< Ecclésiaste 7 >

1 Bon renom vaut mieux que bon parfum; le jour de la mort vaut mieux que le jour de la naissance.
Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.
2 Il vaut mieux aller à la maison du deuil qu'à la maison du festin, puisque le deuil est la fin de tout homme, et que le vivant donnera ainsi de bons avertissements à son cœur.
Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.
3 La tristesse vaut mieux que le rire; parce que, par la tristesse du visage, le cœur deviendra bon.
Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.
4 Le cœur des sages est à la maison des pleurs; le cœur des insensés est à la maison d'allégresse.
Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.
5 Mieux vaut écouter la réprimande d'un sage, que d'entendre le chant des insensés.
Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
6 Le rire des insensés est comme le pétillement des épines sous une chaudière; et cela encore est vanité.
Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Hili nalo pia ni ubatili.
7 La calomnie trouble le sage, et lui fait perdre sa force d'âme.
Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, nayo rushwa huuharibu moyo.
8 La fin du discours vaut mieux que le commencement; un homme patient vaut mieux qu'un esprit présomptueux.
Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, uvumilivu ni bora kuliko kiburi.
9 Ne t'abandonne pas trop vite au souffle de la colère; car la colère réside dans le sein des insensés.
Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
10 Garde-toi de dire: Comment se fait-il que les jours d'autrefois ont été meilleurs que ceux d'à présent? Car il n'est point sage de s'enquérir de ces choses.
Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.
11 La sagesse est bonne, unie aux richesses; elle est alors profitable à ceux qui vivent sous le soleil.
Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema na huwafaidia wale walionalo jua.
12 Car on s'abrite à l'ombre de la sagesse, comme à l'ombre de l'argent; mais l'avantage de la science et de la sagesse, c'est qu'elles font vivre celui qui les possède.
Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, lakini faida ya maarifa ni hii: kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.
13 Considère les œuvres de Dieu; car qui pourrait redresser celui que Dieu a courbé?
Tafakari kile Mungu alichokitenda: Nani awezaye kunyoosha kile ambacho yeye amekipinda?
14 Au jour de la prospérité vis dans le bien-être, et prévois le jour du malheur; prévois-le: car Dieu a fait telle chose concordant avec telle autre, à cause des propos des hommes, afin qu'ils ne trouvent rien à blâmer en Lui.
Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.
15 J'ai vu toutes choses au jour de ma vanité. Le juste meurt avec sa justice; l'impie subsiste avec sa perversité.
Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.
16 Ne sois pas juste à l'excès; ne soit point sage plus qu'il ne faut, de peur que tu ne sois confondu.
Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usiwe na hekima kupita kiasi: kwa nini kujiangamiza mwenyewe?
17 Mais ne sois pas non plus impie ni obstiné à l'excès, de peur que tu ne périsses avant le temps.
Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?
18 Il est bon que tu t'attaches à telle chose, et que tu t'éloignes de telle autre, pour ne point souiller tes mains; car tout vient à ceux qui craignent Dieu.
Ni vyema kushika hilo moja na wala usiache hilo jingine likupite. Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.
19 La sagesse sera utile au sage plus que dix des plus puissants de la cité.
Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi kuliko watawala kumi katika mji.
20 Car il n'est point sur la terre de juste qui fasse le bien, et ne pèche.
Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.
21 Mais ne dépose pas en ton cœur toutes les paroles que dirent les impies, de peur que tu n'entendes ton serviteur te maudire.
Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, la sivyo, waweza kumsikia mtumishi wako akikulaani:
22 Car maintes fois il t'irritera, et il t'affligera de bien des manières; car toi-même aussi tu as maudit les autres.
kwa kuwa unafahamu moyoni mwako kwamba wewe mwenyewe mara nyingi umewalaani wengine.
23 J'ai éprouve toutes choses en ma sagesse, et j'ai dit: Je serai sage; et la sagesse s'est éloignée de moi.
Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, “Nimeamua kuwa na hekima”: lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.
24 Elle était plus loin encore qu'auparavant; l'abîme entre nous était profond: qui le sondera?
Vyovyote hekima ilivyo, hekima iko mbali sana na imejificha, ni nani awezaye kuigundua?
25 Pour moi, j'ai tourné autour de toutes choses, et j'ai appliqué mon esprit à les apprendre, à les examiner avec soin, à chercher la sagesse et la raison des choses, à connaître la démence de l'impie, et ses agitations et son inquiétude.
Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, kuchunguza na kuitafuta hekima na kusudi la mambo, na ili kuelewa ujinga wa uovu, na wazimu wa upumbavu.
26 Et j'ai trouve cette démence, et je la dis plus amère que la mort; de même est la femme que le veneur poursuit comme une proie, tandis que son cœur est un filet, et qu'elle tient des chaînes en sa main. L'homme bon en face du Seigneur fuira loin d'elle, et le pécheur y sera pris.
Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, mwanamke ambaye ni mtego, ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea na mikono yake ni minyororo. Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, bali mwenye dhambi atanaswa naye.
27 Voilà ce que j'ai trouvé, dit l'Ecclésiaste, en prenant les choses une à une, pour en découvrir la raison.
Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:
28 Mon âme l'a cherchée cette raison, et je ne l'ai point trouvée, et j'ai trouvé un homme sur mille; mais parmi toutes les femmes, je n'en ai pas trouvé une seule.
ningali natafiti lakini sipati: nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.
29 Seulement voici ce que j'ai trouvé: Dieu a créé l'homme droit, et les hommes ont cherché une multitude de raisons.
Hili ndilo peke yake nililolipata: Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”

< Ecclésiaste 7 >