< Ézéchiel 26 >

1 Et en l'année onzième, le premier jour du mois, la parole du Seigneur me vint, disant:
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils de l'homme, en punition de ce que Tyr a dit de Jérusalem: C'est bien! elle est brisée, son peuple a péri, son trafic est revenu à moi; elle qui était remplie, la voilà vide;
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 En punition de cela, ainsi dit le Seigneur: Voilà que je suis contre toi, Tyr, et je conduirai coutre toi maintes nations, comme la mer monte avec ses vagues.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Et elles abattront tes remparts, ô Tyr, et elles abattront tes tours; et je vannerai loin d'elle sa poussière, et je ferai d'elle une roche nue.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Elle sera au milieu de la mer un lieu à faire sécher les filets; car c'est moi qui ai parlé, dit le Seigneur. Et elle sera livrée en proie aux nations.
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 Et ses filles, dans les champs, périront par le glaive, et elles sauront que je suis le Seigneur.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 Car ainsi dit le Seigneur: Voilà que de l'aquilon je conduis contre toi, Tyr, Nabuchodonosor, roi de Babylone; il est le roi des rois, avec des chevaux et des chars, et des cavaliers, et un rassemblement de maintes nations.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Il fera périr tes filles par le glaive dans les champs; il placera contre toi des gardes avancées; il bâtira autour de toi des forts; il t'enveloppera de palissades; il t'entourera de camps; il lancera devant toi ses javelines.
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 Il renversera de ses glaives tes remparts et tes tours.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 À cause de la multitude de ses chevaux, tu seras couverte de poussière par le fracas de ses cavaliers et des roues de ses chars; tes murs seront ébranlés quand il franchira tes portes, comme on franchit dans la plaine l'entrée d'une ville.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 Les sabots de ses coursiers fouleront toutes tes places, et il passera ton peuple au fil de l'épée, et tout ce qui fait ta force, il le renversera par terre.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Et il pillera tes richesses, et il enlèvera tes marchandises; il abattra tes murs; il détruira tes maisons si convoitées, et il jettera au fond de la mer qui te baigne tes pierres, tes bois et ta poussière.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Et il fera cesser tes nombreux concerts, et on n'entendra plus la voix de tes harpes.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Et je ferai de toi une roche nue, un lieu à faire sécher les filets, et tu ne seras plus rebâtie; car moi, le Seigneur, j'ai parlé, dit le Seigneur.
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 Car voici ce que dit à Tyr le Seigneur Maître: Les îles ne trembleront-elles pas au bruit de ta chute, quand tes blessés gémiront et que le glaive sera tiré au milieu de toi?
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Et tous les rois des nations maritimes descendront de leur trône, et ils déposeront leurs mitres de leurs têtes, et ils se dépouilleront de leurs vêtements brodés. Ils seront frappés de stupeur; ils s'asseyeront à terre, et ils craindront de périr, et ils gémiront sur toi.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Et ils feront de toi un sujet de lamentation, et ils te diront: Comment as-tu cessé de sillonner la mer, ô ville si célèbre, toi qui inspirais ta crainte à tous ceux qui demeurent sur tes rives?
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Et les elles trembleront au jour de ta chute.
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 Car voici ce que dit le Seigneur Maître: Lorsque j'aurai fait de toi une solitude comme des villes qui ne seront plus habitées, quand j'aurai fait passer sur toi l'abîme, et que les grandes eaux te couvriront,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 Je te précipiterai parmi ceux qui sont tombés dans le gouffre, chez le peuple éternel, et je te placerai au plus profond de la terre, comme en un désert éternel parmi ceux qui sont tombés dans le gouffre, afin que tu ne sois plus habitée; et tu ne reviendras plus sur la terre des vivants.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Je te perdrai, et tu ne subsisteras plus dans les siècles, dit le Seigneur Maître.
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 26 >