voici ce que dit le Seigneur: Si le prince fait sur sa part de bien un don à l'un de ses fils, celui-ci le transmettra à ses fils comme héritage.
Bwana Yahwe asema hivi: Kama mwana wa mfalme akitoa zawadi kwa mmoja wa watoto wake, imekuwa urithi wake. Itakuwa mali ya mtoto wake, imekuwa urithi.
17 S'il fait un don à l'un de ses serviteurs, celui-ci ne le possèdera que jusqu'à l'année du jubilé, et alors il le rendra au prince; quant à ce qui est possédé par ses fils, c'est à eux que la possession continuera d'appartenir.
Lakini kama akimpatia zawadi kutoka urithi wake kwa mmoja wa watumishi wake, kisha itakuwa ya huyo mtumishi mpaka mwaka wa uhuru, na kisha itarudi kwa mwana wa mfalme. Urithi wake yamkini ukawa kwa ajili ya watoto wake.
18 Et le prince ne prendra rien de l'héritage du peuple: il se gardera de l'opprimer; il fera part à ses fils de ce que lui-même possède, afin que nul de mon peuple ne soit expulsé de son héritage.
Mwana wa mfalme hatawaondolea urithi wa watu kutoka kwenye mali zao wenyewe; ataandaa kwa ajili ya watoto wake mali ili kwamba watu wangu wasitawanyike, kila mtu kutoka mali kwenye yake mwenyewe.”
19 Et l'homme me conduisit derrière la porte à la chambre des miels, consacrée aux prêtres, qui regarde l'aquilon; et là était un lieu réservé.
Kisha yule mtu akaniletea kwenye lango la kutokea hata kwenye vyumba vitakatifu kwa ajili ya makuhani, vilivyokuwa vimeelekea kaskazini na tazama! Kulikuwa na sehemu mbele magharibi.
20 Et il me dit: Voici le lieu où les prêtres feront cuire les victimes pour le péché et pour l'inadvertance; ils y feront cuire aussi tous les gâteaux de l'oblation, afin de ne les point emporter dans le parvis extérieur, quand ils purifieront le peuple.
Akanambia, “Hii ndio sehemu ambayo makuhani watakapo chemshia sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na walipookea sadaka ya unga. Wasilete sadaka nje ya uzio, kwa kuwa watu watatakaswa.”
21 Et l'homme me conduisit au parvis extérieur, et il me fit faire le tour de ses quatre côtés, et là il y avait une cour à chacun de ses côtés.
Kisha akanileta kwenye uzio wa nje akaniongoza kuzunguka pembe nne za uzio, nikaona kwamba katika kila pembe ya uzio kulikuwa na uwanja.
22 Il y avait quatre petites cours, une par côté, toutes longues, pareillement de quarante coudées, larges de trente.
Katika hizo pembe nne za nje ya uzio kulikuwa na nzio nne ndogo, dhiraa arobaini urefu na thelathini upana. Ukubwa ule ule kwa nzio zote nne.
23 Et à l'entour de chacune il y avait des chambres; et au-dessous des chambres les cuisines étaient bâties alentour.
Kulikuwa na safu zilizokuwa zimetengenezwa kwa mawe kuzizunguka zote nne, na meko ya kupikia ilikuwa chini ya safu ya jiwe.
24 Et il me dit: Voici les demeures des cuisiniers; c'est ici que les desservants du temple feront cuire les offrandes du peuple.
Yule mtu akanambia, “Hizi ndizo sehemu ambazo watumishi watachemshia dhabihu za watu.”

< Ézéchiel 46 >